Yanga Thread

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Pointi 5 zaipa Kiburi Yanga Kusepa na Ubingwa.​

YANGA-9-1.jpg


MABINGWA mara 27 wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga wameweka wazi kuwa pointi 5 ambazo wamewapita wapinzani wao Simba ni nyingi na zinawapa nguvu ya kuweza kutwaa ubingwa.
Yanga wanaongoza ligi wakiwa na pointi 36 baada ya kucheza mechi 14 huku mabingwa watetezi Simba wakiwa na pointi 31 baada ya mechi 15, tofauti ya pointi tano na Yanga ambao wana mchezo mmoja mkononi.
Akizungumza na Championi Jumamosi, Mkuu wa Kitengo cha Habari ndani ya Yanga, Hassan Bumbuli alisema kuwa pointi tano walizonazo kibindoni sio chache zinawapa hali ya kujiamini na nguvu ya kutwaa ubingwa.
“Tunaongoza ligi ipo wazi na tumewaacha wapinzani wetu kwa tofauti ya pointi tano, hizo sio za kubeza zinatupa nguvu ya kuweza kusaka ubingwa wa ligi na tunahitaji kuweza kutwaa kwa kuwa tumejipanga.
“Wachezaji wapo tayari na benchi la ufundi linaendelea kuwapa mbinu wachezaji, mapumziko yamekwisha kila mmoja kwa sasa yupo kambini kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wetu ujao na haitakuwa kazi rahisi kupata ushindi lakini tupo tayari kwa ajili ya kupata matokeo,” alisema Bumbuli.
Mchezo ujao wa Yanga kwenye ligi ni dhidi ya Mtibwa Sugar unatarajiwa kuchezwa Februari 23, Uwanja wa Manungu, Morogoro.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

YANGA YALIA MASHABIKI WAKE KUDUNDWA NA SIMBA.​

KLABU ya Yanga imelaani kitendo cha mashabiki wake kupigwa na mashabiki wa Simba Jumapili Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
AVvXsEjMPkiGDeBME6qFyZMX-L5zbC1cNcvfw-rysMJWn-m1nsUVI6lT1-PZawIpp0WeHnDf3UIwImuMdde_j53PGwhXLD7tiTCofoXNhNJxoqS2S7sBVBTqZlAgpMrsGRX1wEzP9v6CcP3RBSA23dssPx9shNMswz-IHS8S0hjv-qqiqG9OfO0Rkwe409pz=w640-h640
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Yacouba anarejea mdogomdogo Yanga.​

yacouba-songne-of-yanga-sc_wtewwt5qusg71mdkjhyn93jid-1.jpg

KIUNGO wa Yanga, Yacouba Songne, yupo kwenye hatua za mwisho za kuimarika afya yake kabla ya kuungana na timu na kufanya mazoezi ya pamoja kwa ajili ya mechi za Ligi Kuu na Kombe la Shirikisho la Azam Sports (ASFC).
Yacouba kwa sasa yupo kwenye program maalumu chini ya kocha wa viungo ambayo inamrejesha taratibu kwenye hali yake ya kawaida na huenda wiki ijayo ataungana na wenzake katika viwanja vya mazoezi.
Mkurugenzi wa Mashindano wa Yanga, Thabity Kandoro, aliliambia Championi Jumatatu kuwa alikuwepo kwenye uwanja wa mazoezi juzi na aliona namna ambavyo Yacouba anatia matumaini na anaonyesha amebakiza siku chache ili aweze kurejea uwanjani.
“Yacouba huenda wiki ijayo akaanza mazoezi ya uwanjani, kwa maana nilivyomuona juzi anaonekana hana muda mrefu. Kwa sasa yupo chini ya program ya kocha wa viungo na huenda wiki ijayo akaungana na wenzake,” alisema.
Yacouba yupo nje ya uwanja kwa muda sasa akiuguza majeraha ya goti ambayo aliyapata kwenye mechi ya ligi na kulazimika kufanyiwa upasuaji.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Yanga yeyote anakupiga, Nabi akusanya washambuliaji 15.​

