Simba Sports Club Thread

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Sakho, Morrison waishika Morocco, Ibenge presha imepanda​

sakho pic


SIMBA imetua nchini Morocco kisha kuanza safari ya kwenda Mji wa Berkane tayari kwa mchezo wao wa tatu wa hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika lakini kuna mastaa wawili wa wekundu hao wameanza kuamsha vita upya kwenye kambi ya wapinzani wao.
Timu hizo zinakutana Jumapili ya Februari 27, mchezo wa tatu kwenye kundi lao D linaloongozwa na Simba wenye pointi nne wakati Berkane wakiwa na pointi tatu baada ya timu zote kucheza mechi mbili.
Mchezo wa kwanza Simba ilishinda mabao 3-1 dhidi ya Asec Memosas kwenye Uwanja wa Mkapa, kabla ya kutoka sare ya bao 1-1 ugenini na USGN, nchini Niger.
Berkane watakaokuwa wenyeji wa Simba, mchezo wao wa kwanza waliifunga USGN mabao 5-3, kabla ya kupoteza kwenye mchezo wa ugenini dhidi ya Asec kwa mabao 3-1, hivyo mechi ya nyumbani itakuwa na vita kubwa ya kusaka pointi tatu.
Kocha wa Berkane, Mkongomani Florent Ibenge ameliambia Mwanaspoti kikosi chake kina mtihani mkubwa kuanza kutafuta dawa ya kuwatafutia tiba viungo washambuliaji wawili wa wekundu hao.
Alisema Pape Sakho na Bernard Morrison ndio mastaa wawili wanaotakiwa kutafutiwa tiba ya kuwatuliza wakati huu beki yao imekuwa na makosa makubwa.
“Simba ni timu kubwa, tunakabiliwa na mchezo mgumu dhidi yao, ukiangalia katika mechi zao mbili kuna watu ambao kama tunataka kushinda lazima tuwatafutie mbinu za kuwatuliza,” alisema Ibenge.
“Sakho (Pape) ni mchezaji mwepesi anayehitajika kuangaliwa sana kwa jinsi taarifa za mechi zao nilivyozipata lakini kuna yule Morrison (Bernard) ni mchezaji mzuri mwenye ubora akiwa uwanjani achilia mbali nidhamu yake, namjua vyema ni lazima tuwe na akili ya kuwazuia.
“Shida yetu ni makosa ambayo mabeki wangu wameyafanya kwenye mechi hizi mbili ni lazima tujue kucheza kwa utulivu kabla ya kukutana na Simba makosa haya ndio yametufikisha hapa kwa hizi mechi mbili,” alisema Ibenge.
Kocha huyo wa zamani wa AS Vita ya DR Congo, alisema hana wasiwasi na wachezaji wake wa eneo la ushambuliaji na kiungo juu ya ubora wao huku akicheka akihisi kiungo Clatous Chama anaweza kuwa na hatari katika kutoa siri za wachezaji wao na mbinu zao.
“Hapana Chama hawezi kutuathiri hata kama yuko Simba sasa, tunamkaribisha tu tena hapa Morocco tunatakiwa kucheza kwa ubora wetu na sio kuanza kumwangalia Chama ndio anajua hii timu kwa muda aliokaa hapa lakini hakuna tishio anaweza kuwa msaada mkubwa kwa wenzake wakati hatocheza.”
Hata hivyo, Chama hatocheza mechi hiyo na atakuwa jukwaani kutokana na kuzuiwa kikanuni. Nini maoni yako kuhusiana na kiwango cha Simba hii kimataifa,
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

GABASKI AKUTANA NA MAKIPA WA SIMBA CASABLANCA​

AVvXsEi3sZ0uPI33xTQkyYlXvanWwqLPR87uj8za2BygKKXF7aHRZC-NrqCAoks5e0g0zJofS52hy_dEQHhOgnvl_2TxXWGMfaUC_KBTzpE-7ENmaa_6Gzc0AquG4-ONLIofj8fvicd_Hzd-doX9TAOdWym0XNwaic6E2QqyLQNa4hbdE9gOA7wLs19_2_nh=w640-h426


KIPA wa Zamalek ya Misri, Mohamed Qotb Abou Gabal Ali, ‘Gabaski’ akiwa na makipa wa Simba SC, Aishi Manula, Abdul Salum na Beno Kakolanya Jijini Casablanca nchini Morocco jana.


Wakati Zamalek itamenyana na wenyeji, Wydad Athletic kesho katika mechi ya Kundi D Ligi ya Mabingwa Afrika, Simba watamenyana na wenyeji wengine, RSB Berkane Jumapili katika mechi ya Kundi D Kombe la Shirikisho Afrika.
Gabaski aling’ara kwenye fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika akiisaidia Misri kufika fainali kabla ya kufungwa na Senegal kwa penalti nchini Cameroon.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

