Simba Sports Club Thread

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Mastaa Watatu Simba Waachwa.​

simba-2-2.jpg

WACHEZAJI watatu tegemeo wa Simba, Chris Mugalu, Kibu Denis na Hassan Dilunga, wapo katika hatihati ya
kuongozana na msafara wa timu hiyo utakaokwenda nchini Niger.
Simba leo inatarajiwa kusafiri kuelekea Niger kuvaana na US Gendarmerie kwa ajili ya mchezo wa pili
wa hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika utakaochezwa Jumapili hii.
Katika michuano hiyo, Simba wapo Kundi D na timu za ASEC Mimosas ya Ivory Coast, RS Berkane (Morocco) na US Gendarmarie (Niger).
Kwa mujibu wa taarifa ambazo imezipata Spoti Xtra, orodha rasmi ya wachezaji watakaobaki na kusafiri na timu hiyo, itajulikana mara baada ya mchezo wa Kombe la Shirikisho la Azam dhidi ya Ruvu Shooting uliochezwa jana Jumatano usiku.
Mtoa taarifa huyo alisema hadi hivi sasa wachezaji waliondolewa katika mipango ya Kocha Mkuu, Mhispania, Pablo Franco, ni Mugalu ambaye atakuwa nje ya uwanja wiki mbili, Dilunga (nje wiki tatu) na Kibu Denis.
Aliongeza kuwa, kati ya wachezaji hao, Kibu pekee ndiye ameanza mazoezi mepesi baada ya kupona majeraha.
“Rasmi kikosi kitakachosafiri kuelekea Niger kwenda kuvaana na Gendarmarie kitajulikana mara baada ya mchezo dhidi ya Ruvu.
“Mara baada ya mchezo huo kocha ataangalia hali za wachezaji wote ili kujua kama kuna majeruhi yeyote kabla ya kutangaza watakaoondoka.
“Lakini wapo wachezaji watatu ambao wenyewe wana hatihati ya kuwepo katika msafara huo kutokana na majeraha ambao ni Kibu, Mugalu na Dilunga,” alisema mtoa taarifa huyo.
Akizungumzia hilo, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally, alisema: “Hadi hivi sasa
wachezaji wenye majeraha ni Kibu, Mugalu na Dilunga. “Majeraha hayo yamewasababishia kuukosa mchezo wa Shirikisho dhidi ya Ruvu, lakini wengine wapo vizuri akina Sakho (Pape) na Kanoute (Sadio), orodha ya wachezaji watakaosafiri kwenda Niger itajulikana hivi karibuni.”
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

BEKI WA ZAMANI SIMBA AFARIKI DUNIA​


BEKI wa zamani wa Simba, Adam Suleiman ’Tata’ amefariki dunia usiku wa kuamkia leo nyumbani kwao, Tanga ambako alirudishwa kutoka Morogoro alipokuwa anaishi baada ya hali yake kuwa mbaya.
Adam Suleiman aliyeibukia Muheza Shooting akacheza pia na Reli ya Morogoro ni baba wa beki mwingine wa Simba, Miraj Adam ambaye alifuata nyayo za baba yake kwa kucheza Msimbazi.
Adam Suleiman alicheza Simba mwishoni mwa miaka ya 1980 na mwanawe aliibukia timu ya vijana ya Simba mwaka 2012, kabla ya kupandishwa timu ya wakubwa mwaka 2013, lakini baada ya misimu miwili akaachwa.

Marehemu Adamu Seleman (wanne kushoto) aliyechuchumaa kwenye kikosi cha Simba mwaka1989.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Pablo Aachiwa Msala wa Morrison Simba.​

273129757_1293546667789867_7183809858415196594_n.jpg

UONGOZI wa Simba umeweka wazi kuwa, kiungo mshambuliaji wa timu hiyo, Bernard Morrison bado hajasaini
mkataba mpya kikosini hapo, huku wakisema wanasubiri ripoti ya Kocha Mkuu, Pablo Franco mwishoni mwa msimu kuona kama atamuhitaji.
Mkataba wa Morrison ndani ya Simba unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu huu, huku kukiwa na
taarifa kwamba Yanga inataka kumrudisha kikosini kwao msimu ujao.
Akizungumza na Spoti Xtra, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmedy Ally, alisema: “Morrison bado hajapewa mkataba mpya huku mkataba wake ukiwa ukingoni.
“Lakini hili ni suala la benchi la ufundi chini ya kocha mkuu Pablo ambapo tunasubiri ripoti ya mwisho kutoka kwake kuona kama atamuhitaji basi ataongezewa mkataba wa kuendelea kusalia ndani ya timu.
“Kwa sasa Morrison bado ni mchezaji halali wa Simba na ataendelea kuitumikia timu mpaka hatima yake itakapofahamika mwishoni mwa msimu huu.”
Morrison alijiunga na Simba mwanzoni mwa msimu wa 2020/21 akisaini mkataba wa miaka miwili baada ya kumaliza mkataba wa miezi sita ndani ya Yanga aliyoitumikia kuanzia Januari 2020.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Chama apewa kazi maalumu.​