yanga pic

JESHI la Yanga lipo kambini Avic, Kigamboni likijiwinda na mechi ya michuano ya Kombe la Shirikisho (ASFC) dhidi ya Biashara United, kabla ya kuliamsha tena katika Ligi Kuu, huku ikibainika namna Kocha Nasreddine Nabi alivyo mjanja.
Yanga Jumanne itarudi uwanjani kuvaana na Biashara katika mechi ya 16 Bora, jijini Dar es Salaam, ikiwa kwenye mawindo yao ya kutaka kubeba mataji ya michuano pekee iliyonayo mkononi kwa sasa, Ligi Kuu iliyolikosa kwa misimu minne mfululizo na lile la ASFC misimu mitano mfululizo. Yanga ilibeba ASFC msimu wa 2015-2016 wakati katika ligi ni 2016-2017.
Katika kuhakikisha wanafanikisha jambo lao kwa msimu huu, mabosi wa Yanga chini ya maelekezo ya kocha wao, Nabi imesajili jumla ya washambuliaji 15 na hadi sasa wameshatupia mabao 23 katika ligi na mengine matano ya ASFC.
Washambuliaji hao wanaojumuisha viungo washambuliaji, mawinga na mastraika ni pamoja na wale wapya wakiongozwa na Heritier Makambo, Fiston Mayele, Jesus Moloko, Chico Ushindi, Salum Abubakar ‘Sure Boy’, Khalid Aucho, Yusuf Athuman, Denis Nkane na Crispin Ngushi.
Awali kulikuwa na Deus Kaseke, Dickson Ambundo, Saido Ntibazonkiza, Feisal Salum ‘Fei Toto’, Yacouba Songne na Mapinduzi Balama aliyekuwa majeruhi wa muda mrefu kabla ya kurejea uwanjani hivi karibuni.
Uwepo wa washambuliaji wengi umefanya kila eneo kuwa na wachezaji watatu wa maana hali iliyomrahisishia Nabi hata pale mchezaji mmoja anapokosekana kwani mbadala wake anakuwepo.
Mayele ndiye kinara wa mabao kwenye kikosi akiwa nayo sita, kati ya 23 ya timu yake katika ligi, huku akiwa na jingine moja kwenye ASFC, akifuatiwa na Saido Ntibazonkiza na Fei Toto wenye manne kila mmoja, Moloko, Aucho wenye matatu kila mmoja, huku Dickson Ambundo akiwa na moja sawa na beki Djuma Shaban na kiungo mkabaji aliyetimka TP Mazembe ya DR Congo, Mukoko Tonombe.
Nkane aliyesajiliwa kutoka Biashara, hajafunga lakini alitua akiwa na mabao mawili katika ligi, huku Ngushi naye akiwa na matatu aliyotoka nayo Mbeya Kwanza kuonyesha nao gari likiwaka Yanga itakuwa moto mkali zaidi.

TIZI KALI
Huko kambini Avic, Yanga imeendelea kujifua na mastaa wake wakionyesha kuwa na mzuka mwingi kwa mechi zijazo.
Mechi dhidi ya Biashara ni ya tatu kwa timu hizo kukutana katika ASFC itapigwa kuanzia saa 1 usiku, ili kuamua timu ipi ya kwenda robo fainali. Katika mechi za awali Yanga iliishinda Biashara katika 16 Bora ya 2019-2020 kwa penalti baada ya dakika 90 kuisha kwa sare ya 2-2 kisha msimu uliopita kuing’oa nusu fainali kwa 1-0.
Kocha Nabi ameonekana kuvutiwa na nyota wake wanavyojituma mazoezini na kutimiza kile anachowaelekeza na wasaidizi wake.

WADAU WAFUNGUKA
Mshambuliaji wa zamani Yanga, Herry Morris alisema kikosi hicho kwa misimu mitatu kilikuwa hakina washambuliaji wazuri, walipokuwepo wakipata majeraha ilikuwa changamoto tofauti na sasa.
Morris alisema nyuma eneo la ulinzi lilikuwa hakuna tabu sana kama ilivyokuwa eneo la ushambuliaji, hali hiyo imewafanya viongozi wajitathimini na kugundua makosa yaliyopo.
“Licha ya kwamba wanafanya vizuri bado wanatakiwa kuongeza mkazo kwenye kumalizia nafasi eneo hilo kwa sababu wanatengeneza nafasi nyingi na wanazitumia chache, eneo hilo washambuliaji waongeze umakini.”
Naye mshambuliaji wa zamani Simba na Yanga, Zamoyoni Mogella alisema “Misimu miwili mitatu nyuma hawakuwa na washambuliaji wengi na sasa
wameona wafanye usajili eneo hilo kwa nguvu kubwa na imeonyesha kabisa wamefanikiwa kwa kiasi fulani,” alisema Mogella, huku Bakar Malima ‘Jembe Ulaya’ akisema; “Misimu miwili au mitatu nyuma iliyoisha hawakuwa vizuri kwenye maeneo hayo na ndio maana msimu huu wamefanya usajili eneo la kati (kiungo), ushambuliaji na umeonyesha kuna faida.”
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Nabi afumua ukuta Yanga, Bilionea ajifungia na mastaa.​