UBISHI WA MZEE WA KALIUA: Bado Simba wana kazi ya kufanya Morocco​

simba pic

Tangu Bernard Morrison alipoenda kwenye kibendera kukatika akishangalia bao la kusawazisha la Simba dhidi ya ‘Wanija’ wa US Gendarmerie, ilimaanisha Simba wamepanda kileleni mwa kundi D, huku wakiwaacha USG wakijitafuta kusini kabisa mwa kundi.
Bernard Morrison! Bingwa wa kukera na kuwafurahisha watu wake wa Simba. Wiki iliyopita, niliandika hapa juu ya nidhamu ya Morrison na jinsi alivokuwa akiwaudhi mashabiki wa Simba.
Ni baada ya kutoroka kambini na kusimamishwa na uongozi wa klabu. Alisamehewa kama ambavyo nilitabiri na wiki moja mbele alikuwa akiwafurahisha mashabiki wa Simba.
Morrison alifanya kazi nzuri kuiunganisha kona iliyochongwa kutoka upande wa kulia na kuwapa Simba alama muhimu waliyokuwa wakihitaji ugenini.
Nilijua Morrison atatokea katika sura ya mbele ya kila gazeti la Jumatatu na kila mtu ataisahau kazi ya Shomari Kapombe. Ni kawaida ya soka.
Mara nyingi mfungaji wa bao ndiyo huibuka shujaa wa mchezo. Ni sababu hiyo mpaka leo washambuliaji wanatwaa tuzo za wachezaji bora mbele ya mabeki na viungo.
Hata hivyo bao la Morrison lilianzia kwenye kazi nzuri iliyofanywa katika duara la kona na Kapombe.
Morrison akiwa peke yake katika sanduku, Kapombe alimwona vyema na kukipima kimo chake vizuri kisha akaweka mpira kichwani mwake. Ubora wa lile bao ulitokana na umaridadi wa Kapombe.
Ni bao linalotupa majibu USGN ni timu ya kiwango gani. Si timu ya kiwango cha juu sana kuwazidi Simba.
Kushindwa kumlinda mchezaji ndani ya sanduku lenu mkiwa mnaongoza bao 1-0, ni kosa la kitoto lisilostahili kufanywa katika kiwango cha mashindano ya bara.
Haishtui kusikia hawajawahi kufika hatua ya makundi ya mashindano yoyote Afrika.
Upande wa pili bao lao pia lilitokana na uzembe wa kiungo wa Simba Sadio Kanoute.
Kanoute alikuwa na nafasi nzuri ya kuondoa hatari lakini alitaka kumiliki mpira ulioporwa na mchezaji wa USGN aliyemuona mfungaji vema aliyemtungua Aish Manula aliyekuwa katika kiwango bora sana.
Simba wanaondoka Niger na alama moja kwenda Morocco kuwakabili RS Berkane ambao wakati Simba wanapata sare wao walikuwa wanakufa mabao 3-1 pale Stade de l’Amitie kwa Asec Mimomas.
Hiyo inamaanisha bado timu tatu zina nafasi ya kutoboa kundi D mpaka sasa. Ingekuwa tofauti kama Simba wangekubali kulala dhidi ya USGN.
Simba wataenda Morocco wakijua matokeo ya kupoteza yatawaweka katika hali ngumu bila kujali matokeo yatakayotokea katika mechi ya USGN na ASEC Mimomas.
Kama Simba atakubali kupoteza Morocco, inamaanisha Berkane watapanda juu yao katika msimamo.
Kama mechi ya kule Niger itaisha kwa sare, ASEC watakuwa na alama nne sawa na Simba na kuwasogeza USGN alama mbili nyuma ya Simba.
Kama ASEC atapoteza, USGN atakuwa na alama nne sawa na Simba. Kama ASEC watashinda, watakuwa na alama sita na watakuwa wamepiga hatua mbele ya Simba.
Kumbuka hayo yote ni kama Simba watakubali kupoteza Morocco.
Hiyo ina maanisha, licha ya alama Simba waliyoipata Niger bado wana kazi ya kufanya dhidi ya RS Berkane kule Morocco.
Unaweza kusema Simba wana faida kwa sababu wana mechi mbili nyumbani, lakini kumbuka hakuna tiketi ya moja kwa moja kushinda nyumbani. Ilikuwaje dhidi ya wale makhirikhiri wa Jwaneng? Kumbuka hapohapo kwa Mkapa, Simba alipoteza dhidi ya TP Mazembe Simba day. Kwa vyovote vile, Simba anahitaji alama tatu au moja Morocco.
Simba wataenda Morocco wakijua wana kazi ngumu ya kufanya lakini vichwani mwao watakuwa wakilikumbuka jina la mchezaji wa USGN aliyeitwa Victoria Adebayor.
Ni mshambuliaji msumbufu aliyeipa safu ya ulinzi ya Simba wakati mgumu muda wote wa mchezo. Simba watatamani wasikutane na mshambuliaji wa aina yake tena.
Haitashtua kama jina la Adebayor litaanza kuhusishwa na usajili wa vilabu vya nyumabani.
Simba na Yanga wamekuwa na utaratibu wa kusajili wachezaji waliocheza vizuri dhidi yao au dhidi ya wapinzani wao.
Nasubiri kuanza kusikia Simba na Yanga wakipigana vikumbo kumsajili Adebayor.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Mkude, Mwenda wamuwahi Mwarabu​

Mkude PIC

SIMBA jana ilitua Casablanca tayari kwa safari ya kuifuata RS Berkane mjini Berkane kwa mechi ya Kombe la Shirikisho Afrika, huku nyota wao, Jonas Mkude na Israel Mwenda wakirejea mapema kuwawahi Wamorocco hao.
Wachezaji hao walishindwa kucheza mchezo uliopita wa Kundi D dhidi ya USGN ya Niger ulioisha kwa sare ya 1-1 baada ya kuugua ghafla, lakini kwa sasa wamepona na wameanza kujifua na wenzao.
Kuumwa kwa Mkude kulifanya akosekane kabisa hata katika benchi, huku Mwenda alikaa tu kwa vile kulikuwa na idadi ndogo ya wachezaji wa akiba na Kocha Pablo Franco alisema ilikuwa ngumu kwenye maandalizi ya mchezo huo ikiwemo kuwakosa wachezaji wake kutokana na kuumwa.
“Ukiangalia katika benchi la akiba kulikuwa na makipa wawili, Ally Salim na Benno Kakolanya, jambo ambalo hata Mwenda alikaa kutimiza idadi ya wachezaji ila hakuwa fiti asilimia zote,” alisema Pablo.
Hata hivyo, Daktari wa Simba, Edwin Kagabo alisema baada ya kuwapatia matibabu wachezaji hao wanaendelea vizuri na baada ya kufika Morocco watafanya mazoezi pamoja na wenzao.
“Mkude na Mwenda wote wapo sawa kiafya tofauti na ilivyokuwa siku moja kabla ya kucheza na USGN, kuhusu kama watatumika kwenye mechi ya RS Berkane hilo ni la kocha lakini wapo fiti sasa,” alisema Edwin.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

ZILITRENDI: Sangoma wa Simba alia kutapeliwa​

sangoma pic

EBWANAEEE, kama kawaida tunaendelea na mastori yaliyowahi kutrendi nchini miaka kibao iliyopita na safari hii tunalisongesha hadi 2001 lakini katika tarehe kama ya leo ya Februari 24.
Unaambiwa siku hiyo kuna stori ilibamba kinoma ilityohusu mpiga tunguri anayedaiwa kutumiwa na Simba kufanikisha ushindi wa mechi ya fainali ya michuano ya Kombe la Tusker dhidi ya Yanga.
Mwanaspoti lilipoti stori hiyo ikisema wiki chache baada ya ushindi wa penalti 5-4 iliyopata Simba dhidi ya Yanga katika fainali hiyo ya Tusker 2001, , Mganga wa kienyeji aliyetumiwa na Simba 'kuroga' mchezo huo amelalamika kwamba uongozi wa timu hiyo umemdhulumu Sh1milioni.