chama pic

USHINDI wa mabao 3-1 nyumbani umewapa mzuka zaidi viongozi wa Simba na sasa katika kujipanga kuhakikisha wanaendeleza kasi hiyo ugenini dhidi ya USGN ya Niger na ile ya RS Berkane ya Morocco umempa kazi maalumu Clatous Chama.
Simba ilianza vyema mechi zake za makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Asec Mimosas ya Ivory Coast katika mechi iliyopigwa Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam na Jumapili watavaana na USGN mjini Niamey, Niger.
Katika kuhakikisha mambo yanaendelea kuwa laini, benchi la ufundi la Simba limeamua kumtumia Chama katika mechi hizo za ugenini kwa kumjumuisha katika kikosi kinachoondoka jijini Dar es Salaam leo.
Kikosi cha Simba kinaondoka na wachezaji 24 akiwemo Chama ambaye licha ya kutokuwa sehemu ya mechi hizo kutokana na kwamba alishaichezea RS Berkane katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu huu, lakini ana kazi maalumu ya kuisaidia timu hiyo.
Mmoja wa viongozi wa Simba amelifichulia Mwanaspoti kwamba, wanaondoka na Chama kwa vile ni mzoefu kwenye mechi za kimataifa na kuwahi kucheza Morocco, wakiwa na nia ya kuhakikisha wanapata matokeo mazuri ugenini.
“Tumeamua kusafiri na Chama ambaye tunatambua kabisa kuwa hatakuwa miongoni mwa wachezaji watakaocheza katika mchezo huo, ila kuna sababu za kiufundi ambazo ndizo zimetufanya kusafiri naye,” alisema mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi wa timu hiyo, Mulamu Nghambi.
Licha ya wenyeji wa Simba (USGN), kufungwa mabao 5-3 katika mchezo wao wa kwanza dhidi ya RS Berkane haijawapoteza maboya viongozi wa wana Msimbazi kuwachukulia poa.
Mulamu alisema wameweka mambo sawa ili kuhakikisha timu inaenda kupata ushindi ugenini.
Alifafanua kuwa walituma watu kwenda Niger kufanya uchunguzi na tayari wamekamilisha suala la usafiri, sehemu ya kufikia na chakula.
“Ili timu ifanye vizuri lazima viongozi tuweke mazingira sawa kama usafiri, sehemu ya timu kufikia na chakula ambavyo vipo tayari. Kilichobaki ni kazi uwanjani,” alisema Mulamu.
“Baada ya mchezo huo tutaweka kambi Niger inaweza kuwa siku nne au tano kujiandaa na RS Berkane.”
Mulamu alisema katika msafara wao unaoondoka leo saa 7 mchana, mbali na Chama pia una wachezaji wengine wote isipokuwa Chris Mugalu, Denis Kibu na Hassan Dilunga walio majeruhi.
Mulamu alisisitiza wanatambua mchezo utakuwa mgumu, licha ya wenyeji wao USGN kupoteza kwa mabao 5-3 dhidi ya RS Berkane.
“Benchi la ufundi linafanya kazi yake ya kuwafuatilia wapinzani, viongozi tunafanya kazi yetu ya kuweka mazingira ya wachezaji kuwa vizuri na tumefanya hivyo,” alisema
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Kapombe kumbe alijilipua kwa ASEC​

pablo pic

BEKI wa Simba, Shomary Kapombe amekiri penalti aliyopiga katika mchezo uliopita dhidi ya Asec Mimosas ni kama alijilipua tu kwa kujiamini kwa kuvaa ujasiri baada ya kubaini wenzake walikuwa na mchecheto kwenda kuipiga.
Kapombe alifunga penalti hiyo wakati Simba ikiishindilia Asec mabao 3-1 katika mechi ya kwanza ya kundi D ya Kombe la Shirikisho Afrika baada ya Yusuph Mhilu kuchezea madhambi na kipa wa Asec, Karim Cisse.
Mara baada ya mwamuzi Souleiman Djama kutoka Djibouti kuamuru adhabu hiyo ilionekana wachezaji wa Simba kama wakikwepa kwenda kupiga kabla ya Kapombe kuubeba mpira na kufunga kiufundi.
Akizungumza na Mwanaspoti jana, Kapombe alisema aliamua kujivisha bomu hilo ambalo limewashinda wenzake kwa muda ndani ya kikosi hicho akiamini amebeba dhamana ya wana Simba wengi.
Alisema hakukurupuka tu kwenda kupiga mkwaju huo, bali ni aina ya majukumu ambayo anayafanya chini ya Kocha Pablo Franco wawapo katika mazoezi yao kwenye Uwanja wa Mo Simba Arena.
“Kila siku baada ya mazoezi ya kawaida nimekuwa na muda wa kupiga penalti na hilo ndilo lilinipa ujasiri wa kwenda kubeba jukumu hilo ambalo lilikuwa gumu,” alisema beki huyo.
Kapombe alisema tangu kuanza kwa msimu huu 2021/22 timu yao imekuwa na wimbi kubwa la kukosa penalti, hivyo haukuwa uamuzi rahisi kuufanya alioamua kuutekeleza kwa maslahi ya timu.
Mastaa waliokosa penalti Simba ni nahodha John Bocco dhidi ya Biashara United, Erasto Nyoni dhidi ya Ruvu Shooting, Chris Mugalu alikosa katika mchezo na Mbeya City, huku Rally Bwalya akikosa kwenye mechi ya Azam.
Mbali na penalti hizo za ligi, Simba pia ilipoteza penalti kupitia Bernard Morrison dhidi ya Red Arrows ya Zambia katika mechi ya marudiano ya mchujo (play-off) kuwania kuingia hatua ya makundi ya Kombe ya Shirikisho Afrika.
Kapombe aliongeza kuwa wakati anakwenda kupiga mkwaju huo alimuomba Mungu amsaidie ili aweze kupata kwa kuwa kichwani kwake kulikuwa na mambo makubwa matatu.
“Wakati nakwenda kupiga nilikuwa namuomba Mungu anisaidie nipate. Pia nilikuwa naifikiria timu, familia yangu pamoja na mashabiki ambao walikuwa wanahitaji furaha kwa wakati ule na nilimshukuru Mungu nilifanikiwa,” alisema.
Katika hatua nyingine Kapombe amewaomba mashabiki wao kuendelea kujitokeza kwa wingi kuwapa sapoti katika michezo ambayo wanacheza kwa a iwe ya ndani na hata nje ya nchi.

Nini maoni yako kuhusiana na mwenendo wa simba kimataifa;
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Mugalu, Dilunga labda Machi.​

Mugalu PIC

KLABU ya Simba inayoondoka mchana wa leo itaendelea kuwakosa nyota wake wawili wa kikosi cha kwanza, Chris Mugalu na Hassan Dilunga watakaokuwa nje ya uwanja hadi Machi huku akikosa mechi kadhaa ikiwamo kimataifa.
Simba inaenda Niger kisha kuunganisha Morocco kwenye mechi mbili za Kombe la Shirikisho Afrika ikiwa Kundi D siku chache tangu itoe dozi nene kwa Asec Mimosas ya Ivory Coast katika mechi ya kwanza.
Wawakilishi hao wa nchi waliinyoa Asec mabao 3-1 na usiku wa jana ilikuwa ikimalizana na Ruvu Shooting katika mechi ya Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) kabla ya leo mchana kusafiri kwenda Niger kuvaana na US Gendermarin.
Lakini ikiwa kwenye maandalizi ya safari hiyo imebainika nyota wake watatu hawatakuwa kwenye msafara akiwamo Kibu Denis, Mugalu na Dilunga walio majeruhi na daktari wa timu hiyo, Edwin Anakret alifafanua kila mmoja na tatizo lake.
Anakret alisema kila mmoja anasumbuliwa na majeraha yake hivyo wataukosa mchezo ujao wa Kimataifa na mingine ya ligi.
Alisema Mugalu aliumia kidole katika mchezo na Mbeya Kwanza ambao Simba ilishinda bao 1-0 na atakuwa nje ya uwanja wiki mbili akiwa chini ya uangalizi wa daktari. Kuhusu Dilunga aliumia mguu wakiwa ma-zoe-zini kujiandaa na Asec Mimosas ambaye atakuwa nje wiki tatu. “Baada ya wiki mbili Mugalu ataanza mazoezi mepesi, lakini Dilunga atasubiri vipimo tena kabla ya kuruhusiwa kurudi uwanjani rasmi,” alisema Anakret.
Akizungumzia majeraha yake, Mugalu alisema kila jambo lina sababu zake na anaamini kwa uwezo wa Mungu atapona na kurejea tena katika majukumu yake. “Niliumia kidole cha mkono lakini kwa sasa namshukuru sana Mungu naendelea vizuri,” alisema Mugalu.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Simba Yafanya Umafia Niger.​