nabi pic

YANGA ipo kambini ikiendelea na maandalizi ya mechi yao ya leo ya michuano ya Kombe la Shirikisho (ASFC) dhidi ya Biashara United, huku kocha Nasreddine Nabi, akipokea kwa mshtuko taarifa za kufungiwa kwa beki wake mmoja na fasta ameamua kufumua ukuta mzima wa timu hiyo ili kuhakikisha wakiendelea moto.
Beki wa kati tegemeo, Dickson Job amefungiwa mechi tatu na Bodi ya Ligi kupitia Kamati ya Saa 72 baada ya kumkanyaga vibaya nyota wa Mbeya City, Richard Ng’ondya wakati timu hizo zilipokutana jijini Dar na kuisha kwa suluhu.
Job ataanza kutumikia adhabu hiyo kuanzia mechi ya kesho ya hatua ya 16 Bora ya ASFC dhidi ya Biashara United na hapo ndipo kichwa kilipomuuma kocha Nabi.
Akizungumza na Mwanaspoti juzi jijini Dar es Salaam, Nabi alisema baada ya kufungiwa kwa Job sasa analazimika kurudi kazini akianzia jana na leo kuunda upya safu yake ya ulinzi kitu ambacho awali hakuwa na mpango nao.
Kocha Nabi alisema Job alikuwa aendelee kuziba nafasi ya Djuma Shaban ambaye naye anatumikia adhabu ya kusomamishwa mechi tatu kwa kosa kama hilo dhidi ya mchezaji wa Polisi Tanzania katika mechi yao ya Ligi Kuu Bara iliyopigwa Arusha. Djuma anamaliza adhabu hiyo katika mechi hiyo ya Biashara.
“Ilikuwa niendelee kumtumia pale beki ya kulia, lakini kwa adhabu aliyopewa imeturudishia kazi mpya kabisa ambayo hatukuitarajia,” alisema Nabi na kuongeza;
“Tutalazimika kubadilisha sana eneo la ulinzi na kazi hiyo tutaifanya Jumapili na Jumatatu ili tuone kipi tutaweza kuamua, watu wapo ambao wanaweza kuziba hiyo nafasi kitu ambacho kitatupa wasiwasi ni maelewano yao kwa kuwa baadhi yao watakuwa ni wapya kabisa.”
Nabi anaweza kuwatumia mabeki Paul Godfrey ‘Boxer’ au beki wake mpya Ibrahim Bacca kucheza eneo hilo la beki wa kulia katika mchezo huo wa hatua ya robo fainali. Beki mwingine mwenye namba yake, Kibwana Shomary ni majeruhi.
Huenda pia eneo la beki wa kati na hata beki wa kushoto nako kukawa na mabadiliko makubwa kwa watu wapya kurejea ambapo kuna nafasi kubwa beki wa kushoto Yassin Mustafa kuukosa mchezo huo, huku David Bryson akiwa bado hayuko sawa baada ya kuumia katika mchezo dhidi ya Mbeya.
Yanga inakutana na Biashara katika mechi ya ASFC kwa mara ya tatu, baada ya awali kukutana mara mbili na zote vijana wa Jangwani kuwang’oa wapinzani wao.
Ilikutana katika 16 Bora misimu miwili iliyopita na Yanga kupenya kwa penalti baada ya sare ya 2-2 ndani ya dakika 90 kisha msimu uliopita zikavaana nusu fainali iliyopigwa mjini Tabora na Yanga kushinda kwa bao 1-0.

BILIONEA, MASTAA WAJIFUNGIA MCHANA
Katika hatua nyingine ya kuhakikisha Yanga inaendeleza moto wake kwenye mechi zao zote zilizosalia za Ligi Kuu Bara na ASFC, jana Jumapili kikosi kizima kilikuwa na kikao kizito na bilionea wa klabu hiyo Ghalib Said Mohamed (GSM) ambaye aliwaalika chakula cha mchana.
Baada ya mazoezi ya asubuhi kikosi hicho kilitua katika jumba moja kubwa la kisasa kisha kukutana na GSM ambaye alitaka kukutana na wachezaji na makocha pekee katika kikao hicho.
Haijulikani sababu ya kikao hicho, ila Mwanaspoti linafahamu ni moja ya mikakati ya kuhakikisha timu hiyo inafanya vizuri katika mechi zake zinazokuja.
Yanga inasaka ndoo ya kwanza wa Ligi Kuu baada ya kuukosa kwa misimu minne na taji la ASFC inalolisotea misimu mitano.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Dickson Job ajutia kifungo.​

job pic

KIFUNGO cha kutocheza mechi tatu alichopewa beki wa Yanga, Dickson Job kutoka Bodi ya Ligi kupitia Kamati ya Saa 72 imemvuruga beki huyo na kujutia makosa yake.
Job alimkanyaga nyota wa Mbeya City, Richardson Ng’ondya na ndipo Kamati ya 72 ikampiga kifungo cha kutocheza mechi tatu ikiwamo ya kesho ya Kombe la Shirikisho la Azam Sports (ASFC) dhidi ya Biashara United na mbili za Ligi Kuu Bara dhidi ya Mtibwa Sugar na Kagera Sugar.
Mbali na kuzikosa mechi hizo, lakini beki huyo wa kati ambaye kwa siku za karibuni amekuwa akitumika kama beki wa kulia wa Yanga, amelimwa pia faini ya Sh 500,000 na kumfanya ajutie kosa akimuomba radhi Ng’ondya.
“Inaniuma sana, sikudhamiria kufanya vile. Ilitokea tu kama ajali katika mchezo na nimemuomba radhi Ng’ondya na jamii ya wanamichezo wote kwa ujumla, sitarudia kosa kama lile,” alisema Job na kuongeza;
“Kupitia tukio lile nimejifunza, nitaendelea kufanya mazoezi na nikirejea uwanjani naamini nitakuwa bora na kucheza kwa kwa kuzingatia afya ya wachezaji wenzangu.”
Katika mchezo huo baina ya timu zao, dakika 90 ziliisha kwa suluhu, huku Yanga ikinyimwa bao la wazi baada ya waamuzi kutafsiri Fiston Mayele alikuwa ameotea japo marudio ya Azam TV yaliwaumbua na marefa hao waliondolewa katika orodha ya kuchezesha Ligi Kuu.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Nabi aliandaa jembe jipya la kumrithi Job Yanga SC.​

