Simba Sports Club Thread

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Pablo: Kila mtu lazima afunge.​

pablo pic

LICHA ya kwamba mastraika wa Simba wameendelea kulaumiwa kwa kuinyima ushindi timu hiyo katika mechi mfululizo walizocheza, kocha wa kikosi hicho, Pablo Franco ameshtukia jambo na kulifanya kazi haraka kabla ya kukutana na Asec Mimosas.
Mashabiki wa Simba na wadau wa soka wamepatwa na wasiwasi na safu ya ushambuliaji ya Simba inayoelekea kuikabili miamba hiyo ya Ivory Coast kwenye mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi wa Kombe la Shirikisho Afrika utakaofanyika Jumapili kwenye Uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar es Salaam.
Hata hivyo, kocha Pablo anajua majanga ya safu yake ya ushambuliaji na sasa ameamua kuja na mbinu mbadala ya kuwataka wachezaji wote wa kikosi hicho wakiwemo mabeki kufunga mabao huku akisema soka la sasa limebadilika.
Pablo alisema ni mbaya kwa timu kutegemea mtu mmoja au wawili wawafungie mabao kwani madhara yake ni makubwa kwa sababu wakidhibitiwa inaweza kuwapa wakati mgumu, “Tunapaswa kuwa timu ambayo haitabiriki.
“Kitu muhimu ni kuendelea kutengeneza nafasi na kujitahidi kuzitumia, kila mchezaji ana wajibu wa kutufungia bao, mpira siku hizi umebadilika wapo mabeki wenye idadi kubwa ya mabao,
“Najua hali ilivyo lakini hicho sio kisingizio kwetu tunapaswa kuimarika katika utumiaji wa nafasi si kwa washambuliaji pekee bali kwa mtu yeyote atakayepata nafasi,” alisema Pablo
Katika mazoezi yaliyofanyika juzi jioni kwenye Uwanja wa Mo Simba Arena uliopo Bunju, Pablo aliwaongoza wachezaji wachache kufanya mazoezi, wale ambao hawakucheza kabisa mechi iliyopita ya ligi dhidi ya Mbeya Kwanza na walioingia kutokea benchi wakati wale waliocheza dakika zote 90 walipewa program maalum ya Gym.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Wachezaji Simba waapa.​

waapa pic

WACHEZAJI wa Simba wamewatoa hofu mashabiki na wakaapizana kwamba kwenye mechi za Shirikisho kuanzia Jumapili hii dhidi ya Asec Mimosas jijini Dar es Salaam hakuna kufanya kosa.
Simba wako kundi D na timu za RS Berkane ya Morocco, USGN ya Niger na Asec ya Ivory Coast.
Mastaa wawili wa Simba, Henock Inonga na Rally Bwalya wameliambia Mwanaspoti kwamba wao kama wachezaji wamejipanga na wanataka kulipizia kile ambacho hawakukifanya kwenye mechi za Ligi ya Mabingwa walipotolewa.
Bwalya ambaye anapewa nafasi kubwa ya kuanza Jumapili kama kiungo mkabaji anasema; “Unajua suala la kuondolewa katika Ligi ya Mabingwa Afrika msimu huu wachezaji wote tulikuwa na hasira na kuambiana huku kwenye Shirikisho ndio tunatakiwa kuonyesha ukubwa wetu kwa kupata ushindi mfululizo.”
Inonga ameahidi kuonyesha ubora wake kwa kupambana mwanzo mwisho. ”Kufanya vizuri kwangu maana yake nitaifanya timu kupata matokeo mazuri katika mashindano haya, tutawazuia wote na Simba kupata ushindi,” alisema.
“Malengo ya Simba ni kufanya vizuri katika mashindano haya na kufika mbali kwa maana hiyo kila mchezaji atapambana na kujituma kutimiza majukumu yake ili kuyafikia hayo tuliyokubaliana,” alisema.
Kati ya maandalizi ya Simba kuukabili mchezo huo ni mazoezi makali ambayo kocha wa Simba, Pablo Franco amebadili ratiba na kuweka awamu mbili kwa siku asubuhi yale ya Gym na jioni uwanjani.
Pia juzi benchi la ufundi lilikutana zaidi ya saa moja na kufanya uchambuzi wa kutosha kwa baadhi ya mechi walizocheza Asec Mimosas katika Ligi Kuu ya nchini kwao pamoja na mashindano ya kimataifa msimu huu.
Pablo, wasaidizi wake na mtaalamu wa uchambuzi wa video za wapinzani wa Simba, Culvin Mavunga waligundua wanakwenda kucheza na timu imara ndio maana katika ligi ya kwao inaongoza ikiwa imecheza mechi saba, imeshinda zote, imekusanya pointi 21, imefunga mabao 13 na imefungwa matatu.
Jambo jingine walilogundua na wameanza kulifanyia kazi haraka ni safu ya ushambuliaji ya timu hiyo ina wachezaji hatari na wenye uwezo wa kufunga kama Karim Konate aliyeanza katika michezo yote. Michezo saba waliocheza Mimosas wamefunga mabao 13.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Mo Dewji alipa mishahara Simba ili waiue Asec.​