273803920_1332463253915113_3741366890323213274_n.jpg

UNAAMBIWA Simba tayari imetanguliza jeshi la siri nchini Niger kwa lengo la kuweka mambo sawa kabla ya timu kwenda kupambana na US Gendamarie ya nchini humo, wikiendi hii.
Jumapili hii, Simba inatarajiwa kupambana na US Gendarmerie ukiwa ni mchezo wa Kundi D la Kombea la Shirikisho Afrika utakaochezwa Uwanja wa Général Seyni Kountché uliopo Niamey, Niger.
Huu utakuwa ni mchezo wa pili kwa timu zote ambapo awali Simba ilishinda 3-1 dhidi ya ASEC Mimosas, wakati US Gendamarie ikifungwa 5-3 na RS Berkane.
Chanzo chetu kutoka Simba, kimeliambia Spoti Xtra kwamba, pamoja na kuwa na michezo ya ndani tayari uongozi umetanguliza mashushu wake kwenda Niger ili kuhakikisha wanasoma mazingira ya nchi
hiyo.
“Tunashukuru sana uongozi kwa kupata uzoefu mkubwa katika mashindano haya ya kimataifa, maana pamoja na kuhitajika kusafiri kwa pamoja, tayari kuna jeshi la siri linatarajiwa kuingia Niger kesho (leo Alhamisi) ili kuhakikisha wanasoma ramani zote za mazingira ya nchi hiyo.
“Uongozi umefanya hivyo kutokana na kuwepo na wimbi la hujuma kwa wageni kwani katika michuano hii karibia kila timu inahitaji kuvuna pointi tatu nyumbani jambo ambalo hata sisi tunalijua, hivyo kwa kutambua hilo tumejipanga kupata ushindi ugenini au sare ndiyo maana kuna watu wanatangulia kusoma mazigira,” kilisema chanzo hicho.
Spoti Xtra lilimtafuta Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally, ambapo alisema: “Ni kweli tupo kwenye mipango ya kuhakikisha watu wanasafiri mapema iwezekanavyo kwenda Niger na kwamba mara baada ya mchezo wetu dhidi ya Ruvu Shooting, mipango yote ya kikosi kuondoka itakuwa tayari na tutawafahamisha siku husika.”
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Simba Yatishia Afrika Kuvaana USGN, Niger​

274079798_1304409120060231_8391594303549882028_n.jpg

KUELEKEA michezo yao miwili ya ugenini ya hatua ya makundi Kombe la Shirikisho Afrika, uongozi wa Simba umeweka wazi kuwa umekamilisha maandalizi yote muhimu ya michezo hiyo, huku wakitamba kuwa wanataka kuvuna pointi zote sita za ugenini.
Simba inakwenda kwenye michezo hiyo ikiwa imeweka rekodi ya kufunga mabao 10 katika michezo miwili iliyopita jijini Dar es Salaam – ushindi wa 3-1 dhidi ya Asec Mimosas kwenye Kombe la Shirikisho Afrika, na ushindi wa 7-0 dhidi ya Ruvu Shooting kwenye Kombe la Shirikisho la Azam Sports.
Kiwango walichokionyesha kwenye mechi hizo mbili, kimetosha kuwaaminisha mashabiki wao kuwa Simba imerejea kwenye makali yake, na sasa wanaamini kikosi chao hakikamatiki.
Simba ambayo imepangwa kundi D la michuano ya kimataifa ya Shirikisho, inatarajiwa kuvaana na USGNkeshokutwa Jumapili nchini Niger, kabla ya kucheza dhidi ya RS Berkane nchini Morocco Februari 27.
Kuelekea michezo hiyo, tayari maafisa wa Simba wameshawasili nchini Niger kwa ajili ya maandalizi ya mwisho ya sehemu ambayo timu inayoondoka leo itafikia na kujifua kuelekea mchezo huo.
Akizungumza na Championi Ijumaa, Mwenyekiti wa Simba, Murtaza Mangungu, alisema: “Kwanza kama sehemu ya uongozi wa Simba napenda kuwapongeza wachezaji pamoja na benchi la ufundi kwa ujumla kwa ushindi mnono dhidi ya Ruvu Shooting.
“Ushindi huo umezidi kutupa ari ya kufanya vizuri kuelekea michezo yetu miwili ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya USGN na RS Berkane ambayo kama uongozi tumefanya maandalizi yote kuhakikisha tunapata pointi zote sita ugenini, kabla ya kurejea tena kujipanga kwa ajili ya michezo miwili ya nyumbani, tunaamini kutokana na maandalizi tuliyoyafanya tutafanikiwa.”
Naye Meneja wa Habari wa Simba, Ahmed Ally, ameweka wazi kuwa kikosi hicho kinatarajiwa kuondoka leo saa 11:00 jioni kuelekea nchini Niger kwa ajili ya mchezo huo.
Kikosi hicho kinaondoka na wachezaji 23, akiwemo Clatous Chama ambaye amepewa kazi maalum, kwa kuwa hatacheza kutokana na kanuni kumbana (aliichezea Berkane katika michuano hii).
“Kikosi chetu cha Simba kinatarajiwa kuondoka na wachezaji 23 akiwemo Chama, ambaye licha ya kutokuwa sehemu ya mechi, lakini ana kazi maalumu ya kuisaidia timu hiyo.
“Hatuna hofu, uzuri tayari tulituma watu kwenda Niger kufanya uchunguzi na tayari wamekamilisha suala la usafiri, sehemu ya kufikia na chakula.
“Na mara baada ya kumaliza mchezo wetu huko Niger hatutarudi nchini na badala yake tunaunganisha Morocco kwenye mechi dhidi ya Berkane,” alisema Ally.
Wachezaji wanaotarajiwa kusafiri na timu hiyo ni Aishi Manula, Beno Kakolanya, Ally Salum, Shomari Kapombe,Israel Mwenda, Jimmyson Mwanuke, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Gadiel Michael, Joash Onyango, Pascal Wawa na Henock Inonga.
Wengine ni Kennedy Juma, Erasto Nyoni, Jonas Mkude, Sadio Kanoute, Mzamiru Yassin, Ousmane Sakho,
Peter Banda, Bernard Morrison, John Bocco, Meddie Kagere, Yusuph Mhilu na Clatous Chama.
Wachezaji watakaobaki ni watano ambao ni Larry Bwalya, Cris Mugalu, Denis Kibu, Hassan Dilunga na
Taddeo Lwanga walio na majeraha huku Bwalya akiachwa kutokana na kupatwa na msiba.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