nabi-pic-data.jpg

KOCHA Mkuu wa Yanga, Mtunisia, Nasreddine Nabi, ameanza kumuandaa beki wake mpya wa kati, Ibrahim Abdallah ‘Bacca’ atakayemrithi Dickson Job katika kikosi chake.
Hiyo ni baada ya Job kutumikia adhabu ya kufungiwa michezo mitatu na kutozwa faini ya shilingi 500,000 kwa kosa la kumkanyaga kwenye mbavu mchezaji wa Mbeya City, Richardson Ng’ondya, jambo lililotafsiriwa kuwa ni mchezo wa hatari.
Job, mchezo wake wa kuukosa ni wa leo wa Kombe la FA dhidi ya Biashara United utakaopigwa kwenye Uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam, kisha ataukosa mchezo dhidi ya Mtibwa, Februari 23, na ya mwisho ni dhidi ya Kagera Sugar Februari 27.
Kwa mujibu wa taarifa ambazo imezipata Championi Jumatatu kutoka ndani ya benchi la ufundi la timu hiyo, lililopo chini ya Nabi, Bacca haraka alianza kuandaliwa mara baada ya kupokea taarifa za Job kufungiwa.
Mtoa taarifa huyo alisema kuwa Bacca amepewa mbinu za aina ya uchezaji huku akicheza pacha na nahodha Bakari Mwamnyeto katika mazoezi ya timu hiyo yanayoendelea Uwanja wa Avic Town, Kigamboni nje ya Dar ambako timu hiyo imepiga kambi.
Aliongeza kuwa upo uwezekano wa beki huyo kuanza katika mchezo huo dhidi ya Biashara pamoja na ule wa Ligi Kuu Bara watakaocheza na Mtibwa Sugar huko Manungu, Turiani mkoani Morogoro.
“Mara baada ya benchi la ufundi kupata taarifa za Job kufungiwa kucheza michezo mitatu, haraka benchi la ufundi limeanza kumuandaa mbadala wake atakayechukua nafasi yake.
“Wapo mabeki wengi wenye uwezo wa kucheza nafasi hiyo, akiwemo Bangala (Yannick), lakini kocha anafikiria kumuanzisha Bacca katika mchezo ujao dhidi ya Biashara.
“Uzuri kocha ndiye aliyependekeza usajili wake katika dirisha dogo, hivyo atajua jinsi ya kumtumia katika michezo mitatu ijayo inayofuatia ya ligi na FA,” alisema mtoa taarifa huyo.
Akizungumzia hilo, Nabi alisema: “Nina kikosi kipana cha wachezaji wenye uwezo sawa, hivyo kama akikosekana mmoja, anakuwepo mwingine mwenye kiwango kikubwa, hivyo sina hofu kukosekana kwa Job.”
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Nabi Awapangia Biashara Muziki Mnene.​

273265682_337236161610068_6204935112247286040_n.jpg

YANGA watashuka dimbani leo Jumanne kucheza na Biashara United kwenye mchezo wa hatua ya 16 bora ndani ya Dimba la Mkapa, Dar es Salaam kuanzia saa 1:00 usiku.
Mchezo huo wa Kombe la Shirikisho la Azam Sports, utaamua nani anakwenda hatua ya robo fainali.
Kocha wa Yanga, Nasreddine Nabi, baada ya kufanya maandalizi kwa takribani wiki moja, leo amepanga kuweka kikosi chake cha ushindi kutokana na umuhimu wa mchezo huo.
Mkurugenzi wa Mashindano wa Yanga, Thabity Kandoro, ameliambia Spoti Xtra kuwa: “Mchezo wetu wa kesho (leo) utakuwa na umuhimu mkubwa sana wa kupata matokeo ya ushindi kwa sababu tunahitaji kuvuka hapa na kwenda hatua inayofuata.
“Kocha Nabi nilipozungumza naye aliweka wazi kuwa anataka kuweka mkoko wa maana kwenye mechi hiyo kwani kwa vyovyote anahitaji kushinda na kusonga mbele zaidi hadi fainali na kuwa mabingwa.”
Kwa upande wa Biashara United, Kocha Mkuu, Vivier Bahati, alisema: “Tunamshukuru Mungu tumemaliza maandalizi kuelekea mchezo wetu wa kesho (leo) dhidi ya Yanga.
“Wachezaji wote wapo fiti, tutahakikisha tunapambana na kupata matokeo mazuri kwa ajili ya kuvuka katika hatua
inayofuata kwani mipango yetu ni kuiwakilisha Tanzania katika michuano ya kimataifa msimu ujao.”
Yanga na Biashata United zinakwenda kukutana ikiwa imepita takribani miezi miwili, mara ya mwisho zilikutana Desemba 26, 2021 ukiwa ni mchezo wa Ligi Kuu Bara uliomalizika kwa Yanga kushinda 2-1.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

MAKONGORO KATIBU WA ZAMANI YANGA AFARIKI DUNIA.​

AVvXsEj2AreGTz4voAitQH2BEEAZyH-0KyBkSXXx5R3MsKV0NCLx4w20CIs2YuzhUErzH1Ok_5vj0VIpQzNMFE3qTRbKxASmgYtlPeQI-TFFC9J17S8dIi7dDqkJ7h3bAYRY81qZKmU6oFdT5QkE4S7Ud9ehkiWb3kPWYP5rx5CI4XJxvXsqTX2d5uH4u1iu=w640-h638