mo pic

RAIS wa heshima wa Simba, Mohammed Dewji ‘Mo Dewji’ juzi aliwamwagia mkwanja wachezaji wa kikosi hicho mchana wa Jumatano alipowatembelea kambini kwao.
Bilionea huyo baada ya kikao cha dakika kadhaa na wachezaji, kwanza aliwalipa wachezaji na benchi la ufundi mishahara yao ya mwezi Januari kila mmoja.
Wachezaji wa Simba baada ya hapo walipokea bonasi ya mechi nne walizoshinda awali dhidi ya Azam, Dar City, Tanzania Prisons na Mbeya Kwanza.
Mechi ya Azam walipewa bonasi ya Sh50 milioni wakati Dar City, Prisons na Mbeya Kwanza hizo kila moja ilikuwa Sh20 milioni kwa maana hiyo mara tatu ni Sh60 milioni ukijumlisha na ile ya Azam walivuta jumla ya Sh110 milioni.
Bonasi hizo ukiondoa mechi ya Azam, nyingine zilizobaki wachezaji wanagawana tofauti mchezaji aliyecheza hata dakika moja anapata Sh400,000 aliyekuwa benchi na hakucheza Sh200,000 wakati wale wa jukwaani si zaidi ya Sh100,000. Wachezaji hao wa Simba mbali ya kuongezewa mzuka walielezwa kabla ya mechi ya Mimosas wataahidiwa bonasi nyingine kama watashinda wataichukua kabla ya kwenda Niger katika mechi ya USGN.
Februari 17, kikosi cha Simba kitaondoka nchini kwenda Niger katika mchezo wa pili hatua ya makundi kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya USGN na baada ya hapo hawatarejea nchini wataunganisha huko huko kwenda Morocco.
Baada ya mambo yote hayo, Mo Dewji alisema atakuwepo uwanjani kwenye mchezo dhidi ya Mimosas na anawaomba mashabiki wa timu hiyo wajitokeze kwa wingi.
“Nimekuja kambini kukutana na wachezaji na viongozi kuwapa hamasa, unajua kwa nini Simba imekuwa kati ya klabu kumi bora Afrika ni kutokana na kushindana katika Ligi ya Mabingwa Afrika mwaka huu bahati mbaya tumeteleza,” alisema Mo Dewji na kuongeza;
“Tupo katika kombe la Shirikisho Afrika lazima tujipange kwani ni mashindano ya kweli lakini bado tunakazi ngumu kwenye ligi na lazima tuwe na malengo makubwa.”
Mo Dewji alitumia muda mwingi kuwaeleza wachezaji, benchi la ufundi na stafu wengine thamani ya klabu hiyo. Aliwaambia wanakazi kubwa ya kutetea ubingwa wa Ligi Kuu Bara na kusahau matokeo mabaya waliyopata katika michezo iliyopita ila wanapaswa kuyachukulia kama funzo na kufanya vizuri michezo ijayo na lisiwatokee tena.
Aliwaeleza wachezaji na benchi la ufundi pointi walizoachwa na vinara wa ligi si nyingi kama kwa pamoja kila mmoja atakuwa na lengo la kupambana kushinda kila mechi iliyokuwa mbele yao. Mo Dewji baada ya hilo aliwambia wachezaji malengo mkubwa ya Simba yalikuwa katika Ligi ya Mabingwa Afrika ila imetokea bahati mbaya wameondolewa sasa nguvu zao zote wazihamishie kwenye Shirikisho Afrika.
Aliwaeleza wachezaji wanatakiwa kupambana mpaka tone la mwisho ili kufanya vizuri katika mechi ya Jumapili dhidi ya Asec Mimosas na si hiyo bali zote za hatua ya makundi ili kuvuka na kwenda hatua za mbele zaidi ikiwezekana kuchuku ubingwa.
Baada ya hapo Mo Dewji aliwaambia wachezaji na benchi la ufundi viongozi wapo pamoja nao katika kila kitu wanafanya na kuwa tayari kuwapatia kila kitu ili kutimiza yale malengo ya timu na kuhakikisha hadhi ya Simba inabaki palepale ndani na nje ya nchi. Nini maoni yako kuhusiana na habari hii;
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Mo Awawekea Sh 200Mil Mastaa Wakiifunga Asec.​

SIMBA-12.jpg

KATIKA kuhakikisha wanapata ushindi wa kwanza nyumbani dhidi ya Asec Mimosas ya nchini Ivory Coast katika mchezo wa kwanza wa makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika, Rais wa Heshima wa Simba, bilionea Mohamed Dewji ‘Mo’, ameahidi kuwapa bonasi nzuri inayofikia Sh 200Mil kama wakifanikiwa kuwafunga wapinzani wao hao.
Timu hizo zinatarajiwa kuvaana Jumapili hii saa 10:00 jioni kwenye Uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam.
Simba ambao ni wenyeji katika mchezo huo, watawakosa wachezaji wake muhimu wenye majeraha Chris Mugalu, Kibu Denis na Clatous Chama ambaye kanuni zinambana kucheza michuano hii kutokana na
kucheza mechi za michuano ya Caf akiwa na RS Berkane ya Morocco.
Bosi huyo juzi alivamia kambi ya timu hiyo iliyopo Bunju, nje kidogo ya Dar es Salaam, saa chache kabla ya
kuelekea mazoezini kwa ajili ya kuzungumza na wachezaji hao.
Mara baada ya kuvamia kambini hapo alifanya kikao na wachezaji, benchi la ufundi na viongozi wakiwemo
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya timu hiyo, Salim Abdallah ‘Try Again’,
Mtendaji Mkuu, Barbara Gonzalez na mjumbe wa bodi, Mramu Ng’ambi. Chanzo chetu kimetudokeza kuwa katika kikao hicho, Mo alitoa ahadi hiyo ya bonasi kama wakifanikiwa kupata ushindi wa nyumbani dhidi ya Asec.
“Morali ya wachezaji itaongezeka katika kuelekea mchezo wetu dhidi ya Asec ni baada ya maneno mazuri
waliyoambiwa wachezaji wetu na Mo ambaye ni mwekezaji wetu.
“Wachezaji wote walihimizwa kupambana katika mchezo huu ili kuhakikisha tunafuzu katika
hatua hii na kufuzu kufika nusu fainali, wachezaji chini ya nahodha Bocco (John) walitoa ahadi nzito kwa Mo
na kuahidi kupambana kupata ushindi.
“Ahadi hiyo ya Mo imeongeza morali kwa kila mchezaji aliyepo kambini,” kilisema chanzo hicho.

MO AFUNGA KUELEKEA MCHEZO HUO
“Mimi nimetoka mbali na hii Simba, nashangaa hao watu wanaosema kuwa mimi nimeondoka Simba, nilianza
kuipenda timu hii tangu nikiwa mdogo.
“Nimewekeza pesa nyingi ndani ya Simba nilianza kwa kuweka Sh 25Bil lakini kabla nilikuwa nilishatumia
20Bil kabla ya kuongezea Sh 20Bil, hivyo hadi hivi sasa nimefikisha 85Bil ambazo nimetumia katika kipindi
changu nikiwa na timu.
“Lipo wazi kuiendesha klabu kubwa kama ya Simba ni hasara, lakini naendelea kutoa pesa zangu kwa ajili
ya Simba, hivyo mimi nipo Simba.
“Tuliteleza kidogo katika msimu huu na kutolewa katika Ligi ya Mabingwa Afrika na kuangukia huku Shirikisho,
malengo yetu ni kufika mbali zaidi ya hapa tulipofikia.
“Tunafahamu tuna majukumu mengi, ikiwemo ligi lakini ninaamini tutapambana, ni lazima tujipange kwani haya
mashindano ni magumu na siriazi.
“Bado tunaendelea kupambana na bajeti yetu ya Simba ili timu iweze kujiendesha yenyewe na kwa miaka minne niliyokuwa kiongozi ndani ya Simba ambayo hivi sasa sina mamlaka nayo sana baada ya kujiondoa katika nafasi ya mwenyekiti wa wakurugenzi, lakini bado nipo ndani ya timu kwa ajili ya kuwasaidia, hivyo niwaambie kuwa nitaendelea kuisadia timu yangu ya Simba.
“Lengo ni kuweka bajeti kubwa ndani ya timu hiyo ili tuweze kupambana na baadhi ya klabu kubwa katika
Ukanda wa Afrika kama vile Al Ahly.
“Wengi wanasema mafanikio ya Simba ni Mo lakini mimi naamini mafanikio ya Simba ni mashabiki. Wajitokeze kwa
wingi Jumapili. Kiingilio cha chini ni Sh 5,000 lakini natangaza kushusha hadi Sh 3,000,” alisema Mo.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Simba Yaanika Siri za Kuwaua Asec Mimosas.​