SIMBA SC TAYARI WAPO NIAMEY KUIVAA USGD.​


KIKOSI cha Simba kimewasili salama nchini Niger jioni ya leo kuelekea mchezo wa kesho wa Kundi D Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya wenyeji, US Gendarmerie Nationale (USGD) Uwanja wa Jénérali Seyni Kountché Jijini Niamey.



 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

SIMBA SC YALAZIMISHA SARE YA 1-1 GENDARMERIE NIAMEY.​

AVvXsEgeMat1GJmJlubUrrr5J6Vrxa59iJ7BLGLphI-kbJTBWfpQaeEWz8ZR_wRlGfPPSgYmonT3DklwZNyKEPWnXeAu0gT0r-v8PPfGefTIm4gBJFapKV2Ly4NoF2MB145ijvX-A8mUy1LbPojQepOKkUjNCGLxEPMaF7kJldIETMAljW49jy_TsWATZg5t=w640-h424

MABINGWA wa Tanzania, Simba SC wamelazimisha sare ya 1-1 na wenyeji, Union Sportive Gendarmerie Nationale usiku wa leo Uwanja wa wa Jénérali Seyni Kountché Jijini Niamey nchini Niger katika mchezo wa Kundi D Kombe la Shirikisho Afrika.
Wenyeji, Gendarmerie walitangulia kwa bao la Wilfried Gbeuli dakika ya 12, kabla ya winga Mghana, Bernard Morrison kuisawazishia Simba dakika ya 84.
Kwa ushindi huo, Simba SC inafikisha pointi nne na kupanda kileleni wakifuatiwa na RS Berkane ya Morocco yenye pointi tatu sawa na ASEC Mimosa ya Ivory Coast, wakati Gendarmerie Leeds inakamilisha mechi mbili bila pointi za inaendelea kushika mkia.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Sakho, Aucho waleta vionjo vipya Bara​

sakho pic

KOCHA wa Kagera Sugar, Francis Baraza, amewazungumzia mastaa wa Simba na Yanga, Pape Ousmane Sakho na Khalid Aucho namna walivyonogesha utamu wa Ligi Kuu Bara msimu huu, kutokana na ubunifu wa kazi zaoBaraza alimtaja Sakho wa Simba kwamba licha ya kuchelewa kuonyesha madini ya mguu wake, mechi alizocheza vizuri ameona ubunifu na akili kubwa ya kazi, aliyonayo staa huyo, huku akimtarajia kufanya makubwa zaidi.
Kwa upande wa Aucho, alimuelezea ni mtaalamu wa kusambaza pasi, zinazoisaidia timu yake kuwa na umiliki wa mpira mbele ya wapinzani wao.
“Aina ya uchezaji wa Sakho na Aucho una vitu vinavyovutia macho ya wadau, kutazama kazi zao, mfano Sakho licha ya kutoanza mechi za kwanza za msimu bado anaonyesha Simba haikukosea kumsajili, akiendelea kucheza hivyo atakuwa habari nyingine,” alisema na kuongeza;
“Kuna wachezaji wengine kama Dickson Job wa Yanga, Reliants Lusajo (Namungo), Hassan Materema (Kagera Sugar), Vitalis Mayanga (Polisi Tanzania) na Fiston Mayele (Yanga) na wenyewe wameonyesha kitu kikubwa msimu huu, ambacho kinafaa kuigwa na wengine, lengo ni kuifanya ligi kuwa tamu zaidi.”
Alisema ushindani wa ligi unavumbua vipaji vikubwa, akiwatolea mfano wazawa Job, Lusajo, Materema na Mayanga kwamba wataisaidia timu yao ya taifa kufanya vizuri.
“Napenda ushindani, ndani ya ushindani kuna burudani kali na wachezaji wanakuwa wanajitoa asilimia 100,” alisema Bara alizungumza Kagera akisema moto utawaka zaidi.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Pablo hatari aongeza kocha Mzungu​

