Yanga Thread

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Manara: Hatulalamikii Waamuzi Tunawakumbusha Tu.​

FLEZL9xWQAUGozU.png

Kupitia Mkutano na waandishi wa Habari leo Feburuari 8, 2022, Msemaji wa Klabu ya Haji Manara amesema kuwa Klabu yake na viongozi hawatoi malalamiko kwa Waamuzi ila huwa wanafanya hivyo kuwakumbusha tu.
Haji Manara amesema kuwa Wajibu wao ni Kukumbusha tu, ila sio kupeleka malalamiko kwa Waamuzi kwa kuwa Klabu yao ina mashabiki na wanaona kuwa Haki Haitendeki na wao kazi yao ni Kusema kwa kuwa ndio Kazi ambayo wameichagua.
“Nilisema pale EFM hatuchezi ligi hii kuwa unbeaten tunacheza kuwa champion, Sisi ni klabu ya mpira lazima tutafungwa. Ni wenzetu tu ambao wanaamini wakifungwa wamehujumiwa.
“Sisi tunajua hii ni klabu ya mpira lazima kuna siku utapigwa.”
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Bumbuli: Simba Wameongezewa Dakika 75 Kwenye Mechi 15, Yanga Dk 34 .​

8f6fcdeb5031c74ba25a9b6c4d6082eae3935816.webp

Kupitia Mkutano na waandishi leo Februari 8, 2022 Afisa Habari wa Klabu ya Hassan Bumbuli amezitaja takwimu ambazo zinaonesha kuwa na utata katika kuweka usawa kwenye Timu ya Yanga Dhidi ya Wapinzani wao Simba.
Moja ya Takwimu ambayo ameitaja ya kwanza ni Dakika za Nyongeza ambazo hutolewa mwishoni mwa mchezo.
Bumbuli amesema kuwa katika michezo 14 ambayo Klabu ya Young Africans ilicheza kwenye Ligi Kuu msimu huu, walibahatika kuongezewa dakika 34 tu (Jumla) ikiwa na mgawanyiko wa ongezeko la dakika 2, 3 mpaka 5.
Kwenye Michezo 15 ambayo Klabu ya Simba iliyocheza kwenye Ligi Kuu msimu huu, waliongezewa Dakika 75 ikiwa na Mgawanyiko wa Ongezeko la Dakika 4, 5 mpaka 7.
“Tunataka Waamuzi wetu waanze kujitafakari juu ya haya ambayo yamekuwa yakiendelea na yamekuwa mjadala mkubwa sana kwenye Taifa letu, Lakini pia tunataja mamlaka zinazosimamia mpira zichukue hatua juu Ya jambo hili ambalo watu wamewekeza pesa zao.
“Hii imetokana na mlolongo wa matukio ya maamuzi yenye utata ambayo Kwa namna moja au nyingine yananyima haki ya timu zingine na yanatoa manufaa Kwa timu zingine.
“Tunaongoza Ligi hii kwa tofauti ya alama 5 tukiwa na matumaini makubwa yakwamba tuna kikosi imara na tunakwenda kushinda ubingwa msimu huu, pamoja na hayo yote Klabu ya Yanga tunapenda kueleza kwamba haturidhishwi na mwenendo wa baadhi waamuzi wanaocheza michezo ya Ligi kuu,” amesema Bumbuli.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Manara: Wachezaji Wameingia na Panadol Sita Sita.​