SIMBA-3.jpg

UONGOZI wa Simba umesema kuwa hauna hofu kuelekea mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Asec Mimosas ya Ivory Coast kesho Jumapili kutokana na maandalizi waliyoyafanya huku ukitoa onyo kali kwa wapinzani wao.
Simba inatarajiwa kuvaana na Asec ambayo aliwahi kuichezea beki mkongwe Pascal Wawa kutoka nchini humo, ambaye yeye anaijua vizuri timu hiyo.
Mchezo huo ambao ni wa kwanza wa hatua ya makundi ya michuano hiyo, unatarajiwa kupigwa kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam kuanzia saa 10:00 jioni.
Akizungumza na Championi Ijumaa, Meneja wa Habari na Mahusiano wa Simba, Ahmed Ally, alisema wameshazijua mbinu watakazokuja nazo wapinzani kuelekea mchezo huo mgumu.
Ally alisema baada ya kuifutilia kwa karibu timu hiyo, walichogundua ni kwamba wanacheza soka la kujilinda ‘kupaki basi’ wanapocheza ugenini, hivyo hizo mbinu ndiyo zitakazowaharibia kwani zitawafanya wawapige bao nyingi.
Aliongeza kuwa wanajivunia uzoefu mkubwa walionao wa kucheza soka la Afrika, hivyo mashabiki wajitokeze kwa wingi uwanjani kuisapoti timu yao watakapovaana dhidi ya Asec.
“Tunajivunia uzoefu tulionao hivi sasa wa kucheza soka la Afrika, hivyo hatuna hofu kuelekea pambano hilo na kikubwa niwatahadharishe hao Asec wanapokuja na mbinu za kupaki basi.
“Kama wakijipindua kucheza soka la kupaki basi, watarajie kula bao nyingi za kutosha kabla ya kurudiana nao. Nako huko nyumbani kwao wakijifanya wafunguke kucheza kwa kushambulia ndiyo watakuwa wamejichongea, tutawafunga nyingi zaidi tutakapocheza hapa nyumbani,” alisema Ally.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Simba kuwaweka kikao Bwalya, Chama.​


chama.jpg

SELEMAN Matola, Kocha Msaidizi wa Simba, amesema kuwa watafanya kazi kubwa kwa wapigaji mipira iliyokufa ambayo wanaipata katika mechi ambazo wanacheza.
Akizungumza na Championi Jumamosi, Matola alisema kuwa tatizo la kushindwa kupata matokeo mazuri lina maumivu makubwa na wamegundua tatizo lilipo ikiwa ni pamoja na kushindwa kutumia mipira ya kona na faulo.
“Kushindwa kupata matokeo mazuri kwa Simba ni maumivu lakini tumegundua kwamba suala la kukosa kutumia mapigo huru, hilo nalo ni kosa, hivyo kwa wapigaji wa kona na faulo wote tutazungumza nao ili kuboresha makosa yetu.
“Ikiwa kwenye mechi tunapata kona zaidi ya 9 na hazileti mabao, hilo ni jambo la kufanyia kazi kwenye uwanja wa mazoezi, bado tupo imara na makosa kila siku tunayafanyia kazi na tutazungumza na wachezaji wetu ili tuweze kupata ushindi pia kupitia mapigo hayo.
“Mfano kwenye mchezo dhidi ya Prisons tulipata kona tatu ziliweza kuwa na hatari kwenye lango la mpinzani lakini hatukufunga, bado kuna mechi zinakuja tunaamini tutafanya vizuri,” alisema Matola.
Wapigaji kona wa Simba ni Rally Bwalya, Clatous Chama, Sadio Kanoute na Bernard Morrison ambaye amesimamishwa kwa muda kutokana na masula ya nidhamu.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Morisson Asamehewa Simba.​

MORISSON.jpg

Kiungo Mshambuliaji wa Wekundu wa Msimbazi Bernard Morrison, ameruhusiwa kurejea kikosini leo baada ya kumaliza kesi yake ya utovu wa nidhamu iliyokuwa inamkabili.
Siku chache zilizopita Morrison alituhumiwa kwa makosa ya utovu wa nidhamu ambapo alisimamishwa kwa muda pamoja na kutakiwa kutoa maelezo kwa Mtendaji Mkuu wa Klabu Barbara Gonzalez.
Morrison aliomba radhi kwa uongozi na benchi la ufundi na mapema leo alifika katika ofisi za Klabu na kuwa na maongezi na Mtendaji Mkuu Barbara.
Taarifa za uhakika zinadai kuwa katika maelezo yake Morrison ameomba radhi na ameahidi kutorudia makosa. Taarifa zinasema Morrison ameshawasili kambini Jioni ya leo na amefanya mazoezi katika Uwanja wa Mo Arena Uliopo Bunju.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Pablo alainishiwa kazi Bara.​