KOLAMU YA ENZI HIZO IMEHAMA KUTOKA GAZETI LA JUMAPILI HADI KILA ALHAMISI
Akizungumza na Mwanaspoti nyumbani kwake Vingunguti Dar es Salaam, Sangoma huyo aliyeomba jina lake lihifadhiwe alisema kabla ya mchezo huo wa fainali ya Kombe la Tusker viongozi wa Simba walimfuata ili 'aroge'.
Mganga huyo alisema Simba walimuahidi kiasi hicho cha fedha, lakini mara baada ya ushindi kwenye mchezo huo na kushinda kitita cha Sh 15Milioni iliyokuwa zawadi wa bingwa wa michuano, hakuwaona tena kumalizia deni lao.
"Lakini cha ajabu ni kuwa ilipofika Februari 16, viongozi wa Simba walikuja tena na kuniambia niwasaidie ili washinde mchezo wao na Yanga (kugombania Ngao ya Hisani), ila nikawakatalia."
Sangoma huyo alisema aliwataka viongozi wa Simba kuingia mkataba mpya ikiwa pamoja na kulipa kwanza Sh 1milioni za awali kabla ya kuwafanyia kazi wanayoitaka, lakini wakaingia mitini
Katika mchezo huo wa kuwania Ngao ya Hisani iliyotolewa na kampuni ya Bia ya Tanzania (TBL) Yanga ilishinda mabao 2-1 na kufanikiwa kutwaa taji hilo na kitita cha Sh 10milioni.
"Inaelekea wana matatizo makubwa katika uongozi wao na ndio maana hawajanilipa fedha zangu, lakini mimi sitowafanyia kitu chochote zaidi ya kumwachia Mungu," alisema.
Katibu Mkuu wa Simba, Kassim Dewji alipoulizwa kuhusiana na sakata hilo alidai kuwa hajui chochote na wala hamfahamu mganga huyo na kwamba hawana fungu la kuwalipa waganga.
"Unajua mashabiki wanapenda mambo hayo, inawezekana kuna baadhi yao walifanya hivyo lakini sio klabu, labda mwenyekiti, Juma Salum anaweza kujua zaidi kuhusu hilo."
Akizungumza na Mwanaspoti kwa njia ya simu jana kutoka Mbeya, Juma Salum alisema hajui chochote kuhusu hilo na kudai walipata ushindi wao kihalali na wala sio kwa kutumia Sangoma.
"Tungekuwa tunaamini mambo hayo tusingeagiza kocha kutoka Kenya (James Siang'a) na kama huyo mganga anatudai basi anaweza kwenda mahakamani kutushitaki."
Alidai kwamba toka wametwaa Kombe la Tusker wamekuwa wakiletewa madeni mbalimbali ambayo hawayajui.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Manula kumbe ana balaa!​

manula pic

KIPA Aishi Manula ameweka rekodi ya kibabe katika mechi mbili za makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika na bila shaka itawapa Simba hali ya kujiamini katika mchezo ujao utakaopigwa Morocco Jumapili hii dhidi ya RS Berkane ya huko.
Licha ya uwepo wa makipa wenye majina makubwa wanaochezea timu maarufu katika michuano hiyo kuliko Simba, Manula hadi sasa ndiye kinara wa kuokoa hatari nyingi langoni mwake kuliko yeyote katika raundi mbili za makundi hayo.
Kwa mujibu wa mtandao wa www .fotmob. com , Manula katika mechi mbili alizoichezea Simba dhidi ya Asec Mimosas ya Ivory Coast na US Gendarmerie ya Niger, ameongoza kwa kuwa na wastani wa kuokoa hatari nyingi ambazo kwa wastani ni hatari 5.5 kwa kila mechi.
Kiujumla katika mechi mbili, Aishi Manula ameokoa hatari 11 akimuacha anayemfuata kipa wa RS Berkane, Hamza Hamian Akbi mwenye wastani wa kuokoa mashuti 5 kwa mchezo huku kiujumla akiwa ameokoa mashuti matano.
Nafasi ya tatu inashikiliwa na kipa CS Sfaxien ya Tunisia ambaye ameokoa jumla ya hatari sita huku akiwa na wastani wa kuokoa hatari 3 kwa mechi.
Mechi dhidi ya Gendarmerie Nationale ugenini Jumapili iliyopita ambayo Simba ilipata sare ya bao 1-1 ndio imembeba zaidi Aishi Manula kwani katika mchezo huo aliokoa jumla ya hatari nane na kuisaidia timu yake kupata pointi moja muhimu huku hatari nyingine tatu akiziokoa katika mechi dhidi ya Asec Mimosas.
Lakini hakuishia kuokoa hatari nyingi tu kwenye mechi hiyo ya Gendarmerie bali pia Manula alishika nafasi ya tatu kwa makipa waliopiga pasi nyingi sahihi ambapo alipiga jumla ya pasi 21 zilizofikia walengwa kwa usahihi kati ya pasi 29 alizoelekeza kwa wenzake ikiwa sawa na 72%.
Katika viwango vya ubora kwa mchezaji mmoja mmoja katika raundi ya pili ya hatua ya makundi ya Shirikisho, Manula ameshika nafasi ya tatu katika orodha ya makipa waliofanya vizuri akipata alama 6.8 chini ya 10, nyuma ya kipa wa Al Masry, Ahmed Massoud aliyepata 7.8, huku nafasi ya pili akienda kwa kipa wa Pyramids FC, Sherif Ekramy, aliyepata 7.3.
Mafanikio hayo ambayo Manula ameanza nayo kwenye Kombe la Shirikisho Afrika ni kama muendelezo wa kung’aa kwa nyota yake katika miaka ya hivi karibuni ndani na nje ya nchi.
Kipa huyo hadi sasa ndiye anaongoza kwa kucheza idadi kubwa ya mechi za ndani bila kuruhusu bao katika misimu mitano mfululizo iliyopita ambayo minne kati ya hiyo mitano alishinda tuzo ya kipa bora na mara moja hakukuwa na zawadi kwa washindi.
Manula aliyejiunga na Simba mwaka 2017, ameshinda mataji manne ya Ligi Kuu, mawili ya Kombe la Shirikisho la Azam Sports, taji la Ngao ya Jamii mara tatu taji moja la Kombe la Mapinduzi na kutinga hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika mara mbili tofauti.
Akizungumzia kiwango bora anachokionyesha, Manula alisema ni matokeo ya kujituma, ushirikiano na mbinu bora za benchi la ufundi.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Simba kutua Berkane leo
BERKANE PIC