Pablo PIC

KIKOSI cha Simba kilichokuwa uwanjani mjini Niamey, nchini Niger usiku wa Feb 20 ilipokuwa ikimalizana na US Gendermarie, kinajiandaa kuanza safari kuifuata RS Berkane ya Morocco, huku kocha mkuu wake, Pablo Franco akimleta fundi mpya.
Mbali na kuleta fundi mpya kutoka Hispania anayejua soka la tiki-taka kama linalopigwa Manchester City ya Pep Guardiola, lakini kocha huyo ameanza mapema kuisoma RS Berkane ya Morocco watakayovaana nayo Jumapili hii katika mfululizo wa mechi za makundi ya michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Tuanzie hapa! Kocha Pablo amependekeza kuboreshwa kwa benchi la ufundi la kikosi hicho kwa kuongeza nguvu ya makocha wengine wawili watakaofanya kazi kwenye maeneo mbalimbali.
Kocha huyo kwanza ametaka aletewe kocha msaidizi mwingine, pia akipendekeza Mkurugenzi wa Michezo wa kuja kuongeza nguvu kikosini pamoja timu za vijana na ile ya wanawake ya Simba Queens.
Na habari za uhakika kutoka ndani ya Simba ambazo Mwanaspoti imezinasa ni kwamba katika eneo la Mkurugenzi wa Michezo, Pablo amempendekeza, Arno Buitenweg aliyewahi kufanya kazi katika timu mbalimbali kwa nafasi tofauti.
Mtaalam huyo aliyebobea kwenye soka la vijana anatajwa ni fundi wa soka la pasi nyingi maarufu kule Hispania kama tiki-taka huku akifundisha timu kutoka nchini kwao Uholanzi, Hispania ikiwamo Real Mallorca pamoja na Uarabuni.
Taarifa hiyo inaeleza Pablo amemtaka Arno kwa ajili ya kushauri na kushirikiana katika masuala ya kiufundi kwa timu ya wakubwa pamoja na kuwekeza nguvu Simba Queens na ile ya vijana ili kuzalisha wachezaji bora watakaopata nafasi katika timu ya wakubwa au kuuzwa.
Inaelezwa mabosi wa Simba baada ya kukubaliana na ombi hilo la kumleta Arno, lakini waliamua kwanza kuzungumza naye ikiwemo kumtumia majukumu atakayotakiwa kuyafanya akija nchini na kukubaliana masilahi watakayomlipa.
Japo haijawekwa wazi walipofikia, lakini kama Arno atakubaliana na majukumu hayo pamoja na maslahi atakayopata Simba atawasili nchini muda wowote kuanzia leo ili kusaini mkataba kabla ya kuanza kazi Machi Mosi 2022.
Kocha huyo aliyewahi kuinoa timu ya Ajax Amsterdam na Al Arabi SC ya Qatar na kufanya kazi na kituo cha kimataifa cha kukuza soka cha Aspire Academy, ana leseni za AFC Pro na UEFA Leseni A akifanya kazi kama kocha na Mkurugenzi wa Ufundi kwa baadhi ya timu barani Ulaya na Asia.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Simba, Barbara Gonzalez alipoulizwa kuhusu jambo hilo alisema uongozi upo tayari kuwapatia kila wanachohitaji benchi la ufundi ili kuhakikisha wanafanya vizuri na kufikia malengo ya klabu.
“Simba tuna malengo ya muda mrefu na kufanya vizuri katika kila mashindano tutakayokuwepo, hivyo tumejipanga kuboresha katika maeneo yote ikiwemo kusikiliza benchi la ufundi linahitaji vitu gani,” alisema Barbara mwenye kiu kubwa msimu huu kuona Simba inafika mbali katika michuano ya Shirikisho Afrika ambayo jana ilikuwa ikimalizana na USGN ya Niger kabla ya kuifuata Berkane ya Morocco
Kocha Pablo kwa ajili ya mchezo huo ameanza maandalizi mapema ya kuwasoma Morocco hata kabla ya kuwafuata, lengo likiwa kujua ubora na udhaifu wake akimtumia zaidi Clatous Chama waliyesafiri naye licha ya hawezi kutumika katika michuano ya CAF sababu alishacheza msimu huu akiwa na Berkane.

MDACHI ALIVYO
Arno aliwahi kuwa mkufunzi wa makocha katik Shirikisho la Soka visiwa vya Balearic kisha akaajiriwa kama kocha wa Al-Arabi na kuteuliwa kocha wa timu ya taifa ya Qatar.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Mwameja afichua siri nzito Simba​

Mwameja PIC

KATIKA sehemu zilizotangalia, kipa gwiji wa soka wa Simba na Taifa Stars, Mohammed Mwameja alizungumzia usajili wake Yanga ulivyokaribia kumtoa roho kabla ya dili hivyo kufa, ugomvi wake na Ndolanga ambao hawakusuluhishwa hadi kigogo huyo akafariki dunia na ile stori ya kuuza matikiti Uingereza badala ya soka. Endelea…
MWAMEJA ambaye sasa ni mjasiriamali akisisitiza kuwa anapenda kujiita Mmachinga anayefanya biashara zake Temeke, Dar es Salaam amesisitiza kuwa hobi yake ni soka na aliondoka Simba akiwa bado anapenda mpira na akiwa kwenye kiwango bora.
“Yaliibuka maneno maneno baada ya mechi yetu moja tuliyotwaa ubingwa, ile mechi tuliicheza katika mazingira magumu, wachezaji ndiyo tulibeba jukumu la kusafirisha timu, viongozi walikuja kwenye fainali.
“Tuliposhinda, pesa wakapewa viongozi, wakati wa kugawa wakataka baadhi ya wachezaji wapewe 300,000 na wengine 150,000, nilikataa nikasema kitu hicho hakipo, wote tupewe Sh300,000 hapo nikaonekana mjeuri na hiyo ndiyo ilikuwa moja ya vitu vilivyosababisha niondoke Simba na kuamua kustaafu,” anasema.