pablo pic

SIMBA juzi ilimalizana nan Asec Mimosas ya Ivory Coast katika mechi ya kwanza ya Kundi D ya michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika, kabla ya kurudi uwanjani wiki hii kucheza na Ruvu Shooting, huku kocha Pablo Franco akilainishiwa Bara.
Simba itavaana na Ruvu kesho kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, kabla ya kutimka kwenda Niger kucheza mchezo wao wa pili wa michuano ya CAF dhidi ya wenyeji wao, US Gendermarin kisha kuifuata RS Berkane ya Morocco.
Mechi hizo za CAF zinapigwa kati ya Februari 20-27 kisha itarudi katika Ligi Kuu Bara na ndani ya Machi na Simba itacheza michezo mitatu, huku miwili ikiwa ya nyumbani ambazo kama Pablo atakomaa nazo badi huenda akaitia presha Yanga.
Yanga ndio vinara wa ligi hiyo ikiwa na pointi 36 baada ya mechi 14 ikisubiri kukamilisha duru la kwanza wiki ijayo dhidi ya Mtibwa Sugar kabla ya kuanza mechi za duru la pili Februari 27 kwa kuivaa Kagera Sugar jijini Dar es Salaam.
Hata hivyo, Yanga imekuwa na presha kubwa kutokana na watani wao waliopo nyuma yao walivyozipunguza pointi kutoka 10 hadi kuwa tano, licha ya kuwa mbele kwa mchezo mmoja. Simba imeshacheza mechi 15 na ina pointi 31.
Pablo anaweza kuongeza presha zaidi kwa Yanga, kama timu yake itazitumia vizuri mechi zao mbili kati ya tatu watakazocheza ndani ya Machi kupunguza zaidi pengo la pointi, huku akiiombea Yanga ivurunde kwenye mechi zao zijazo.
Ratiba inaonyesha Simba ndani ya Machi itavaana na Biashara Utd (Mar 03), kisha itaikaribisha tena Dodoma Jiji katika mechi ya Machi 7 kabla ya kusafiri kuifuata Polisi baadaye Machi 27 mara itakapomaliza majukumu yake ya kimataifa. Kama itashinda zote itavuna pointi tisa.
Ratiba ya Yanga inaonyesha ndani ya Machi itacheza mechi mbili tu moja ya ugenini dhidi ya Geita Gold siku ya Machi 6 kisha Machi 16 italizana na KMC jijini Dar es Salaam. Hii ina maana Yanga inasaka pointi 6 ndani ya Machi, huku Azam iliyopo nafasi ya nne kwa sasa ikiwa na mechi tatu ndani ya Machi ikiwamo dhidi ya Coastal Union itakayochezwa Machi 1 jijini Dar.
Mechi nyingine ya Azam ikiwa nyumbani ni ya Machi 05 dhidi ya Polisi kisha Machi 16 itaifuata Namungo.
Juu ya mechi hizo za Ligi zijazo, kocha Pablo alikaririwa akisema anataka ushindi ili kutimiza malengo ya klabu, huku Nasreddine alisema hataki kupoteza pointi tena baada ya suluhu ya Mbeya City wakati Abdihamid Moallin alisititiza hajaridhika na matokeo ya timu yake na kwamba anaendelea kunoa makali ili kuona wanaingia Tatu Bora.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Simba ya Kimataifa: Kwani nyie wenzetu mnafeli wapi?​

simba-13.jpg

SIMBA imeanza vizuri hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika kwa ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya ASEC Mimosas ya Ivory Coast juzi Jumapili kwenye Uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam.
Wekundu wa Msimbazi ndio pekee waliobaki wakiiwakilisha nchi kwenye michuano ya kimataifa, na mashabiki kadhaa wa Simba walisikika wakihoji kwa furaha: “Kwani nyie mnafeli wapi?”
Wawakilishi wengine wa Tanzania – Azam, Yanga, Biashara, Mafunzo na KMKM – walitolewa mapema kabisa.
Matokeo hayo ni mazuri na muhimu kwa Simba ikielekea kucheza mechi yake ya pili ya michuano hiyo dhidi ya USGN ya Niger, Februari 20, mwaka huu.
Katika mchezo wa juzi, bao la kwanza la Simba lilifungwa na Pape Ousmane Sakho dakika ya 12, lilikuwa ni bao kali lililofungwa kwa staili ya mbinuko ‘Acrobatic Style’ akiitendea wema krosi kutoka Magharibi mwa uwanja iliyopigwa na Shomari Kapombe.
Simba walianza kwa kumiliki mpira katika dakika mbili za mwanzo na kutengeneza shambulizi kupitia kwa Meddie Kagere.
Ndani ya dakika 5 za kwanza, Simba walikuwa wamepiga krosi sita na kutengeneza kona moja.
Lakini dakika ya 14, Asec walitengeneza shambulizi na Anicet Allain Oura akapiga shuti lililopaa juu ya lango.
Dakika ya 22, Kagere alijaribu kufunga bao na nusura afunge, lakini shuti lake aliligongesha mwamba wa chini.
Dakika ya 25, Simba walipata kona nyingine lakini walishindwa kuitumia vizuri. Dakika 31 Karim Konate wa Asec, alipiga shuti langoni lililodakwa na Aishi Manula.
Dakika ya 36, Pape Sakho anakaa chini na kuonyesha ana maumivu, na dakika ya 40 anaonekana ameshindwa kuendelea na mchezo, na nafasi yake inachukuliwa na Mzamiru Yasini.
Katika hali ambayo haikutarajiwa na wengi, dakika ya 45 Peter Banda anakosa bao akiwa amebaki yeye na kipa. Shuti lake linapaa juu la lango na kuacha mashabiki wakishika midomo.
Dakika 45 za kwanza, zilimalizika kwa Simba wakiwa wanaongoza bao 1-0.
Kipidi cha pili kilianza kwa spidi ya chini, timu zikiwa zimerejea kama ambavyo zilikwenda mapumziko kwa maana hakuna mabadiliko.
Dakika mbili za kwanza, 45 hadi 47, Asec walitengeneza mashambulizi mazuri moja likiwapa kona.
Dakika ya 60, Asec walisawazisha kupitia kwa Azizi Stephenie, baada ya uzembe na kujichanganya kwa safu ya ulinzi ya Simba. Joash Onyango akipiga mpira unaogonga kiungo wa Asec na mpira kumkuta Azizi aliyemtoka Henock Inonga na kuuweka mpira kwenye kamba.
Dakika ya 68, Sadio Kanoute alitolewa nje na machela na kushindwa kuendelea na mchezo, Yusuph Mhilu alichukua nafasi yake.
Meddie Kagere alitoka na nafasi yake ikachukuliwa na John Bocco dakika ya 70.
Mabadiliko hayo yaliwapa faida Simba, Mhilu aliwekwa chini dakika ya 76 kwenye 18 na Simba kupata penalti, iliyofungwa na Shomari Kapombe dakika 77.