KIKOSI cha Simba kinatarajia kuondoka Jijini Casablanca, Morocco usiku wa leo Februari 25 kuelekea mji wa Berkane ambako Jumapili wanatarajiwa kumenyana na timu ya RS Berkane katika mchezo wa kombe la Shirikisho la Afrika.
Simba itashuka uwanjani siku hiyo ikiwa na akiba ya pointi nne kibindoni baada ya kushinda mchezo dhidi ya ASEC Mimosas kwa mabao 3-1 huku wakitoka sare ya bao 1-1 na US Gendarmerie.
Meneja wa simba, Patric Rweyemamu amesema kikosi chao baada ya mazoezi ya jioni kitaondoka kwenda Berkane tayari kwa mchezo wao wa tatu wa makundi.
"Kikosi chetu kinatarajia kuondoka usiku wa leo, na kesho kitafanya mazoezi katika uwanja ambao tutacheza mchezo wetu huo muhimu katika michuano hii," anasema Rweyemamu.
Aidha Rweyemamu amesema kikosi chao kipo fiti na salama kwa ajili ya mchezo huo na kila mchezaji ana morali ya hali ya juu kuhakikisha timu inapambana kupata matokeo.
Rweyemamu amesema, wachezaji wao wako katika hali nzuri isipokuwa Jonas Mkude ambaye ataendelea kukosekana kutokana na afya yake kutotengamaa vizuri kwa sasa.
Amesema kikosi chao chenye wachezaji 23 mmoja pekee Clatous Chama ambaye walienda naye kwa ajili ya uwenyeji wake na timu hiyo hayuko katika mipango ya mwalimu kutokana na kusajiliwa wakati akiwa amecheza michuano hiyo msimu huu.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Simba Yawatumia Wamorocco Kuwavuruga Berkane​

simba-7-1.jpg

NI jino kwa jino huko Morocco. Katika kuhakikisha wanaibuka na ushindi kwenye mchezo wao wa Jumapili dhidi ya RS Berkane, uongozi wa Simba umeamua kutumia uhusiano wao na maofisa wa Raja Casablanca ya Morocco kuhakikisha wanapata mbinu za kuwamaliza Berkane.
Simba inanufaika kutokana na kuwa na makubaliano ya ushirika na Klabu ya Raja Casablanca yaliyotokana na ziara ambayo aliifanya Ofisa Mtendaji Mkuu wa Simba, Barbara Gonzalez mwaka jana katika nchi za Morocco na Misri.
Akizungumzia mapokezi yao kutoka kwa uongozi wa Raja Casablanca ya Morocco baada ya kuwasili nchini humo, Kocha Msaidizi wa Simba, Selemani Matola, alisema:
“Tunashukuru kwa kufanikiwa kufika salama hapa Morocco baada ya safari ndefu kutokea nchini Uturuki, ambapo tulikuwa na mapumziko ya muda mfupi baada ya kutokea nchini Niger.
“Jambo lililotufurahisha zaidi ni mapokezi mazuri ambayo tumeyapata kutoka kwa uongozi wa Klabu ya Raja Casablanca ya hapa ambao kwa kiasi kikubwa wameshirikiana na viongozi wetu waliotangulia hapa kuhakikisha tunafikia mahali salama na pia kupeana uzoefu juu ya wapinzani wetu na kuhakikisha tunafanya vizuri.” Simba ikiwa Morocco inatumia pia basi kubwa la Raja Casablanca katika mishe zote nchini humo.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