ALIYEWAHI kuwa Katibu Mkuu klabu ya Yanga miaka ya 1980, Issa Makongoro amefariki dunia usiku wa kuamkia leo.
Kwa mujibu wa taarifa ya familia yake zinasema msiba uko Mikocheni kwa Warioba na maziko yatafanyika leo Makaburi ya Kisutu, Dar es Salaam.
Uongozi wa Yanga SC umesema umepokea kwa msikitiko makubwa taarifa ya msiba wa kiongozi wake huyo wa zamani, enzi za mfumo wa Makatibu wa kuchaguliwa kwa kura za wachama, tofauti na sasa watendaji wa nafasi hizo wanaajiriwa.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Yacouba Apewa Siku 45 Tu Yanga.​

yangasc_273981881_4154637584638908_8217086733076312454_n-1.jpg

DAKTARI wa viungo wa Yanga, Mtunisia, Youssef Ammar, amesema kiungo mshambuliaji wa timu hiyo, Yacouba Songne, amepata nafuu na atarejea uwanjani baada ya takribani siku 45.
Yacouba yupo nje ya uwanja tangu Novemba mwaka jana alipoumia goti ambapo tayari amepatiwa matibabu nchini Tunisia.
Akizungumza na Spoti Xtra, Ammar alisema Yacouba ameanza program ya mazoezi ya kukimbia mbio fupi na
ndefu kwa ajili ya kujiweka sawa, ikiwa ni baada ya kumaliza program ya gym.
Aliongeza kuwa nyota huyo atakuwa fiti na kamili kuanza kuipambania timu hiyo, baada ya mwezi mmoja na nusu ambao ni sawa na siku 45.
“Licha ya Yacouba kupata nafuu pamoja na kuanza program ya mazoezi ya kukimbia mbio fupi na ndefu, lakini bado anaendelea na matibabu chini ya uangalizi wangu. “Kwani bado hajapona vizuri, hivyo yupo chini ya uangalizi kwa hofu ya kujitonesha ili asirejee tena katika majeraha hayo ya goti.
“Kutokana na maendeleo yake hivi sasa, upo uwezekano wa kurejea rasmi uwanjani baada ya mwezi mmoja na nusu,” alisema Ammar.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Yanga waitana fasta.​

waitana pic

WAKATI vita ya ubingwa wa Ligi Kuu Bara ikizidi kupamba moto, wanachama na mashabiki wa Yanga tawi la Mwanjelwa wameitana fasta kuweka mikakati ya kumaliza kazi mapema.
Kwa sasa ni misimu minne Yanga haijaonja ubingwa wa Ligi Kuu na Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC), jambo linalowafanya mashabiki na viongozi wao nchini kutokuwa na furaha.
Hata hivyo, msimu huu wakongwe hao wameonekana kupania zaidi kutokana na mwenendo wao wakiwa kileleni kwa pointi 36, huku wakicheza mechi 14 bila kupoteza.
Katibu wa tawi hilo kongwe jijini hapa lenye wanachama 77, Rajabu Mrisho alisema Jumamosi hii mashabiki na wanachama watakuwa na mkutano kujadili mambo mbalimbali juu ya timu yao.
Alisema lengo kubwa ni kuhamasisha uandikishaji kupata wanachama wapya, pia ishu ya mikakati ya kuipa ubingwa timu yao na kuweka umoja na mshikamano.
“Mkutano utafanyika Jumamosi, kwenye Ukumbi wa Tughimbe, lengo ni kuhamasisha wanachama kujiandikisha lakini kujadili namna ya timu yetu msimu huu kupata ubingwa, niwaombe mashabiki kujitokeza kwa wingi,” alisema Mrisho.
Naye Said Athuman mwanachama wa timu hiyo kutoka tawi hilo, alisema kwa sasa wana matumaini makubwa kwa timu yao kubeba taji baada ya kulikosa muda mrefu.
“Iwe FA tunachukua, Ligi Kuu hapo ndio tunapataka zaidi, msimu huu tumedhamilia kuhakikisha tunakata kiu ya muda mrefu, mashabiki tuungane kwa pamoja,” alisema Athuman ambaye ni Katibu Msaidizi.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Nabi Kufyeka Mishahara Ya Mastaa Yanga.​