Bocco on Fire
Ndani ya dakika mbili tangu aingie, anatengeneza nafasi mbili, finishing tamu ya Peter Banda baada ya kazi nzuri ya Bocco dakika ya 78, Simba wakaandika bao la tatu.
Banda alivua shati na kwenda kushangilia, akapewa kadi ya njano.
Dakika ya 86, Banda alikwenda nje nafasi yake ikachukuliwa na Israel Mwenda, huku Bwalya akitoka na Erasto Nyoni akaingia kuchukua nafasi yake katika kile kilichoonekana ni mabadiliko ya kuongeza ulinzi baada ya kuongoza.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Pablo: Bocco Atawashangaza Zaidi.​



273890088_5491332650882489_7739261459188953460_n.jpg


LICHA ya Nahodha wa Simba, John Bocco kushindwa kufunga kwenye mechi za Ligi Kuu Bara msimu huu, lakini
Kocha Mkuu wa Simba, Pablo Franco amesema mshambuliaji huyo atawashangaza kwa kuwa ni mfungaji bora.
Simba ikiwa imecheza mechi 15 za ligi, imetupia mabao 16 na kinara ni Meddie Kagere mwenye mabao matano na pasi moja ya bao, huku Bocco akiwa bado hajatupia bao kwenye ligi msimu huu licha ya msimu uliopita kuwa mfungaji bora na mabao 16.
Akizungumza na Spoti Xtra, Pablo alisema kuwa hana hofu na uwezo wa Bocco, hivyo anaamini
kwamba atawashangaza wengi kadiri siku zinavyokwenda.
“Ninaye hapa mfungaji bora wa viwango ambaye anacheza Simba (Bocco), anapitia katika kipindi cha mpito na ninajua kwamba anapenda kufunga na atafanya hivyo bila mashaka.
“Ikiwa una mfungaji bora, hakuna haja ya kuwa na mashaka kwa kuwa muda upo na kuna masuala mengine ambayo
yanatokea kama uchovu na ushindani kuwa mkubwa, hilo tumeliona na tumelifanyia kazi,” alisema.
Bocco ambaye msimu huu amekuwa akikosolewa sana kutokana na kushindwa kufanya vizuri, juzi Jumapili alionekana shujaa katika ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya ASEC Mimosas wa Kombe la Shirikisho Afrika ambapo kuingia kwake kulibadili mambo.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Mbinu zilizoibeba Simba kuiua Asec.​

mbinu pic

HII ndio Simba. Achana na kikosi cha Simba ambacho kinapata ushindi wa kusuasua Ligi Kuu Bara, lakini kwenye mashindano ya kimataifa wameanza na moto.
Simba ndio wawakilishi pekee wa Tanzania kimataifa na juzi walianza vizuri Kombe la Shirikisho Afrika baada ya ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Asec Mimosas.
Mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu Bara wapo katika hatua ya makundi na ushindi huo una maana kubwa kwao kwani michezo miwili inayofuata wanacheza ugenini dhidi ya USGN na RS Berkane.
Katika mechi ya juzi, Simba kipindi cha kwanza walitangulia kwa bao 1-0 hadi mapumziko lililofungwa na Pape Ousmane Sakho, lakini haya ndio yaliyoibeba Simba katika mchezo huo.

ASEC 10 NYUMA
Katika mchezo huo, Asec waliingia na plani ya muda mwingi kujilinda na walikuwa na wachezaji tisa mpaka kumi katika eneo lao la kujilinda ili kuwapa Simba wakati mgumu kufunga bao.
Baada ya Simba kufunga bao lilitokana na krosi ya Shomary Kapombe na Sakho kufunga kwa mtindo wa aina yake wa tiki taka ndipo Asec walianza kufunguka na kwenda kushambulia na kuacha kucheza kwa kujilinda zaidi.
Ukiachana na Asec, timu zingine ambazo Simba imecheza nazo msimu huu katika Ligi Kuu Bara zikicheza kwa mfumo huo ni Coastal Union, Mbeya City, Kagera Sugar na Mtibwa Sugar.

KIUNGO NOMA
Kipindi cha kwanza eneo ambalo Simba walifanikiwa kutawala na kuzalisha bao lilikuwa la kiungo ambalo walianza Jonas Mkude, Sadio Kanoute na Rally Bwalya .
Pale walipocheza eneo hilo Simba walianzisha mashambulizi hatari ikiwemo shuti la chini lililopigwa na Meddie Kagere likagonga mwamba wa goli la Asec.
Kutawala kwa Simba eneo la katikati kulianzisha shambulizi lingine hatari ambalo lilitumiwa na Sakho kufunga bao akiunganisha krosi ya Kapombe.
Simba walipojaribu kushambulia kwa mipira mirefu bila kupitia katika eneo la kati hawakuwa na madhara zaidi na walipoteza mipira mara nyingi.
Ubora wa Sakho aliyecheza kwa dakika 40 na kutolewa akingia Mzamiru Yassin ulikuwa katika kiwango bora na aliwasumbua mabeki wa Asec kila alipokuwa na mpira.

NAFASI MURUA
Simba katika mechi hiyo miongoni mwa mambo ambayo walifanikiwa kutawala ni kucheza katika maeneo tofauti na kuyamiliki kwa kupiga pasi ndefu na fupi za uhakika.
Kucheza huko kwa Simba kuliwapa nafasi ya kufunga mabao matatu, lakini muda waliolazimisha kucheza kwa aina tofauti kama ile mipira ya juu hawakufanikiwa walipoteza mipira mingi.
Kucheza huko kwa Simba kuliendelea kuimarisha ubora wa kikosi hicho kwani walitengeneza nafasi sio chini ya tatu kwa wachezaji tofauti, ila walipoteza kutokana na kukosa utulivu na umakini.
Miongoni mwa nafasi ambazo Simba walikosa kuzigeuza kuwa mabao ni ile ya Meddie Kagere, Peter Banda, Rally Bwalya na nyinginezo.

KUJIAMINI ZAIDI
Miongoni mwa makosa ambayo yanaendelea kuwagharimu Simba msimu huu ni mabeki kucheza kwa kujiamini mara baada ya kuwa mbele kwa matokeo.
Kujiamini huko kulimfanya beki Joash Onyango kufanya kosa ambalo halikuwa na ulazima kupoteza mpira mbele ya mchezaji wa Asec, Aziz Stephane na kupata urahisi kufunga bao la
kusawazisha. Kosa hilo la kucheza kwa kujiamini zaidi kwa mabeki sio tu kwa Onyango, bali hata Henoc Inonga amekuwa akifanya hivyo kwenye baadhi ya mechi za mashindano.
Onyango na Inonga wanatakiwa kubadilika haraka katika aina hiyo ya uchezaji kwani wasipobadilika wanaweza kujikuta wanaigharimu zaidi timu yao.