MTU WA MPIRA: Ujenzi wa Uwanja Simba umekaa kisiasa​

Uwanja PIC

Jumamosi moja yenye heka heka hivi ndani ya Jiji la Dar es Salaam. Ni Jumamosi ya Desemba 11 mwaka jana. Ilikuwa Jumamosi ya pambano la watani wa Jadi Simba na Yanga kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa. Ni siku yenye hisia tofauti.
Ni Jumamosi hii Mtendaji Mkuu wa Simba, Barbara Gonzalez alionekana zaidi kwenye Mtandao wa Instagram kuliko sehemu nyingine yoyote.
Haikuwa siku nzuri sana kwake. Ya kumkuta yalimkuta pale kwa Mkapa na akaishia kulitazama pambano hilo kwenye televisheni.
Ni Jumamosi hii iliyozaa wazo la Simba kuwa na Uwanja wake wa mashindano. Baada ya Barbara kuzuiwa kuingia na watoto wadogo kwenye Ukumbi wa VVIP pale kwa Mkapa, ndipo Simba ikafikiria kujenga uwanja wake wa mashindano. Ni ajabu na kweli.
Timu yenye miaka zaidi ya 80 inafikiria kujenga uwanja wa mashindano kwa sababu mtendaji wake alizuiwa kuingia na watoto wadogo katika sehemu wanayokaa Wageni wa heshima. Tanzania haiishi vituko. Lakini unadhani hili ni tatizo kubwa? Hapana, subiri nitakueleza tatizo zaidi liko wapi.
Tatizo ni namna jambo lenyewe la Uwanja lilivyoanza. Ujenzi ukaanzia huko Twitter. Mtendaji Mkuu wa zamani wa timu hiyo, Crecentus Magori akasema kitendo cha Barbara kunyanyaswa kabla ya pambano hilo la watani kiwe msukumo wa kujenga uwanja wao.
Wazo hilo likatiliwa mkazo na Mwekezaji wa timu hiyo, Mohammed Dewji ‘MO’.
Naye akaitumia Twitter hiyo hiyo kusema kwamba muda wa Simba kuwa na uwanja wake umefika na yeye atachangia Sh2 bilioni. Ikaonekana kama habari njema kwa Wanasimba wote.
Lakini hiki ndio kilikuwa pengine ndio kituko kikubwa zaidi. Kabla ya kufahamu gharama za uwanja wenyewe, mwekezaji ametangaza kutoa Sh2 bilioni.
Ni kiasi kidogo sana kwenye ujenzi wa Uwanja. Nadhani mwekezaji alipaswa kusubiri kwanza tathmini ifanyike.
Uwanja wa Benjamin Mkapa ulijengwa Zaidi ya miaka 15 iliyopita. Uligharimu zaidi ya Sh56 bilioni. Wiki hii huko Senegal wamezindua uwanja wao wa kisasa unaoingiza mashabiki 50,000 ambao umegharimu zaidi ya Sh500 bilioni. Leo hii MO anatangaza kuchangia Sh2 bilioni kwenye Ujenzi wa Uwanja wa Simba. Kuna uwanja hapo? Akili mtu wangu.
Vituko havikuishia hapo. Mtendaji Mkuu wa Simba, Barbara akaita Waandishi wa Habari kwenye ofisi zao Masaki.
Akatangaza kuanza kwa mchakato wa ujenzi wa uwanja huo. Mchakato ukaanza kwa kuhamasisha Wanasimba wote kuchangia.
Zikawekwa namba za mitandao ya Simu za kuchangia. Zikawekwa akaunti za benki. Mchakato ukaanza. Nini kimetokea baada ya hapo?
Ni miezi miwili sasa tangu kufunguliwa kwa mchakato huo. Kwanza hadi leo, Simba haijasema inataka kukusanya kiasi gani cha fedha kwa ajili ya ujenzi huo. Haijasema uwanja huo utatengenezwa wapi. Haijatoa ramani ya uwanja. Yaani ni siasa tupu.
Ajabu zaidi ni tangu mchakato wa kuchangisha ufunguliwe, mpaka leo Simba haijawahi kusema imekusanya kiasi gani cha fedha. Yaani watu wanachanga tu kwa miezi miwili na hakuna anayejua kimepatikana kiasi gani. Inashangaza sana.
Yawezekana hii ndio harambee ya ovyo zaidi kuwahi kufanyika duniani. Hakuna hamasa ya kuchangia. Hakuna taarifa za michango. Watu hawafahamu wanatakiwa wachange kiasi gani. Uwanja wanaochangia hawajui utajengwa lini na wapi.
Hii ndio sababu nasema mchakato huo umekaa kisiasa. Ni zoezi lililokaa kimihemko Zaidi. Ina maana kama Barbara angeruhusiwa kuingia na watoto hao wadogo pale kwa Mkapa, basi mpaka leo Simba isingekuwa na mpango huo. Yaani kwa kifupi ni kwamba Simba haijawahi kuwa na mpango wa kujenga uwanja wake.
Hii mi mihemko tu iliyoanzia pale kwa mkapa, ikahamia Instagram na kisha Twitter. Mengine yote ni siasa.
Kwa kifupi sioni Simba ikiwa na uwanja wake leo ama kesho. Sioni mchakato huu ukipiga hatua yoyote.
Ni kupotezeana tu muda. Ni afadhali Yanga hawana mpango wa uwanja. Kila siku wanazindua nyimbo mpya ya kusifia klabu yao na watendaji wake.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Lwanga Afungua Mdomo Simba​

kwanga.webp

BAADA ya kukaa nje kwa muda mrefu bila kucheza ndani ya Simba, kiungo wa timu hiyo, Taddeo Lwanga, amefungua mdomo kwa mara ya kwanza akidai sasa yupo fiti.
Lwanga alisema alikuwa na muda mrefu wa kuuguza majeraha yake, hivyo kwa sasa kila kitu kipo sawa na muda wowote ataingia uwanjani kuitumikia Simba.
Akizungumzia maendeleo yake akiwa Morocco alikokwenda na wenzake kwa ajili ya mechi ya Kombe la Shirikisho dhidi ya RS Berkane, Lwanga alisema:
“Nilipata majeraha mwezi Oktoba, mwaka jana katika mchezo dhidi Jwaneng Galaxy.
“Jeraha lilikuwa kubwa, namshukuru Mungu nimepona na nipo tayari kurudi uwanjani na mashabiki watarajie kuniona hivi karibuni hasa kwenye raundi ya pili.”
Urejeo wa Lwanga ndani ya kikosi cha Simba, unazidi kuongeza uimara wa timu hiyo hasa kwenye safu ya kiungo. Simba sasa watakuwa na machaguo ya nani wa kuanza kati ya Jonas Mkude au Lwanga kucheza kama namba sita kwenye mzunguko wa kwanza.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Pablo Ataja Mechi Mbili za Kutinga Robo Fainali CAF​

simba-7-1.jpg

MARA baada y kufungwa dhidi ya RS Berkane ya nchini Morocco, Kocha Mkuu wa Simba, Mhispania, Pablo Franco, amesema ili wafuzu robo fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika, lazima washinde michezo miwili ya nyumbani.
Simba wanautumia Uwanja wa Mkapa uliopo Dar kama uwanja wao wa nyumbani katika michuano hiyo wakiwa hatua ya makundi ambapo mechi ya kwanza kucheza hapo waliifunga ASEC Mimosas mabao 3-1.
Ikiwa tayari imecheza mechi tatu, moja nyumbani na mbili ugenini, imebakiwa na tatu zikiwa mbili nyumbani dhidi ya US Gendarmarie na RS Berkane, huku moja ugenini itakuwa dhidi ya ASEC Mimosas.
Pablo amesema katika mechi hizo tatu, anahitaji kushinda mbili za nyumbani na sare ugenini kujihakikishia nafasi ya kwenda robo fainali.
“Tumekubali kupoteza ugenini, lakini katika michezo mitatu tumekuwa timu pekee ambayo imepata pointi ugenini, tuna michezo miwili nyumbani.
“Malengo yetu ni kushinda michezo yote mwili ya nyumbani na kutafuta pointi moja ugenini dhidi ya ASEC Mimosas ambao tuliwafunga nyumbani,” alisema Pablo.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Simba yabadili mbinu, yarudi kivingine CAF​