MSOTO WA SIMBA
Mwameja anasema ukiwa nahodha wa Simba wakati ule ilikuwa ni kama kiongozi, kuna muda unabeba jukumu la kutafuta fedha ili mambo ya timu yaende.
“Tumepitia maisha magumu, wakati ule klabu imecheza sana ndondo ili kupata huduma muhimu, kuna muda mko njiani basi la timu halina mafuta, hamjui mtakula nini, hivyo unalazimika kama nahodha kuomba msaada kwa wapenzi au timu icheze ndondo ili mambo yaende,” anasema.
“Wakati ule hakukuwa na mshahara, baadaye mwaka 1993 ndiyo tulikuja kupewa tena sio wachezaji wote, nakumbuka mshahara wangu wa kwanza ilikuwa Sh100,000 kisha 120,000 na ni mtu tu aliamua kutoa kama yeye na sio klabu.
“Kabla tulikuwa tunapata bonasi kwa kila mechi, kulikuwa na mkataba wachezaji na uongozi, kabla ligi kuanza mnazungumza kwa maana kwamba ili tuchukue ubingwa, lazima mshinde hivyo tunaposhinda mechi moja bonasi ni asilimia 60, tukitoka sare ni asilimia 30 na tukifungwa ni asilimia 10, hivyo mishahara yetu tulikuwa tunaitengeneza kwa hivyo.
“Wachezaji tuliishi kwa staili ya kutengeza hamasa ili mashabiki wajae uwanjani, kuna muda unaweza kusikia baadhi ya watu wanasema wachezaji wa zamani tulipata pesa na kuzitumia vibaya, sisi tunaamua tu kunyamaza lakini maisha ya wachezaji zamani yalikuwa ni magumu sana,” anasema.
Anasema kuna hatua ilifika klabu ya Simba iko mkoani na haina pesa, hawajui watasafiri vipi kufika eneo la tukio, watakula nini au watalala wapi.
“Hizi klabu zina wapenzi, hata Mo (Mohammed Dewji sasa ni mwekezaji wa Simba) kabla hajawa mfadhili amewahi kutusaidia mafuta.
“Nilimpigia simu nikiwa nahodha, timu iko Singida tunaelekea Mwanza, dereva akasema mafuta hayatufikishi Mwanza, alitusaidia mafuta, Abood ametusaidia sana mimi nikiwa nahodha pale Simba, kama nilivyosema ukiwa nahodha ni kiongozi.”
Anasema kuna muda timu iko mkoani hawana uhakika wa kula, wanalazimika kucheza mechi za ndondo, wanapewa laki tatu inagawanywa, maisha yanaendelea.
“Tumewahi kupiga ndondo Magu, Maswa, Kyela na maeneo mengi tu, ndiyo yalikuwa maisha yetu, tuliishi kwa ndondo, bonasi na wafadhili.”
Anasema waliwahi kukwama Mwanza timu ilikuwa haina pesa wakati huohuo wachezaji walikuwa wanapaswa kucheza mechi Zanzibar siku inayofuata kwenye mashindano ya Afrika Mashariki na Kati.
“Kocha wetu alikuwa James Siang’a sasa ni marehemu, viongozi wameshasema hawana pesa ya kutulipia ndege ili tuwahi kwenye mechi ile, tukapiga hesabu kwa timu zilizopo sisi uwezo wa kufika fainali tunao, hata tukiishia nusu bado tuna uhakika wa kupata pesa.
“Mimi, Hussein Marsha na Malota Soma akiwa nahodha-msaidizi tulimpigia mpenzi mmoja wa Simba anaitwa Bituro yuko Mwanza, tukamuomba aisaidie timu tiketi 12 tu za ndege, halafu tutamlipa.”
Anasema wachezaji ndiyo waliweka dhamana, yule jamaa akampigia meneja wa ATC usiku saa nne, wakafanikiwa kupata tiketi 12 za ndege kutoka Mwanza kwenda Dar es Salaam za siku iliyofuata saa 4 asubuhi, mechi inachezwa saa moja usiku Zanzibar siku hiyo hiyo.
“Kocha alipanga timu yake tukiwa Mwanza, tukaondoka wachezaji 11 na wa 12 ni kocha Siang’a kuja Dar ili tuwahi mechi Zanzibar usiku, wengine tukawaacha Mwanza wanasubiri ratiba ya treni ili kurudi.
“Sisi tulipofika Dar tukaunganisha bandarini tukachukua boti, siku hiyo bahari ilikuwa imechafuka, tulitapika sana, tumefika Zanzibar tuko hoi, hatuna sub, tukaunganisha uwanjani, tulicheza na timu moja dhaifu sana ya Somalia, tukatoka nayo sare, tulisemwa na kubezwa sana na mashabiki kwa matokeo yale, lakini hawakujua nyuma ya pazia kuna nini.”
Anasema mechi ya pili waliifunga Tusker hadi timu ikatinga fainali na wenzao waliowaacha Mwanza tayari walishaungana na timu Zanzibar baada ya kusafiri kwa treni kwa siku kadhaa na ile mechi Simba ilitwaa ubingwa na kupata pesa za kulipa deni la Bituro.
“Viongozi walikuja siku ya fainali kupokea pesa, maana yale mashi-ndano, chakula, usafiri wa ndani na malazi tulikuwa tunalipiwa na Cecafa, kuna changamoto nyingi sana wachezaji tumepitia zamani kwenye soka letu,” anasema.

MATOLA AOSHA
Mwameja anasema baada ya Malota Soma, Matola Suleiman ndiye alikuja kuwa nahodha msaidizi, sasa mwaka 1996 walitwaa ubingwa wa Cecafa na Matola ambaye sasa ni kocha msaidizi wa timu hiyo ndiyo alikuwa ameingia Simba.
“Mimi nilikuwa nahodha mkuu, lakini Matola akaniomba nimuachie akaoshe kwenye picha kwa kukabidhiwa kombe, nikamwambia sawa.
“Sasa meneja wetu Innocent Njovu baada ya kukabidhiwa bahasha ya pesa za washindi wa kwanza, akaichukua na kuipeleka kwa viongozi badala ya kuileta kwa wachezaji moja kwa moja kama ambavyo tulikubaliana,
“Hapo ndiyo mtafaruku ambao uliniondoa mimi Simba ulianzia, viongozi walisema kuna watu wametumika sana kwenye mechi na wengine hawatumiki sana, hivyo hawawezi kupata mgawo sawa wa pesa, tukasema hicho kitu hakipo, wale wasiotumika pia wana mchango wao na tumekubaliana tunapata mgao sawa sawa.
“Ikaonekana mimi nabishana na viongozi, sikutaka maneno ikabidi tu niondoke, huo ndiyo ukawa mwanzo wa mimi kustaafu, ila hawakujua sababu na sikucheza timu yoyote ile hadi leo.”

MIAKA 29 AKICHEZA SOKA
Safari ya Mwameja kwenye soka imedumu kwa miaka 29 hadi mwaka 2001 alipostaafu na kupishana na kipa Juma Kaseja, safari ambayo anasema ilikuwa ni safari nzuri na tamu kwake.
“Wenzangu nilioingia nao Simba walistaafu, wakaja wengine wakastaafu, wakaja wengine tena wakastaafu mimi nilikuwa bado nacheza, ingawa kipa ni mchezaji ambaye anaweza kudumu kwa muda mrefu uwanjani akiwa kwenye kiwango bora.
“Hata mimi nilistaafu nikiwa bado na kiwango changu tena kizuri tu, baada ya kuitumikia Simba kwa miaka 10, Coastal Union kwa miaka sita, Ndovu miaka minne, achilia mbali timu ya Bandari Tanga na timu ya kijijini nilikozaliwa ya Mwakidira Sports kwa miaka mingi, nimecheza soka kwa miaka 29,” anasema.
Anasema kila kitu katika safari yake hiyo kilibebwa na nidhamu na ukikipenda unachokitumikia na kufuata miiko, ukiongeza na kipaji unakifikia malengo,” anasema.

YANGA CHIMBUKO LA TANZANIA ONE
Katika safari hiyo ya soka, Mwameja alipachikwa jina la Tanzania One ambalo anasema alilisikia kwa mara ya kwanza akiitwa na wapenzi wa Yanga kwenye Uwanja wa Taifa (sasa Uhuru).
“Ilikuwa kwenye mechi ya Stars na Uganda, tunaingia Shamba la Bibi (Uhuru) nikasikia wananiambia wewe ndiyo Tanzania One, lakini kabla alikuwa akiitwa Ally Bushiri, baadaye Idi Pazi kidogo ndipo nikapewa mimi.”
Anasema tofauti za Simba na Yanga zipo lakini kuna baadhi ya wapenzi ukiachilia upenzi wao wanasema ukweli hasa kama mchezaji akiwa na kiwango na hayuko kwenye timu yake.
“Simba walikuwa wanasema Said Mwamba kizota yuko Yanga lakini ni bonge la mchezaji na Yanga wanasema Mwameja yuko Simba ila ndiyo kizingiti kwa timu yangu, Yanga ndiyo walianza kuniita Tanzania One, nakumbuka Simba waliwaambia kama mmemkubali nyinyi basi huyu ndiye Tanzania One halisi,” anasema.