273265682_337236161610068_6204935112247286040_n.jpg

KUFUATIA wachezaji wa Yanga, Dickson Job na Djuma Shabani, kusimamishwa kucheza mechi za ligi na Shirikisho
la Soka Tanzania (TFF) kutokana na makosa waliyofanya katika michezo iliyopita, kocha wa timu hiyo, Nasraddine Nabi, ameibuka na kuwaonya kutorudia vitendo hivyo la sivyo atachukua mshahara wote.
Djuma alisimamishwa na Bodi ya Ligi kucheza mechi tatu baada ya kumpiga kiwiko mchezaji wa Polisi Tanzania, Yahaya Mbegu kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara, ambapo Yanga ilishinda kwa bao 1-0, huku Job akipewa adhabu baada ya kumchezea rafu, Richardson Ngodya wa Mbeya City hivyo na yeye kusimamishwa michezo mitatu.
Chanzo chetu kutoka Yanga kimeliambia Championi kuwa, pamoja na Bodi ya Ligi kutoa maamuzi yake, Nabi naye katoa onyo kali kwa nyota hao ambapo amewataka wachezaji wote wa Yanga kuepuka makosa ya kizembe ambayo yanaweza kuigharimu timu kwa kukosa huduma zao uwanjani.
“Kocha ameitisha kikao mara baada ya Djuma na Job kupewa adhabu ya kukosa mechi tatu, aliwaambia mara nyingine ataondoka na mshahara wa mchezaji atakayeonekana kusimamishwa baada ya kufanya kosa la kizembe.
“Kocha amewaambia wachezaji kujichunga sana katika kudhibiti hasira kwani endapo hawatakuwa makini basi wanaweza kujikuta takribani kila mechi kuna mchezaji anasimamishwa kwani kutokana na mwenendo wa timu kwa sasa wapinzani wanahakikisha wanawachokonoa ili wapate adhabu ambayo itawapunguza kasi,” kilisema chanzo hicho. Alipotafutwa Msemaji wa Yanga, Haji Manara alisema: “Samahani niko hospitali, nitakupigia.”
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

GSM Yampa maagizo maalum Mayele.​

YANGA-MAYELE-MOLOKO-FEI-TOTO.jpg

RAIS wa Makampuni ya GSM Group, Gharib Salim Mohammed, juzi Jumapili aliwaalika mastaa wa Yanga nyumbani kwake Kigamboni, Dar es Salaam wakiongozwa na Fiston Mayele na Chico Ushindi kwa ajili ya kula chakula cha mchana sambamba na kufanya kikao kizito.
Yanga ambao ni mabingwa wa kihistoria wa Ligi Kuu Bara wakibeba ubingwa huo mara 27 ikiwa ni nyingi kuzifunika timu zote ikiwemo Simba iliyobeba mara 22, msimu huu inaongoza msimamo wa ligi kwa kukusanya pointi 36 ikicheza mechi 14.
Licha ya kuwa kileleni kwa tofauti ya pointi tano dhidi ya Simba yenye 31, lakini Yanga imekuwa na presha kubwa ya kuzidiwa ujanja na wapinzani wao hao na kuukosa ubingwa.
Mmoja wa mabosi wa Yanga, ameliambia Spoti Xtra kuwa, Gharib aliwaalika nyumbani kwake mara baada ya kumaliza program ya mazoezi ya asubuhi.
Bosi huyo alisema kuwa, wakiwa huko, walifanya kikao kilichoandaliwa maalum kwa ajili ya kuwaongezea hamasa mastaa hao ili wafanye vema katika michezo ya ligi pamoja na Kombe la Shirikisho la Azam Sports wakianza na Biashara United.
Aliongeza kuwa, kikao hicho pia kiliwahusisha viongozi wa Benchi la Ufundi linaloongozwa na Kocha Mkuu Mtunisia, Nasreddine Nabi na baadhi ya viongozi wa Kamati ya Utendaji wa Yanga.
“Kikao kilikuwa na malengo mazuri ya kuijenga timu na zaidi kuwaongezea hamasa na morali wachezaji ili wapambane katika michezo ijayo.
“Gharib alipata nafasi ya kuzungumza na mchezaji mmoja mmoja hapo nyumbani kwake baada ya kikao cha pamoja ambapo kuna maagizo maalum wachezaji wamepewa.
“Hii siyo mara ya kwanza kwake kufanya kikao na wachezaji chenye lengo la kuwaongezea morali na kufahamu majukumu yao ya uwanjani ili wafanikishe malengo ya kuchukua ubingwa,” alisema bosi huyo.
Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Frederick Mwakalebela, alizungumzia hilo kwa kusema: “Mara kwa mara uongozi tumekuwa tukifanya vikao na wachezaji, kikubwa ni kuwakumbusha majukumu yao ya uwanjani, kama unavyofahamu malengo yetu msimu huu ni kuchukua ubingwa katika michuano tunayoshiriki.”
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Moloko akifanya hivi atawavuruga kinoma.​

Moloko PIC

WINGA wa Yanga, Jesus Moloko kwa kasi aliyonayo ameshauriwa kuongeza maarifa kwenye umaliziaji jambo litakalompa urahisi wa kufanya makubwa Ligi Kuu Bara.
Tangu amejiunga na Yanga msimu huu, Moloko amecheza mechi 13 za ligi na hajacheza dakika 90, huku akicheza dakika chache zaidi (23) dhidi ya Tanzania Prisons, ambapo dakika alizocheza katika mechi 13 ni 886, jambo ambalo wadau wameona kitu cha ziada kwake. Katika mahojiano na Mwanaspoti, wadau walidai Moloko ana vitu miguuni ambavyo hajavionyesha na kumtaka aongeze bidii ili atishe.
Staa wa zamani wa timu hiyo, Sekilojo Chambua alisema nyota huyo ana kasi nzuri, isipokuwa anapaswa kuongeza maarifa katika umaliziaji wa mipira ya mwisho.
“Ana kasi nzuri inayoendana na nafasi anayocheza. Pamoja na hilo siyo mzuri kwenye umaliziaji wa mipira ya mwisho, ila akiongeza bidii katika hilo ataifanyia mambo makubwa Yanga,” alisema.
Straika wa zamani wa timu hiyo, Said Bahanuzi alisema kwa mbio zake akiwa na umaliziaji mzuri anaweza kufunga mabao na kutoa asisti nyingi. “Ana kasi ambayo inaweza kuwa mwiba kwa mabeki, isipokuwa aongeze umakini kwenye kumalizia mipira ya mwisho.”
Kipa wa zamani wa Simba na Yanga, Steven Nemes alisema Moloko anapaswa kuboresha umaliziaji ili kuendana na kasi yake.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Nabi afichua siri ya mataji.​