Simba1 PIC

KUFUNGWA kunauma, ukitaka kuamini hilo ni namna mastaa wa Simba walivyotua kinyonge Uwanja wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, baada ya kutoka kufungwa na RS Berkane ya Morocco.
Kipigo cha mabao 2-0 ambacho Simba imekumbana nacho huko Morocco ni cha kwanza kwao kwenye hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Hadi sasa Simba imecheza mechi tatu kwenye hatua hiyo na kuvuna pointi nne, baada ya kuifunga ASEC ya Ivory Coast kwa mabao 3-1 na kutoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Gendarmerie huko Niger.
Baada ya kutua leo Jumanne, Machi Mosi, 2022 alianza kutoka kiungo Jonas Mkude akiwa amevaa barakoa na kofia iliyoziba uso, zilipita dakika takribani tano akatoka kipa Beno Kakolanya, zikapita dakika tano nyingine akafuata Erasto Nyoni.
Baada ya hapo wakatoka wachezaji wengine kwa pamoja, huku sura zao zikiwa hazina furaha, jambo ambalo baadhi ya mashabiki wao waliishia kuwashangaa.
Mwanaspoti iliwashuhudia baadhi ya mashabiki wakishangazwa na baadhi ya wachezaji ambao walificha sura zao wakati wanawasili uwanja wa ndege, jambo ambalo baadhi yao liliwanyima uhuru wa kuwafuata kupiga nao picha.
Ndipo mkuu wa kitengo chao cha Habari, Ahmed Ally aliposema hawana wasiwasi kupoteza mbele ya RS Berkane, kwasababu sifa ya kundi lao D kila timu imeshinda kwao.
"Kila timu imeshinda kwao, tunasubiri kushinda kwetu, safari ilikuwa ndefu tunashukuru tumefika salama, wachezaji wamechoka watapata muda wa kupumzika tayari kujiandaa dhidi ya Biashara United." amesema.
 

mhariri

Mpiga Chabo
Dec 17, 2021
203
0
0

Simba wana jambo lao CAF​

Simba PIC

NAHODHA wa Simba, John Bocco amesema bado wana nafasi ya kufanya makubwa kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika, licha ya kuchapwa na RS Berkane ya nchini Morocco.
Simba imecheza mechi tatu za CAF katika kundi lao D ambazo ni dhidi ya Asec Mimosas ya Ivory Coast, ikashinda 3-1, Uwanja wa Benjamin Mkapa, huku mechi mbili ikicheza ugenini dhidi ya USGN mchezo ulimalizika kwa sare ya bao 1-1 na ilichapwa mabao 2-0 dhidi ya RS Berkane.
Jambo ambalo Bocco ameona kwenye kundi lao wana nafasi ya kusonga mbele kwa kuitumia vyema michezo miwili watakayocheza nchini.
"Tunashukuru angalau tumeambulia pointi moja ugenini, hivyo tumejipanga kuhakikisha tunashinda mechi za nyumbani ili tusonge mbele kwenye michuano hiyo." amesema Bocco na kuongeza;
"Ni michuano yenye ushindani, ila tupo kwa ajili ya kuipambania timu yetu kuandika rekodi ya aina yake kwenye michuano hii.
Mbali na kuzungumzia michuano hiyo, Bocco amesema kwa sasa wanaelekeza nguvu zao kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara uliopo mbele yao, wanacheza dhidi ya Biashara United, Alhamisi ya wiki hii.
"Hatuna muda wa kupoteza, akili zetu zimehamia kuzipambania pointi tatu za kwenye Ligi Kuu, baada ya kutoka nao suluhu kwenye mechi ya mzunguko wa kwanza." amesema.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Pablo Atangaza saa 48 za Hatari Simba​

SIMBA-1.jpg

KOCHA Mkuu wa Simba SC, Mhispania, Pablo Franco, ametangaza siku mbili sawa na saa 48 za vijana wake kupata ushindi katika mchezo ujao wa Ligi Kuu Bara.
Hiyo ni baada ya juzi Jumanne kurejea nchini wakitokea Morocco kuvaana na RS Berkane katika mchezo wa tatu wa Kombe la Shirikisho Afrika ambao ulimalizika kwa kufungwa mabao 2-0.
Timu hiyo mara baada ya kurejea nchini, moja kwa moja kikosi hicho kiliingia kambini tayari kwa ajili ya kuanza maandalizi ya mchezo wa ligi dhidi ya Biashara United utakaopigwa kesho Ijumaa kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam.
SIMBA-2.jpg

Akizungumza na Spoti Xtra, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally, alisema Kocha Pablo amepanga kuzitumia
vema siku mbili ambazo ni jana Jumatano na leo Alhamisi kwa ajili ya kukiandaa kikosi chake ili kuhakikisha wanapata matokeo mazuri.
Ally alisema mchezo huo ni muhimu kwao kupata ushindi yatakayorejesha hali ya kujiamini na morali wakielekea katika michezo yao ya Shirikisho dhidi ya Berkane, US Gendarmarie watakayocheza Uwanja wa Mkapa, sambamba na wa ugenini dhidi ya ASEC Mimosas.
“Tumetoka kupoteza ugenini dhidi ya Berkane, hii michuano mikubwa Afrika ndivyo inavyokuwa, kila timu inashinda nyumbani kwake, zamu yetu inakuja na sisi tutashinda nyumbani kwetu.
“Kiukweli safari ilikuwa ndefu, tunashukuru tumerejea salama nchini, wachezaji wamechoka watapata muda wa kupumzika tayari kujiandaa dhidi ya Biashara.
“Kocha amepanga kutumia siku mbili Jumatano na Alhamisi kwa ajili ya kukiandaa kiosi chake vema huku akiwapa muda mzuri wa kupumzika kwa ajili ya kutoa uchovu walioupata tayari kwa ajili ya michezo ijayo ya ligi ukiwemo huu unaofuatia dhidi ya Biashara,” alisema Ally.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania
Washambuliaji wa klabu ya Simba Sc Kibu Denis
🇹🇿
pamoja na Chris Mugalu
🇨🇩
wameanza mazoezi mara baada ya kupona majeraha yao yaliyokuwa yakiwakabili
Welcome Back!
⭐️