MABADILIKO SIMBA
Baada ya Asec kupata bao la kusawazisha walikuwa wakicheza kwa kujiamini na kuendelea kuimarisha eneo la ulinzi ambalo halikuwa linafanya makosa mara kwa mara.
Benchi la ufundi lilifanikiwa kwa kiasi kikubwa katika mabadiliko ya ya pili kuingia John Bocco na Yusuph Mhilu.
Bocco aliyekuwa katika kiwango bora kwa dakika alizochezea alihusika na mabao mawili yaliyowapa Simba ushindi wa kwanza wa michuano hiyo. Bao la pili ambalo lilikuwa la penalti lilitokana na uhodari na kujitoa kwake alipokwenda kuchukua mpira kwenye mstari wa kutoka na kupiga krosi ambayo kipa wa Asec alishindwa kuokoa vizuri mpaka kumchezea rafu Mhilu ndani ya boksi na mwamuzi kuamuru kuwa ni penati uliyopigwa na Kapombe.
Ubora wa kuomba mpira kwenye njia, uharaka na utulivu mkubwa aliokuwa nao Bocco ulizaa bao la tatu lililotokana na krosi ya maana aliyopigia Banda aliyefunga bao la tatu.

MAKOCHA HAWA HAPA
Akizungumzia mchezo huyo, Kocha wa Simba, Pablo Franco alisema ilikuwa mechi ngumu kutokana na ubora wa wapinzani wao ambao waliingia na mbinu za kuwazuia na kuhakikisha hawafanyi vizuri.
“Wapinzani walikuwa katika kiwango bora. Tulibadilika aina yetu ya uchezaji ili kupata pointi tatu dhidi yao na tulifanikiwa hilo,” alisema Pablo.
“Mechi hii imetupa mwanga kuelekea nyingine zilizo mbele kwani tunaenda kucheza ugenini na huko tunatafuta pointi kama ilivyokuwa nyumbani.”
Kocha wa Asec, Julien Patrick alisema ilikuwa mechi ngumu na walifanya makosa yaliyowarahisishia Simba kufunga mabao mawili ya haraka yaliyoamua mechi.
“Kuna wakati katika kipindi cha pili tulishika mchezo, tulikuwa na uwezo wa kushinda ila ubora wa Simba hasa katika eneo la kiungo ulichangia ku tuzidi,” anasema Patrick.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Simba yapewa mchongo CAF.​

mchongo pic


NI mwanzo mzuri kwa Simba, kupata pointi tatu hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika (Caf), kumewaibua wachezaji wa timu nyingine kuwapa mbinu za kushinda ugenini.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Simba, Salim Abdallah ‘Try Again’ alisema kwanza anawashukuru mashabiki wa Simba kwa kujitokeza kwa wingi uwanjani na waendelee kusherekea.
Alisema wanachohitaji zaidi ni umoja zaidi kwani wamepania kufanya mambo makubwa kwenye michuano hiyo ya kimataifa msimu huu na si lazima kila silaha wanayotumia waiweke wazi kwa maadui zao kwani wanajua na wana uzoefu mkubwa na timu za Afrika. Anasema sababu kubwa ya kushinda mechi ya juzi ni mshikamano baina yao na wamejipanga vizuri kila hatua ya wanayokanyaga ndio maana amewataka mashabiki kuwaombe na kuwapa sapoti kubwa iliyoko ndani ya uwezo wao kila wanapocheza.
Alisema wanaendelee kupambana kwani Simba ni timu kubwa na wanajua kucheza mechi kama hizo za kimataifa na kila mmoja ameona kilichotokea kwa
Asec Mimosas.
“Tulizungumza na wachezaji na tuliweka mipango ya mpira na ukweli katika eneo hilo Simba tupo vizuri, tuna utulivu wa kutosha na tunatambua nini tunafanya,” alisema Try Again na kuongeza;
“Tulikaa na wachezaji wetu, tulikaa na benchi la ufundi tulijua Mimosas ni timu ngumu na haifungiki kirahisi na tunajua historia yao hawajapoteza mechi na tulifanya kile kinachostahili kufanyika hatimaye tumepata matokeo mazuri,”
“Siri ya Simba kufanya vizuri katika mashindano ya kimataifa maana yake ni mcheza kwao hutunzwa hakuna zaidi ya hapo. Mipango yetu katika mechi zijazo niweke wazi na watu wote wafahamu haya mashindano ya kimataifa ndio mashindano yetu, ndio levo yetu na nafikiri wametangaza mashindano ya (Super Cup) na tutakwenda kucheza huko na sisi ni timu kubwa tupo tayari kwa hilo.
“Yote kwa yote niwambie Wanasimba tumejipanga na tunajua tunachokifanya na tuna mipango mizuri na kuhakikisha tunapasua katika mashindano haya ya kimataifa kwani haya kwetu ni mashindano ya kawaida.”
Katika hatua nyingine bosi huyo alisema hata mechi ijayo dhidi ya USGN ya Niger inayotarajiwa kucheza Februari 20 Jumapili, watafanya vizuri huku wachezaji pia wakishauriwa cha kufanya na wakongwe mbalimbali.
Kipa wa Ruvu Shooting, Mohamed Makaka alikiri Simba kuwa nzuri michuano ya Caf, pamoja na hilo alishauri mastaa kuusoma mchezo unataka nini na kuongeza umakini hadi kipenga cha mwisho (dakika 90).
“Simba ina uzoefu mkubwa na michuano hiyo, ninachoweza kuwashauri mastaa wa timu hiyo, kila mmoja akafanye kazi yake kikamilifu, naamini watafanikiwa zaidi na ndio wanaoiwakilisha nchi kwa sasa,” alisema Makaka na kuongeza;
“Wakipata bao la kuongoza wajitahidi kulilinda na kutoridhika wakijua wapinzani wao wapo kwa ajili ya kutaka ushindi, safu ya mbele mmoja akikabwa sana wengine watumie nafasi hiyo kufunga.
Wakati Kipa wa Mbeya City, Deogratius Munishi ‘Dida’ alisema kuwa; “Ujue wasiichukulie Simba kufungwa mechi mbili na sare sare nne haimanishi wana timu mbaya ni upepo tu ndio maana mechi ya juzi wamewafunga wapinzani wao.”
Simba msimu huu imepania kucheza nusu fainali ya Shirikisho Afrika ikiwa ni hatua kubwa zaidi kwao kwenye mashindano hayo yenye fedha nyingi Afrika. Try Again ameweka wazi malengo yao waliyompa Kocha ni kubeba ubingwa wa Ligi Kuu Bara na Kombe la FA pamoja na kucheza nusu fainali ya Kombe la Shirikisho la Afrika. Simba ipo kundi moja na timu za RS Berkane ya Morocco, USGN ya Niger pamoja na Asec ya Ivory Coast ambayo mpaka jana mchana bado ilikuwa Jijini Dar es Salaam haijarudi kwao.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Sakho, Kanoute Fiti Kuwavaa Ruvu.​