Nabi PIC

KOCHA Mkuu wa Yanga, Nesreddine Nabi amefichua kitu juu ya ushindani wa Ligi Kuu Bara huku akitaja siri kuu mbili zinazoweza kuwabeba kutwaa taji msimu huu.
Yanga ndio vinara wa ligi hiyo baada ya kucheza michezo 14 ya mzunguko wa kwanza na kukusanya pointi 36 wakiwa mbele pointi tano na watani zao Simba walio nafasi ya pili na pointi 35.
Akizungumza na Mwanaspoti, Nabi alisema ameangalia misimu minne ambayo timu yake imesota bila kutwaa taji lolote na kujipiga kifua kuwa yeye ni bora na ana nafasi nzuri ya kufanya vizuri.
“Yanga wana ukame wa kutwaa taji ndani ya misimu minne nimefuatilia na nimebaini mapungufu ndani ya misimu hiyo ni ufinyu wa kikosi na kukosa mastaa wenye mwendelezo wa ubora kitu ambacho msimu huu anacho,” alisema na kuongeza;
“Nafurahi msimu huu nimeikuta timu nzuri na ina kikosi kipana ambacho akikosekana mmoja mwingine anachukua nafasi na anafanya kile kinachotakiwa kufanywa,” alisema.
Alisema Yanga ya msimu huu imekuwa na mfululizo wa majeruhi lakini hakuna pengo linaloonekana tofauti na misimu iliyopita na aliongeza kuwa mastaa wake wana ari ya ushindani.
“Timu sasa inaweza ikatanguliwa kufungwa wachezaji wakarudi mchezoni na kusawazisha hadi mpira unamalizika wanaongeza bao la ushindi tofauti na nyuma alivyoifuatilia timu hiyo,” alisema.
Akizungumzia ishu ya kutoka sare kama imewaondoa mchezoni alisema hawana sababu ya kufanya hivyo kwa sababu bado wanamichezo mingi mbele, hivyo wanapambana kuhakikisha wanarekebisha walipokosea ili waweze kusonga mbele.
Alisema wanaongoza ligi wanahitaji kuendelea hivyo hadi mwisho wa msimu hivyo hawahitaji kumfikiria zaidi anayewakimbiza zaidi ni kupambana kupata matokeo kila mchezo huku akiitaja Mtibwa Sugar kuwa ndio timu inayompa wakati mgumu kwani wanaenda ugenini.
Yanga mchezo wake wa mwisho wa ligi waliambulia suluhu na Mbeya City na wanatarajia kuwa ugenini Februari 23 dhidi ya Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Manungu, Morogoro.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Chico Yamkuta, Aondolewa Yanga​

Chico-Ushindi-1.jpg

KIUNGO mshambuliaji wa Yanga, Mkongomani, Chico Ushindi, atakaukosa mchezo ujao wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Mtibwa Sugar kutokana na kuumwa ghafla.
Timu hizo zinatarajiwa kuvaana Februari 25, mwaka huu mchezo unaotarajiwa kupigwa kwenye Uwanja wa
Manungu, Turiani mkoani Morogoro.
Akizungumza na Spoti Xtra, Daktari wa Viungo wa Yanga, Mtunisia, Youssef Ammar, alisema kiungo huyo alipata maumivu ya misuli siku moja kabla ya mchezo dhidi ya Biashara United uliochezwa juzi Jumanne.
Ammar alisema Chico alikuwepo katika mipango ya kucheza mechi hiyo ya juzi, lakini maumivu aliyoyapata yalisababisha aondolewe kikosini.
“Chico alikuwepo katika mipango ya kocha kuanza kikosi cha kwanza dhidi ya Biashara, lakini alikuja kuondolewa saa chachebaada ya kupata maumivu ya misuli akiwa mazoezini.
“Kuondolewa kwake kuliharibu mipango ya kocha, hivyo kutokana na maumivu hayo aliyoyapata, atatakiwa kukaa nje ya uwanja kuanzia siku saba hadi kumi kwa ajili ya kupatiwa matibabu, hivyo huenda akaukosa mchezo ujao wa ligi dhidi ya MtibwaSugar,” alisema Ammar.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Mwamnyeto: Tunabeba Ubingwa ASFC.​