Inaweza kuwa picha ya Watu 2, watu wanacheza spoti na nyasi
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Pablo alia na adhabu TFF​

pablo pic

Kocha mkuu wa Simba, Pablo Franco leo ametema nyongo na kufukunga kuhusiana na adhabu ya kufungiwa michezo mitatu na kutozwa faini Sh3 milioni na Bodi ya Ligi Kuu Tanzania.
Adhabu hiyo ilitokana na kukataa kufanya mahojiano na wanahabari baada ya kumalizika kwa mchezo dhidi ya Mbeya City, Mtibwa Sugar sambamba na ule kati ya timu yake na Kagera Sugar ikiwa ni Sh1 milioni kwa kila mechi.
Akizungumza na waandishi wa habari kuelekea katika mchezo wao dhidi ya Biashara United hiyo kesho, Pablo anasema kuwa anashangzwa kwa adhabu hiyo aliopewa kwani anakumbuka kuwa ni mchezo mmoja tu ndio ambao hakuweza kuhudhuria mahojiano na waandishi wa habari na sio mitatu.
"Sikuhudhuria mahojiano baada ya mechi yetu na Geita Gold lakini nashangwa na kusikia kuwa sikuhudhuria pia na wa Kagera Sugar jambo ambalo sio sahihi kwani kwa kumbukumbu zangu ni kuwa siku hiyo hakukua na mahojiano baada ya mchezo kumalizika"anasema Pablo.
Pablo alifungiwa michezo mitatu na kutozwa faini ya Sh500,000 kwa kosa la kupiga teke chombo maalumu cha kuhifadhia barafu/vinywaji baridi kwenye mchezo wa ligi namba 102, dhidi ya Mtibwa Sugar.
Katika taarifa hiyo ya TPLB imeeleza kuwa hiyo si mara ya kwanza kwa Pablo kufanya tukio la namna hiyo ambapo mara ya kwanza alipewa onyo baada ya kupiga teke kiti katika mchezo dhidi ya KMC uliopigwa kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Tabora.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Try Again na mikakati mizito Simba​

Simba1 PIC

LICHA ya Yanga kutambia pointi 11 zaidi ilizoipiku Simba katika harakati za ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu huu, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa klabu ya Simba, Salim Abdallah ‘Try Again’ ameonya wana mechi 15 watakazocheza kimkakati na wanaamini kushangaza wengi.
Amesisitiza; “Sawa tunaanza mzunguko wa pili tukiwa tumezidiwa pointi 11, lakini tuna mechi 15 mbeleni, hivyo tusubiri, msiwe na haraka na mambo.”
Yanga Jumapili iliyopita ilifikisha pointi 42 na kujiimarisha kileleni kwenye msimamo ikiwapiku watani zao Simba kwa pointi 11 na kesho Wekundu wa Msimbazi wataikaribisha Biashara United ikiwa ni mechi yao ya kwanza ya mzunguko wa pili.
Hadi sasa Simba ni ya pili kwenye msimamo ikiwa na pointi 31 na ikishinda itafikisha 34 na kupunguza gepu la pointi.
Tofauti ya pointi hizo zimesababisha baadhi ya wapenzi wa Yanga kutamba kasi hiyo haitoshuka kwenye mzunguko wa pili na kila timu ishinde mechi zake.
Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Fredrick Mwakalebela alisema “Pointi 11 hadi watufikie maana yake washinde mechi tatu na kutoka sare michezo miwili, wakati huo sisi tunafungwa, jambo ambalo wasilitarajie, Yanga hii ni moto mwingine.”
Jana Try Again alisema “Timu imerejea na tunaelekeza nguvu kwenye ligi kuendeleza safari yetu ya kutetea ubingwa, hii ni ligi sio mtoano, hivyo yeyote anaweza kufungwa na kushinda na kibao kikageuka wakati wowote.
“Sawa tunaanza mzunguko wa pili tukiwa tumezidiwa pointi 11, lakini tuna mechi 15 mbeleni, hivyo tusubiri kuona bingwa atakuwa ni nani mwishoni mwa msimu.”
Alisema msimu uliopita pia waliingia kwenye mechi za mzunguko wa pili wakiwa wameachwa kwenye msimamo, lakini kibao kiligeuka na kutwaa ubingwa.