manara-4.jpg

KLABU ya Yanga imedai kutotendewa haki na baadhi ya maamuzi yanayotolewa na waamuzi wa mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara pamoja na Bodi ya Ligi kwa ujumla kwani wamekuwa wakiegemea upande wa Klabu ya Simba pekee na si kwa vilabu vingine vya ligi hiyo.
Manara amesema hayo leo Jumanne, Faebruari 8, 2022 na Msemaji wa Klabu ya Yanga, Haji Manara wakati akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam kuhusu mwenendo wa uendeshaji wa ligi hiyo inayoendelea.
“Utapaje Quality Players wa kisawasawa, utafuzu vipi AFCON back to back, utakwendaje World Cup kama Ligi unayotegemea uzalishe wachezaji wa Timu ya Taifa inakuwa na malalamiko ya maamuzi kila siku.
“Kuna matukio yasiyopungua 9 mpaka 10 yanayohusisha mechi za Simba ambazo watu wamelalamika kama watu wanavyolalamika kwenye mechi zingine hatuna shida na hilo lakini hiyo humanity iwe kwa timu zote.
“Maamuzi yawe sawa anayekosea aadhibiwe tu, wajibu wetu sisi ni kukumbusha hatulalamiki, hatuwezi kukubali kuona haki haitendeki alafu nikae kimya, tunataka haki itendeke
“Kuna mechi Simba waliomba kutocheza kwasababu wachezaji wao wanaumwa the next day sisi tunacheza Sumbawanga, hakuna mechi ngumu tuliyocheza kama ile ya Prisons wachezaji wameingia wanaumwa lakini tuliambiwa hamjafuata utaratibu jinsi ya kuomba, kina Mwamnyeto na mapanadol sita sita, mchezaji akitoka Half Time anakula Panadol anakula Diclopar.
“Mechi na Biashara, Beki wa Simba kafanya mchezo wa hatari kabisa, nani alichukuliwa hatua? Mechi mmoja Golikipa wao alifanya mambo ya ajabu kabisa lakini hakuchukuliwa hatua, unawezaje kuchukua hatua tukio la Polisi ukaacha tukio la Biashara,” amesema Haji Manara.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Bila Kupepesa Macho, Jerry Muro Awachana Manara na Bumbuli.​

manara-muro.jpg

KIMEUAMANA, hivyo ndivyo unavyoweza kusema! MKUU wa Wilaya ya Ikungi mkoani Singida, Jerry Muro amewataka wasemaji wa klabu ya Young Africans kusoma alama za nyakati na sio kukurupuka na kuzungumza na Waandishi wa Habari.
Jerry Muro ambaye aliwahi kuwa Afisa habari wa Young Africans ametoa ushauri huo kwa wasemaji wa klabu hiyo kwa sasa, ikiwa ni saa kadhaa baada ya kufanyika kwa mkutano na Waandishi wa Habari Makao Makuu ya klabu hiyo leo Jumanne (Februari 08), Jijini Dar es salaam.
Mkutano huo na Wanahabari umefanywa chini ya Afisa Habari wa klabu hiyo kwa sasa Hassan Bumbuli na Msemaji wake Haji Sunday Manara, huku ajenda kuu ikiwa ni kutoridhishwa na mwenendo wa baadhi ya waamuzi waliochezesha michezo yao msimu huu.
Ajenda nyingine katika mkutano huo ilikua ni kulitaka shirikisho la soka nchini TFF kuwachukulia hatua baadhi ya viongozi wa klabu na wadau wengine kama inavyofanya kwa baadhi wa viongozi wa klabu hiyo kongwe katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.
Jerry Muro amesema: “Inashangaza kumsikia Afisa Habari wa klabu akielezea baadhi ya mambo ya msingi ya timu kama shabiki au kuongelea masuala ya ufundi kama kocha wakati kazi hizo si zao.”
“Hata kama klabu zina utaratibu wa kuwapa fursa ya kuzungumza na kutoa ufafanuzi wa mambo yanayoulizwa na waandishi wa habari, lakini wamekuwa wakienda mbali na mipaka yao. Ifike wakati wasemaji wa Yanga waonyeshe ukomavu katika kazi wanazopewa, wasikurupuke na kuonekana vituko.”
Kwa hali hiyo ni dhahir Jerry Muro hajafurahishwa wala kuyapokea yaliyozungumzwa katika mkutano na Waandishi wa Habari uliofanyika Makao Makuu ya klabu ya Young Africans leo Jumanne (Februari 8) jijini Dar es salaam.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Diarra amdatisha hadi Shikhalo.​

DIARRA PIC

KIPA wa KMC, Mkenya Farouk Shikhalo ameweka wazi kuukubali mziki wa kipa mwenzake, Diarra Djigui anayecheza kikosi cha Yanga msimu huu.

Kwa sasa katika Ligi Kuu Bara, Diarra ndiye kipa aliyeruhusu mabao machache akifungwa manne tu, akifuatiwa na Aishi Manula wa Simba aliyetunguliwa sita (kabla ya mechi ya jana).