273994423_159030173143872_5780108529921510937_n.jpg

BEKI wa kati wa Yanga ambaye pia ni nahodha wa timu hiyo, Bakari Mwamnyeto, amesema safari hii wanahitaji kufika fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) na kuwa mabingwa.
Yanga juzi Jumanne walifanikiwa kutinga robo fainali ya michuano hiyo baada ya kuibuka na ushindi wa
mabao 2-1 dhidi ya Biashara United katika Uwanja wa Mkapa, Dar.
Akizungumz na Spoti Xtra, Mwamnyeto alisema, malengo yao msimu huu ni kuhakikisha
wanatwaa ubingwa wa michuano hiyo.
“Tunatakiwa kufika fainali ili tuwe mabingwa wa a michuano hii, akili zetu na malengo yetu yapo katika michuano hii na lazima tuhakikishe tunatimiza.
“Wapinzani wanatakiwa kujipanga kwani hata sisi tayari tumeshajipanga kucheza na timu yoyote itakayojitokeza
mbele yetu, hakuna jambo ambalo lisilowezekana, ni kujituma tu na kuwa na nia ya kuwa mabingwa na sisi tunayo
nia,” alisema nahodha huyo.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Yanga yahamishia mchakato Bungeni.​

Yanga pic

Klabu ya Yanga leo Feb 18 itafanya uzinduzi wa kadi mpya za Uanachama za kielektroniki kwa Wabunge wa Bunge Ia Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao ni Wanachama wa Yanga.
Uzinduzi wa kadi za Kielektroniki ni sehemu ya mchakato wa mabadiliko ya kidigitali na ya mfumo wa uendeshaji wa Klabu kwa mujibu wa katiba ya Yanga toleo Ia 2021.
Hafla ya uzinduzi huo itafanyika kwenye Hoteli ya Morena jijini Dodoma kuanzia saa 4:00 asubuhi ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Spika wa Bunge Dk. Tulia Ackson.
Hafla hiyo itahudhuriwa na Waheshimiwa Wabunge, Viongozi wa Klabu ya Yanga, wadau na waandishi wa habari.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Mziki wa Mayele wamkuna Nabi.​

MAYELE PIC

KOCHA wa Yanga, Nesreddine Nabi amechekelea msako wa mabao kwa kikosi chake katika mechi walizocheza hadi sasa, lakini akampa tano zaidi straika namba moja wa kikosi hicho, Fiston Mayele akisema jamaa anajua sana kusumbua.
Akizungumza na Mwanaspoti, Nabi alisema anavutiwa na Mayele jinsi anavyoongoza jahazi la kusaka mabao bila kujali kuna wakati yanakataliwa.
Mayele aliyesajiliwa msimu huu kutoka DR Congo, ameifunga Yanga mabao sita katika Ligi Kuu Bara na mawili ya Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) na kuifanya timu hiyo itishe.
Yanga inalisotea taji la Ligi Kuu Bara kwa msimu wa nne mfululizo sasa huku kwa ASFC inalisaka kwa msimu wa tano, kwani ilibeba mara ya mwisho ule wa 2015-2016.
Nabi alisema baada ya kukataliwa kwa bao lake la kwanza katika mchezo wa juzi dhidi ya Biashara United wa hatua ya 16 Bora ya ASFC, mshambuliaji huyo hakukata tamaa badala yake alipambana kuisaidia Yanga kushinda mabao 2-1.
Mayele alifunga bao la pili baada ya Yannick Bangala kufungua pazia na Biashara ikapata la kufutia machozi kupitia Collins Opare aliyemalizia pasi ya Christian Zigah na kuivusha Yanga hadi robo fainali.
Katika mchezo wa juzi wakati Yanga ikicheza dhidi ya Biashara, Mayele alifunga bao dakika ya pili, lakini lilikataliwa kwa sheria ya mtego wa kuotea ambapo baada ya picha za marejeo zilionyesha ni kweli ilikuwa usahihi kukataliwa kwa bao hilo.
“Mchezaji mwenye moyo mwepesi baada ya kukataliwa kwa lile bao angeweza kutoka mchezoni na kukata tamaa kwa mambo ambayo pia yalitokea hapa kati, lakini kwake (Mayele) haikuwa hivyo,” alisema Nabi.
“Angalia alivyoendelea kupambana kwa nguvu na kasi kubwa kusaka ushindi zaidi. Ni mpambanaji sana hakati tamaa wala haogopi mabeki hata wakimuumiza.”
Vilevile Nabi alifichua kwa-mba aliwa-ambia ma-staa wa-ke kwa-mba katika kukabiliana na makosa ya waamuzi kukata mabao yao wanachotakiwa ni kufunga zaidi kwa kuwa hayawezi kukataliwa mabao yote.
Alisema mashabiki wa timu yao bado wanatarajia kuona kikosi chao kikipambana bila kujali changamoto ambazo wanapitia na kwamba ili malengo yao yatimie wanatakiwa kufunga mabao zaidi yatakyowahakikishia ushindi.
“Kuna makosa kidogo kila mtu anayaona lakini sio kila wakati utatakiwa kulalamika unatakiwa kuendelea kupambana niliwaambia tunatakiwa kufunga zaidi kutumia nafasi nyingi tunazotengeneza.
“Mfano unaweza kuangalia mchezo dhidi ya Mbeya City hatukutakiwa kupata pointi moja, lakini tulitakiwa kutumia nafasi zaidi kuliko ile ambayo tutaendelea kuikumbuka.
“Sasa wachezaji wameanza kuelewa na ndio maana unaona kila mmoja anapambana anataka kuona ushindi unapatikana kama ni beki akipata nafasi anataka kuitumia kwa ushindi ni wetu sote.”