WAPINDUA MEZA
Ukichana na kichapo ilichopata Simba cha mabao 2-0, dhidi ya RS Berkane katika mchezo wa hatua ya makundi Kombe la Shirikisho Afrika ila mwenendo mzima wa timu hiyo umeimarika tofauti na ilivyoanza msimu.
Tangu ifungwe bao 1-0, kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Kagera Sugar Januari 26, mwaka huu timu hiyo imekuwa na matokeo mazuri kuanzia makombe ya ndani hadi yale ya kimataifa ikicheza michezo saba kati yake ikishinda mitano, sare moja na kupoteza mmoja.
Ilianza kutoa kichapo kizito cha mabao 6-0, dhidi ya Dar City Januari 30, 2022, mchezo wa Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) hatua ya 32, kisha ushindi wa bao 1-0, dhidi ya Tanzania Prisons Februari 3 na Mbeya Kwanza Februari 6.
Baada ya hapo ikaanza kampeni ya hatua ya makundi Kombe la Shirikisho Afrika Februari 13, kwenye Uwanja wa Mkapa na iliendeleza moto wake kwa kushinda mabao 3-1, dhidi ya Ases Mimosas kutoka Ivory Coast, kabla ya kuishushia kipigo wazee wa ‘kupapasa’ Ruvu Shooting cha mabao 7-0, katika mchezo wa ASFC hatua ya 16 bora uliochezwa Februari 16, Uwanja wa Mkapa.
Michezo miwili iliyofuata ni ya Kombe la Shirikisho Afrika ikitoka sare ya kufungana bao 1-1, dhidi ya Gendarmerie Nationale ya Niger katika mchezo wa pili wa hatua ya makundi Februari 20, kabla ya kufungwa 2-0, na RS Berkane ya Morocco.
Licha ya kupoteza mchezo huo ila bado Simba iko kwenye wakati mzuri wa kufuzu hatua ya makundi ya Kombe hilo kwani iko nafasi ya pili na pointi nne, ikihitaji pointi sita tu ili kujihakikishia nafasi hiyo kutokana na kusaliwa na michezo miwili ya nyumbani dhidi ya RS Berkane Machi 13, na Gendarmerie Nationale April 3, Uwanja wa Mkapa na mmoja wa ugenini dhidi ya Asec Mimosas Machi 20.
Kabla ya kuanza hesabu za michezo hiyo itakayoamua hatima yao, ila wanakabiliwa na pengo la pointi 11 kwenye Ligi Kuu Bara kutoka kwa wapinzani wao Yanga waliojikusanyia pointi 42, katika michezo 16, huku Simba ikiwa na pointi 31, baada ya michezo 15.
Kesho itakuwa kwenye Uwanja wa Mkapa kucheza na Biashara United na katika mchezo wao wa raundi ya kwanza waliokutana katika Uwanja wa Karume Musoma Septemba 28, 2021, zilitoka suluhu ya 0-0, huku nahodha wa Simba John Bocco akishindwa kuipatia timu yake pointi tatu muhimu baada ya kukosa mkwaju wa penalti iliyodakwa na kipa James Ssetupa dakika ya mwisho ya mchezo.
Nyota wa zamani wa timu hiyo, Bakari Malima ‘Jembe Ulaya’ alisema Simba bado ni imara tofauti na wengi wanavyoichukulia kwa sababu wachezaji wengi ni bora ila kinachowagharimu ni uchovu wa wachezaji wao muhimu kutokana na kucheza kwa misimu minne mfululizo.
“Bado wana nafasi kubwa ya kurejea katika ubora wao, unajua sio rahisi wachezaji wale wale kutumika kwa muda mrefu ingawa kwa jinsi wanavyozidi kupata matokeo chanya, inawaongezea morali kubwa na hali ya kujiamini zaidi.” alisema.
Naye Kocha wa zamani wa KMC na Mkufunzi wa makocha nchini, John Simkoko alisema.
“Endapo watatulia na kuacha kucheza kwa presha ya kuwaangalia wengine, naamini kabisa bado wana timu shindani na imara inayoweza kuleta athari kwa wapinzani wao wengine.”
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

SIMBA YAICHAPA BIASHARA UNITED 3-0 MKAPA​

AVvXsEgj0gRjaC2GB8ms2vEHBz7S-7rnYQN1OY9HV9VBHIqB18b4cDegkxRK1gSRLfwpCIxyLLnqdBRaJjAHqzSU383NX3PgtpLXdNN7D93t6b3oj54tGkvC1tbrIWzpNt2yA2rU4QncFw7XY9bnDAIuS1mJepUd4pBo0iYDHEMATNtMGLcAne9DivlkRQ6n=w640-h408

MABINGWA watetezi, Simba SC wamerejea na moto kwenye Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya kuichapa timu ngumu, Biashara United mabao 3-0 usiku huu Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Mabao ya Simba yamefungwa na winga Msenegal, Pape Ousmane Sakho dakika ya tisa na viungo, Mzawa Muzamil Yassin dakika ya 14 na Mzambia, Clatous Chama dakika ya 18.
Kwa ushindi huo, Simba SC wanafikisha pointi 34, sasa wakizidiwa nane na watani, Yanga baada ya timu zote kucheza mechi 16, wakati Biashara United inabaki na pointi zake 15 za mechi 16 nafasi ya 14.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Straika Simba Atimkia Uturuki​

176670646_543419086644680_1278133473838448039_n.jpg

STRAIKA na kinara wa mabao wa Simba Queens, Opah Clement, usiku Machi 4 alipaa kwenda nchini Uturuki kwa ajili ya kujiunga na timu ya Yikatel Kayseri inayoshiriki Ligi Kuu ya Wanawake nchini humo.
Meneja wa kikosi hicho, Selemani Makanya, amelithibitishia Championi Jumamosi, juu ya straika huyo kuondoka kikosini humo baada ya Waturuki hao kutuma barua ya kumhitaji.
“Ni kweli Yikatel Kayseri iliwasilisha barua ya kuhitaji huduma ya Opah Clement na ameelekea nchini uturuki kujiunga nao.”
Opah ndiye kinara wa mabao ndani ya Simba Queens kwa msimu huu akifunga mabao 19, pia akiiacha timu hiyo ikiongoza kwenye msimamo wa ligi kuu ikiwa na pointi 33.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Pacha Wa Chama Ampa Mzuka Pablo Simba​

chama.jpg

PABLO Franco, Kocha wa Simba amefunguka kuwa kurejea kwa viungo wake Rally Bwalya na Mzamiru Yassin kumeongeza nguvu na ari ya kufanya vizuri zaidi katika ratiba yao ngumu.
Timu hiyo itacheza mechi tatu mfululizo ndani ya siku 10, ambapo Ijumaa walianza ratiba hiyo kwa kucheza na Biashara United kisha dhidi ya Dodoma Jiji Machi 7, na mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya RS Berkane Machi 17.
Bwalya ambaye amekuwa akitumika kucheza pacha kwenye kiungo cha timu hiyo na Clatous Chama hakuwepo katika timu hiyo kutokana na matatizo ya kifamilia.
Akizungumza na Championi Jumamosi, Pablo alisema: “Tumekuwa na ratiba ya michezo mitatu migumu na muhimu dhidi ya Biashara United, Dodoma Jiji na RS Berkane, kwa kuwa michezo hii ni ya mfululizo, tunahitaji kuwa na kikosi chetu kamili na wachezaji wote muhimu.
“Nafurahi kuona tayari Mzamiru na Bwalya wakirejea kujiunga na wenzao baada ya kushindwa kusafiri nasi kwenye Kombe la Shirikisho, katika kipindi ambacho tunakabiliwa na majeruhi kurejea kwao ni wazi kumetuongezea nguvu ya kufanya vizuri zaidi.