Akizungumza na Mwanaspoti, Shikhalo alisema Djigui ni kipa wa kisasa mwenye uwezo wa kutumia miguu na mikono kwenye uchezaji wake lakini pia kuanzisha mashambulizi.

“Diarra ni kipa mzuri sana kwa soka la sasa, naweza kusema hawakukosea kabisa kumsajili kwa sababu ni mbadala wangu mzuri kwao Yanga na viongozi walipatia,” alisema Shikhalo na kuongeza;

“Wakati naondoka Yanga licha ya kuwa na sintofahamu lakini nilipokea vizuri cha msingi ni kutakiana kheri kwa sababu mpira ni mchezo wa kuonana mara kwa mara.”

Kipa huyo baada ya kuondoka Yanga msimu amejiunga na KMC ambayo anawania namba na kipa mkongwe Juma Kaseja na yeye ameweka wazi yupo kwenye wakati mzuri akijifunza zaidi.
Shikhalo na Djigui wamepishana langoni msimu huu baada ya mmoja kuingia na mwingine kuondoka kwenda kucheza soka katika timu nyingine.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Mastaa 9 washtukiwa, Nabi awataja...aita kikao kizito fasta.​

Kikosi PIC

KOCHA wa Yanga, Nesreddine Nabi amepania kubeba ubingwa wa Ligi Kuu Bara mapema iwezekanavyo, lakini amechunguza mwenendo wa mastaa wake kiutimamu wa mwili akashtukia kitu.
Wapo kama tisa ambao wanaumia mara kwa mara. Lakini wanaumia majeraha ambayo yamekuwa pia tatizo kwa wengine mara kadhaa.
Nabi ameamua kutumia muda wake wa ziada kuitisha kikao na uongozi pamoja na wataalam wa tiba kuona jinsi ya kupambana na tatizo la wachezaji hao ili wasimtoe kwenye reli ya kuwania ubingwa.
Nabi ameliambia Mwanaspoti kwamba kama kuna kitu kinampasua kichwa ni uwepo wa mastaa wake 9 ambao wanakabiliwa na majeruhi nyakati hizi za hesabu kali. Alisema hadi sasa ingawa ameanza mazoezi kiungo wake Feisal Salum bado hajamuona kama yuko sawasawa sambamba na beki wa kushoto Yassin Mustapha ambaye naye amepata maumivu mara kadhaa.
Wengine ni pamoja na beki Kibwana Shomari,Abdallah Shaibu Ninja na Yacouba Songne ambao walifanyiwa upasuaji nchini Tunisia ambao bado wako katika programu maalum ya kupona huku Yusuf Athuman na beki Dickon Job nao hali zao zikiwa bado ngumu.
“Inaumiza sana kichwa hali hii lakini bado tunapambana kutafuta kujua kipi kinawakumba baadhi yao wameanza kurejea taratibu inatia imani lazima tujue kipi kinasababisha haya majeruhi ya aina hii wakati huu.
“Wapo ambao najua walihitajika kupumzika hapa kati hatukutakiwa kucheza baadhi ya mashindano lakini niliambiwa kwamba haitawezekana hilo nalo linachangia,” alisema Nabi
“Ni muhimu kukutana na kulifanyia tathimini hili tutakutana na viongozi tuweze kutafuta njia ya kuondoka katika eneo hili vinginevyo linaweza kutuharibia hesabu zetu kwenye mambo ambayo tunataka kufanikisha.”
Kwa upande wa Daktari wa Yanga, Shecky Mngazija alisema ni kweli idadi ya majeruhi imeongezeka ndani ya timu baada ya Chrispin Ngushi kugundulika na tatizo ambalo linamuweka nje ya uwanja kwa muda wa wiki sita.
“Matatizo yanayowasumbua wagonjwa ni siri ya daktari na mgonjwa hauwezi kuweka wazi kinachotakiwa kufahamika sasa ni kwamba hatutakuwa na wachezaji hao kwa muda hadi watakapokabidhiwa tena chini ya Nabi,” alisema na kuongeza;
“Ngushi ishu yake ni tofauti na wengine baada ya kubaini tatizo lake imetulazimu kumpa mapumziko ya wiki sita, Nkane na Yassin ameanza mazoezi ya viungo wakati Yacouba, Kibwana na Ninja tayari wameanza mazoezi ya nguvu,” alisema Mngazija ambaye ni miongoni mwa madokta wazoefu.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Mayele Awatuliza Yanga, Aahidi Neema.​