MECHI NA TIMU YA GEORGE WEAH
Mwa-meja anasema Bushiri ndiye alikuwa mfano wake wa kuigwa, na ndiye alimhamasisha kupambana kwenye timu ya taifa baada ya kumueleza kwamba wao tayari umri umesogea hivyo akaze ili awe mbadala.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

MTU WA MPIRA: Chama anaufanya mpira wetu uonekane rahisi​

chama pic


UNABURUDISHWA na starehe gani kubwa? Ni mapenzi, soka au pombe? Wanadamu wanasema kila mtu ana starehe yake. Lakini hakuna starehe kubwa kwenye soka kama kumtazama Clatous Chama akicheza. Ni burudani kweli.
Kwa siku chache tu alizorejea nchini ametuonyesha yeye ni nani. Anaufanya mchezo wa soka uonekane kazi rahisi.
Wapo mashabiki wa timu pinzani waliobeza kiwango cha Chama katika mechi chache za mwanzo. Wapo walioanza kusema amekwisha lakini ukweli ni kwamba ndani ya muda mfupi ametukumbusha uwepo wake. Tazama pasi zake za mabao kwenye mechi ya Kombe la ASFC dhidi ya Dar City. Aliifanya Simba kuwa hatari. Alimfanya Kagere arejee katika makali yake. Ndani ya dakika 22 tu Simba ilikuwa ikiongoza kwa mabao manne na Chama ndiye alikuwa nyota wa mchezo.
Akafanya hivyo dhidi ya Mbeya Kwanza. Akafunga bao lake la kwanza kwenye ligi. Alifunga katika eneo ambalo hutegemei kuwa angekuwepo mtu anayecheza nafasi yake. Lakini kwa Chama kufunga haijawahi kuwa kazi ngumu. Ndani ya mwezi mmoja tu, amefunga mabao matano asisti nne za mabao.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Simba Haizuiliki CAF​

274079798_1304409120060231_8391594303549882028_n.jpg

MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba, Salim Abdallah Muhene ‘Try Again’ amesema kwa mikakati ya usiri kambini, umoja na ushirikiano uliopo, basi ngumu kutokea timu ya kuwazuia kufuzu hatua ya robo fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika msimu huu.
Simba wameipata jeuri hiyo baada ya kukaa kileleni katika Kundi D wakikusanya pointi nne mbele ya ASEC Mimosas, RS Berkane na US Gendarmerie.
Akizungumza baada ya Simba kupata sare ya 1-1 ugenini dhidi ya US Gendarmarie, juzi Jumapili, Try Again alisema usiri mkubwa uliokuwepo kambini baada ya baadhi ya wachezaji kuugua ghafla, ulichangia kwa kiasi kikubwa wao kuambulia pointi moja ugenini.
Try Again alisema kabla ya mchezo huo, wachezaji wao akiwemo Jonas Mkude, aliugua ghafla, lakini hakuna mtu kutoka nje ya kambi hiyo ambaye alifahamu na kuwafanya wapinzani wakutane na sapraizi uwanjani.
“Haikuwa kazi rahisi kupata matokeo haya hapa ugenini, vijana wetu walipambana sana kutokana na kucheza katika mazingira magumu. “Moja ya ugumu tuliokutana nao ni hali ya hewa ambayo ilikuwa nzito iliyosababisha baadhi ya wachezaji wetu kuugua ghafla mara baada ya kutua hapa nchini.
“Pia mazingira ya hoteli zilizopo hapa nyingi za ovyo ikiwemo hii tuliyofikia, kwa mfano leo (juzi) siku nzima hakukuwa na maji hotelini, siyo hujuma, lakini hali ya kiuchumi hapa nchini ndiyo imesababisha haya yote, lakini tunashukuru hatujapoteza mechi.
“Hivi sasa nguvu na akili zetu tunazielekeza katika mchezo unaofuata dhidi ya Berkane, tayari tumeanza maandaliz hayo. “Mtendaji mkuu wetu Barbara (Gonzalez) ametangulia Morocco kwa ajili ya kuandaa mazingira ya kambi kwa maana ya hoteli tutakayofikia na uwanja tutakaoutumia mazoezini, usafiri na chakula.
“Hivyo tutakaa hapa Niger kwa siku mbili na baada ya hapo tutaanza safari kuelekea Morocco kwa ajili ya mchezo huo,” alisema Try Again.
Kwa upande wa Barbara Gonzalez, alisema: “Tayari tumekamilisha taratibu zote za maandalizi ya kikosi chetu kuelekea mchezo dhidi ya RS Berkane, tunajua ni mchezo mgumu lakini tuko tayari.” Inaelezwa kuwa, Barbara ameongozana na kiungo mshambuliaji wa timu hiyo, Mzambia, Clatous Chama ambaye aliwahi kucheza Berkane kwa ajili ya kwenda kufanya umafia Morocco.
Naye Kocha Mkuu wa Simba, Pablo Franco, amesema: “Tulijua ratiba ya michezo yetu hii miwili tangu mwanzo, hivyo tumefanya maandalizi ya kutosha kuhakikisha tunafanya vizuri, tutacheza na RS Berkane Februari 27, mwaka huu, tunajua hii ni miongoni mwa timu ngumu zaidi kwenye kundi letu.
“Lakini jambo zuri kwetu kuelekea mchezo huo ni kuwa ndani ya kikosi chetu tuna Clatous Chama ambaye amecheza Berkane na anaijua vizuri Ligi Kuu ya Morocco, hivyo atatusaidia kuelewa mazingira.”
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Pablo: Wachezaji walikuwa wanashindwa kupumua​

pablo.jpg

KOCHA Mkuu wa Simba, Pablo Franco Martin raia wa Hispania, amefunguka kuwa wachezaji wake walikutana na hali ngumu wakiwa Niger kiasi cha kushindwa kupumua vizuri kutokana na hali mbaya ya hewa.
Pablo aliweka wazi kuwa, haikuwa kazi rahisi kwao kupata pointi moja mbele ya US Gendarmarie kwani kila kitu kwao hakikuwa rafiki, mbali na hali mbaya ya uwanja kwenye sehemu ya kuchezea, hata hali ya hewa ilikuwa tatizo.
“Wachezaji wangu wanapaswa kupongezwa sana kwa kile walichopata tukiwa Niger, kulikuwa na mazingira magumu sana, hali ya hewa ilikuwa mbaya sana kiasi cha wachezaji kupumua kwa tabu.
“Uwanja hasa eneo la kuchezea hapakuwa rafiki hata kidogo, kila kitu kilikuwa kigumu. Lakini wachezaji waliungana na kuipambania timu yao.”
Simba walipata alama moja ugenini wikiendi iliyopita na kufikisha nne kileleni mwa msimamo wa Kundi D. Februari 27 watashuka dimbani kucheza na RS Berkane ikiwa ni mchezo wao wa tatu hatua ya makundi.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Chama: Simba Fanyeni Hivi Kuiua Berkane​