SIMBA-5.jpg

VIUNGO tegemeo hivi sasa katika kikosi cha Simba, Ousmane Pape Sakho na Sadio Kanoute wote wapo fiti na vizuri kuwavaa Ruvu Shooting.
Nyota hao wote walipata majeraha katika mchezo uliopita wa hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika uliochezwa wikiendi iliyopita dhidi ya Asec Mimosas ya nchini Ivory Coast.
Kurejea kwa viungo hao kutaimarisha kikosi hicho kinachonolewa na Kocha Mkuu Mhispania, Pablo Franco na msaidizi wake, Selemani Matola.
Akizingumza na Championi Jumatano, Meneja Habari na Mawasiliano wa timu hiyo, Ahmed Ally alisema kuwa,
viungo hao wote juzi Jumatatu walifanyiwa vipimo na kuonekana kutopata majeraha makubwa.

SIMBA-4-1.jpg

Ally alisema kuwa, baada ya vipimo walivyopatiwa viungo hao, madaktari wakashauri wapumzike kwa siku moja
kabla ya leo Jumanne kuanza mazoezi ya pamoja na wenzao tayari kwa kuwavaa Ruvu.
Aliongeza kuwa kurejea kwa viungo hao kutaimarisha kikosi chao ambacho bado kina majeruhi wawili ambao bado
hawajapona vizuri Chris Mugalu, Kibu Denis na Taddeo Lwanga wanaoendelea na mazoezi binafsi. “Sakho na Kanoute wote wapo fiti na leo (jana) wamejumuika kwenye mazoezi ya pamoja na wenzao kujiandaa na mchezo wa FA dhidi ya Ruvu Shooting.

SIMBA-8.jpg

“Hiyo ni baada ya uchunguzi wa daktari Sakho na Kanoute wakapewa mapumziko ya siku moja ambayo ni jana (juzi Jumatatu) kabla ya leo (jana) kurudi mazoezi kujiandaa na mchezo huo.
“Mchezo huu ni muhimu kwetu kupata matokeo mazuri kutokana na malengo yetu tuliyojiwekea kutetea mataji yote tunayoshindania katika msimu huu,” alisema Ally.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Kocha ASEC aukubali mziki wa Simba SC.​

simba-13.jpg

KOCHA Mkuu wa Asec Mimosas, Julien Chevalier raia wa Ufaransa, ameukubali muziki wa Simba na kuweka wazi kuwa ameamini wapinzani wao hao kuwafunga wakiwa uwanja wao wa nyumbani, ufanye kazi kubwa sana.
Chevalier alisema mbali ya ubora wa kikosi cha Simba, wamekuwa na nguvu kubwa ya mashabiki ambao amekiri walikuwa na mchango mkubwa kwenye ushindi waliopata.
Juzi Jumapili, Simba ikiwa Uwanja wa Mkapa, Dar, iliibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya ASEC Mimosas ukiwa ni mchezo wa kwanza wa Kombe la Shirikisho Afrika Kundi D.
Chevalier alisema: “Kusema ukweli Simba walikuwa wanastahili kushinda dhidi yetu kutokana na ubora mkubwa wa kikosi chao na nguvu yao wakiwa wanacheza nyumbani.
“Tulijitahidi kutumia mbinu na mipango yetu, lakini hatukufanikiwa, mashabiki wao walikuwa msaada mkubwa kwao wakiongezewa hamasa.
“Wachezaji wangu wengi vijana, kelele ziliwaathiri kwa sababu wamekaa miaka miwili bila uwepo wa mashabiki viwanjani kutokana na corona.”
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Simba: Msihofu Wametushikia Nafasi Yetu.​

simba-16.jpg

LICHA ya Yanga kuongoza Ligi Kuu Bara kwa tofauti ya alama tano, aliyekuwa Mwenyekiti wa Simba, Hassan
Dalali, amesema kuwa Yanga imewashikia kwa muda tu nafasi yao.
Yanga kwa sasa wako kileleni mwa ligi kuu wakiwa na pointi 36 baada ya kushuka dimbani mara 14 ambapo
wameshinda mechi 11 na sare tatu.
Simba wao wamecheza mechi 15, wameshinda tisa, sare nne na kupoteza mbili wako nafasi ya pili na alama zao 31.
Dalali aliliambia Championi Jumatano kuwa: “Kuhusu ubingwa wa Ligi Kuu Bara hilo halina ubishi wale wenzetu wametushikia nafasi yetu na muda utakapowadia tunakwenda kuwashusha na safari ya ubingwa itaanzia hapo, kikubwa tuwe wamoja tusitengeneze makundi ambayo yatakuja kutuvuruga na tukatoka kwenye malengo yetu.”
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Simba Wampa Masharti Mawili Morrison.​