chama-2.jpg

KIUNGO wa Simba, Clatous Chama amewaibia siri nyota wenzake wa klabu hiyo wakati wakijiandaa kucheza na RS Berkane akiwataka kuwa makini zaidi uwanjani na kucheza kwa malengo wakati wote wa mchezo huo.
Chama amesema kuwa wapinzani wao hao ni watu hatari na kwenye hatua kama hii ambapo kila timu huwa inahitaji kupata ushindi na kutimiza malengo ambayo wamejiwekea.
Chama alisema wakati wakiwa wanakwenda kucheza mechi yao dhidi ya RS Berkane wanatakiwa kuwa kuwa huru na kufurahia kila hatua ya mchezo huo kwani hiyo ndiyo njia pekee ya kuweza kufanikiwa.
“Kikubwa wanatakiwa watambue kuwa wapo juu ya msimamo na wanatakiwa kufanya kila kitu hili kuhakikisha wanabakia kwenye nafasi hiyo.
“Wafurahie mchezo na kuwa huru wakati wote wa mechi kwani hiyo ndiyo njia pekee ya kuweza kufanikiwa,” alisema.
Chama hatokuwepo kwenye mchezo huo dhidi ya RS Berkane kutokana na kubanwa na kanuni na mechi itachezwa Februari 27, nchini Morocco.
Chama aliitumikia Berkane kwa miezi sita, kabla ya kuvunja mkataba na kurejea tena Simba. Simba ni vinara wa kundi D wakiwa na pointi nne, huku Berkane na Asec Mimosas wakiwa na pointi tatu kila mmoja na US Gendermarie wakiwa na alama moja.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Kisa Waarabu, matajiri waongezea mkwanja Simba​

274079798_1304409120060231_8391594303549882028_n.jpg

AWALI uongozi wa Simba uliwatangazia wachezaji kuwapa bonasi ya dola 100,000 (Sh mil 231) katika kila mechi watakayoshinda, lakini kutokana na ugumu wa mechi ijayo dhidi ya RS Berkane ya Morocco, matajiri wa timu hiyo wameongeza mezani dola 50,000 (Sh mil 115.5) hivyo jumla mastaa hao watavuna zaidi ya Sh mil 300.
Wikiendi hii Simba itakuwa ugenini kupambana na RS Berkane ya Morocco, kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika, baada ya mchezo wao wa mwisho na US Gendarmarie ya nchini Niger kumalizika kwa bao 1-1.
Chanzo chetu kutoka Simba kimeliambia Championi Jumatano kwamba, uongozi wa Simba kupitia kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, Salim Abdallah ‘Try Again’ wanadaiwa kuahidi ongezeko la dola elfu 50, kwenye bonasi ya mwanzo na kufikia dola 150,000.
“Katika siku wachezaji wamewahi kuufurahisha uongozi basi ni pamoja na juzi Jumapili baada ya kupata sare katika mchezo wetu na US Gendarmarie ya nchini Niger, huwezi kuamini sare hiyo sasa imewafanya kuongezewa dau la dola elfu 50.
“Kama watashinda katika gemu hiyo ni wazi sasa mastaa wetu watarudi na kitita cha maana, maana bonasi imeongezeka kuachana na ile ya awali ambayo wamekuwa wakipewa kila mechi ya kimataifa dola laki moja,” kilisema chanzo hicho.
Alipotafutwa Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally kuzungumzia ishu hii hakupatikana.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Adebayor Amchomoa Mkongo Simba
6ED675E0-4B79-4DAD-B4C9-2AD83DA215EA.jpeg

RASMI uongozi wa Simba umethibitisha kuachana na staa mmoja mkubwa wa kigeni katika timu hiyo ili kiungo mshambuliaji wa US Gendarmerie ya nchini Niger, Mnigeria, Victorien Adebayor achukue nafasi yake.
Hiyo ikiwa ni siku chache tangu uongozi wa Simba utangaze kuwepo mipango ya kumsajili Adebayor baada ya kuvutiwa na kiwango chake walipokutana kwenye mchezo wa pili wa Kundi D katika Kombe la Shirikisho Afrika msimu huu.
Taarifa zinasema kuwa, mshambuliaji Mkongomani, Chris Mugalu, ndiye anayetajwa kuachwa kutokana na kuwa na matatizo mengi ikiwemo majeraha ya mara kwa mara.
Akizungumza na Spoti Xtra, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba, Salim Abdallah ‘Try Again’ alisema mara baada ya usajili wa Adebayor kukamilika, watalazimika kuachana na mchezaji mmoja wa kigeni.
Try Again alisema lengo ni kwa ajili ya kupata nafasi ya moja ya mchezaji wa kigeni watakayemsajili kutokana
na kubanwa na kanuni za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ambazo zimeruhusu kusajili wachezaji 12 wa kigeni idadi ambayo ndani ya Simba kwa sasa imekamilika.
Aliongeza kuwa, jukumu hilo la kumuacha mchezaji mmoja wa kigeni kati ya hao 12, lipo chini ya benchi
la ufundi linaloongozwa na Kocha Mkuu, Pablo Franco.
“Muda wa usajili bado haujafikia, hivyo kocha ana nafasi ya kuangalia mchezaji gani hawezi kuendana na falsafa yake na asiye na mchango katika timu.
“Hivyo tupo katika mazungumzo mazuri na meneja wa Adebayor ambaye katika dirisha dogo alinishawishi tumsajili, lakini kanuni za wachezaji wa kigeni zikatuzuia.
“Ili tumsajili Adebayor, basi itatulazimu kumpunguza mchezaji mmoja wa kigeni, na wale tutakaowaacha ni walioshindwa kuonesha kiwango bora cha kumshawishi kocha,” alisema Try Again.
Wachezaji wa kigeni waliopo Simba kwa sasa ni Pascal Wawa, Joash Onyango, Henock Inonga, Sadio Kanoute, Taddeo Lwanga, Pape Sakho, Meddie Kagere, Chris Mugalu, Bernard Morrison, Peter Banda, Clatous Chama na Rally Bwalya.