bm3gh_235895398_355056516250960_4071643913854102453_n.jpg

UONGOZI wa Simba licha ya kumsamehe winga wao, Bernard Morrison, lakini wamepatia masharti ambayo anatakiwa kuyafuata baada ya kupewa msamaha huo ndani ya kikosi chao.
Morrison alisimamishwa ndani ya timu hiyo kutokana na vitendo vya utovu wa nidhamu alivyoonyesha huku uongozi wa Simba ukimtaka mchezaji huyo kuandika barua ya maelezo kwenda kwa CEO wa timu hiyo, Barbara Gonzalez jambo ambalo Morrison alilitekeleza
Akizungumza na Championi Jumatano, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmedy Ally alisema kuwa
tayari uongozi wa timu hiyo umepokea barua ya maelezo ambapo mchezaji huyo aliomba msamaha kwa maandishi na maneno baada ya kukutana na uongozi wa Simba ambao baada ya kumsamehe umempa masharti ya kuwa mfano mzuri wa kuigwa ndani ya timu hiyo na kutorudia vitendo vya utovu wa nidhamu.
“Jumatatu mchana Bernard Morrison aliwasilisha barua ya msamaha kwa uongozi wa Simba ambapo alikutana na uongozi wa timu wakazungumza na Morrison alipatiwa msamaha na siku hiyohiyo alijiunga na wenzake na kuanza rasmi mazoezi.
“Katika msamaha ambao amepewa winga huyo anatakiwa kuacha kufanya tena vitendo vya utovu wa nidhamu na kuwa mfano wa kuigwa kwa wachezaji wengine ambapo mwenyewe amekiri kuwa atafanya hivyo na kuwa mfano bora wa kuigwa na kucheza kwa kujituma ndani ya timu hiyo,” alisema kiongozi huyo.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Mwameja: Bocco hajachuja ila...​

Bocco PIC

LICHA ya baadhi ya mashabiki wa soka kumtazama kwa jicho la kushuka kiwango nahodha na straika wa Simba, John Bocco, lakini nahodha wa zamani wa timu hiyo, Mohammed Mwameja ameshauri nyota huyo kupatiwa huduma ya kisaikolojia ili kuwa sawa.
Hata hivyo, Bocco ambaye amekuwa akishtumiwa kwa kutofunga mabao katika siku za karibuni, kwenye mechi ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Asec Mimosas alisaidia upatikanaji wa mabao mawili kati ya matatu iliyopata Simba katika ushindi wa mabao 3-1.
Wakati Bocco akianza kurejea taratibu katika anga zake, Mwameja amekwenda mbali zaidi na kusisitiza kuwa ni miongoni mwa washambuliaji watatu bora kwake na hajachuja kama ambavyo baadhi ya mashabiki wamekuwa wakifikiria.
“Namuona Bocco kama mshambuliaji namba moja Tanzania bila ubishi kwa washambuliaji wetu wazawa. Kwenye tatu bora hakosekani hiki anachopitia sasa ni upepo na huwa inamtokea mchezaji yeyote,” alisema katika mahojiano maalumu na Mwanaspoti.
Alisema kinachomkuta Bocco sasa ni
kuwa kwenye mwendelezo tofauti na ni kipindi cha mpito ambacho ili kukiepuka tiba yake ni kupata mtaalamu wa saikolojia.
“Ana kiwango bora. Hajachuja na bado anaweza kuwa tegemeo kwenye kikosi cha Simba kama atapata mtu wa saikolojia kumuweka sawa na maneno ya nje ya uwanja hasa yale ya kukatisha tamaa asikubali yakae kwenye akili.”
Japo hivi karibuni Bocco hakutaka kuzungumzia kipindi hiki anachopitia, Mwameja alisema anapaswa kukichukulia kuwa ni cha mpito, atulie na akianza kufunga atafunga hadi watu watashangaa.
“Soka la Tanzania lina makocha makocha wengi. Wapo wenye fani lakini pia lina makocha wasio na fani, hivyo ukiwasikiliza wote wanakuvuruga,” alisema.
Kuhusu safari ya ubingwa msimu huu, Mwameja alisema mbali na Yanga na Simba pia kuna Azam na Mbeya City zinapaswa kutazamwa kwa jicho la tatu.
“Ubora wa kikosi cha Yanga msimu huu nafasi iliyopo kwenye msimamo ni dhahiri inampa presha Simba kutetea ubingwa, lakini tusiziangalie hizo timu mbili tu kuna Azam na Mbeya City zinakuja vizuri.
“Tangu Azam wamebadili kocha kuna mabadiliko. Hivyo lolote linaweza kutokea aliyetarajiwa kuwa bingwa au mshindi wa pili ikawa tofauti,” alisema.
Yanga ina pointi 36, Simba 31, Azam ni ya tatu na pointi 24 ilhali Mbeya City ina pointi 23. Simba pekee ndio imemaliza mechi za raundi ya kwanza lakini nyingine zimesalia na mechi moja kila moja.
“Hapo ukiteleza tu maana yake umeachwa. Nauona mzunguko wa pili utakuwa ni wa kufa na kupona,” alisema.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Morrison Alizua Upya Simba.​

simbasctanzania_271464146_1004142703514157_1878481776837137082_n.jpg

UNAAMBIWA mara baada tu ya kuingia kambini, nyota wa Simba, raia wa Ghana, Bernard Morrison, amejikuta
akizua jambo jipya baada ya kugoma kuhamishwa chumba cha kulala.
Morrison alikuwa nje ya kikosi hicho tangu Februari 4, baada ya kusimamishwa na uongozi wa timu hiyo kwa makosa ya utovu wa nidhamu aliouonyesha kwa baadhi ya uongozi na benchi la ufundi.
Chanzo chetu kutoka kambi ya Simba iliyopo Ndege Beach jijini Dar es Salaam, kimesema kuwa, mara baada ya juzi Ju– matatu, Morrison kuwasili kambini, alijikuta akizua gumzo jipya mara baada ya meneja wa klabu hiyo, Patrick Rweyamamu, kutaka kumhamisha chumba alichokuwa akilala mwanzo, ambapo aligoma na kulazi– mika kurejeshwa kwenye chumba hicho.

273129757_1293546667789867_7183809858415196594_n.jpg

“Ebwana eeh … nikwambie siku zote mtu mtundu huwa haji– fichi tabia kabisa, yaani pamoja na Morrison
kusimamishwa kwa muda, huwezi kuamini jana (juzi) baada ya kurudi kambini tu alilizua jambo jipya baada ya kugoma kuhamishwa chumba na meneja kiasi cha kulazimika kurejeshwa
alikokuwa awali.”
Championi Jumatano baada ya kuelezwa hali hiyo, lilimtafuta Meneja Patrick Rweyamamu, ili aweze kuthibitisha uwepo wa hali hiyo ambapo alisema: “Ni kweli Morrison karejeshwa na uongozi na tayari aliingia
mazoezi ya jana (juzi).
“Hivyo mimi kwa nafasi yangu nimempokea na kumuelekeza kinachotakiwa akiwa kambini, hivyo tupo
naye na anaendelea na ratiba za kocha kama inavyotakiwa.”