yanga-3.jpg

MSHAMBULIAJI wa Yanga, Fiston Mayele, ambaye ndiye kinara wa utupiaji katika klabu hiyo akitupia sita,
amewaondoa presha mashabiki wa timu hiyo kwa kusema kuwa watulie kwani mambo mazuri yanakuja.
Hiyo imekuja mara baada ya Yanga kutoka suluhu dhidi ya Mbeya City katika mchezo uliopita wa ligi na hivyo kupunguzwa pointi dhidi ya watani zao, Simba kutoka 10 hadi tano.
Akizungumza na Championi Jumatano, Mayele alisema kuwa, kupata suluhu katika mchezo uliopita isiwe sababu ya mashabiki kuona watashindwa kuyatimiza malengo yao msimu huu ambayo ni ubingwa na kuahidikuwa bado watapambana kwa hali na mali kuhakikisha kuwa wanatimiza ahadi hiyo.
“Mashabiki wasiwe na wasiwasi na sisi kwani bado tupo katika mapambano ya kuhakikisha kuwa malengo yetu yatatimia msimu huu kuhakikisha kuwa tunatwaa ubingwa, hivyo wanatakiwa kutupa sapoti kila mara bila kuchoka ili tuendelee kusonga mbele.
'Michezo bado ni mingi sana kama ambavyo imeonekana na sisi kama wachezaji tunatakiwa kupambana bila kuchoka kwani kwenye nia pana njia siku zote na sisi tunayo nia kweli kuhakikisha kuwa mashabiki wanapata furaha ambayo wameikosa kwa muda mrefu,” alisema Mayele.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Yanga Yaitengea Mtibwa Siku 15.​

yanga-2.jpg

KIKOSI cha Yanga, kimeitengea Mtibwa Sugar siku 15 za kuhakikisha zinaibuka na ushindi katika
mchezo wa Ligi Kuu Bara unaotarajiwa kuchezwa Februari 23, mwaka huu kwenye Uwanja wa Manungu,
Morogoro.
Yanga wametamba kuwamaliza Mtibwa wakiwa kwao huku wakiwa na kumbukumbu ya kuishuhudia Simba
ikitoka suluhu ilipokwenda kucheza huko hivi karibuni.
Katika msimamo wa Ligi Kuu Bara hivi sasa, Yanga wanaongoza wakiwa na pointi 36, huku Mtibwa ikiwa na pointi 12 katika nafasi ya 14. zote zimecheza mechi 14.
Akizungumza na Championi Jumatano, Winga wa Yanga, Dickson Ambundo, amesema: “Maandalizi yetu
yapo vizuri kuelekea mchezo huo, tumepata muda wa kupumzika wa kutosha, sasa ni muda wa kujipanga kuwamaliza Mtibwa.
“Kwaupande wangu nimejipanga kupambana kwa hali ya juu ili kuweza kuisaidia timu yangu kupata matokeo
mazuri, ukiangalia tulipata matokeo ya sare kwa mchezo uliopita na mchezo huu tunataka matokeo ya ushindi.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Nabi Atakiwa Kuwasilisha Ripoti Yanga.​

yangasc_249408202_1159546137913421_4384637946363514116_n.jpg

HATIMAYE Uongozi waYanga, umelitaka benchi la ufundi la timu hiyo, linaloongozwa na kocha raia wa Tunisia, Nasreddine Nabi, kuwasilisha mara moja ripoti ya mpango kazi unaoainisha mambo watakayoyafanya takribani wiki mbili za mapumziko kabla mechi za Ligi Kuu Bara kurejea.
Yanga bado ni vinara wa ligi, wakiwa na jumla ya pointi 36, walizozipata baada ya kucheza mechi 14 na kuvuna ushindi katika mechi 11, huku wakitoka sare tatu.
TayariYanga ipo kambini ikiendelea kujinoa kwa ajili ya mchezo wao wa Kombe la Shirikisho laAzam Sports, ambapo Februari 15 watakuwa wenyeji wa Biashara United, mchezo utakaopigwa katika Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam.
Chanzo chetu kutoka ndani yaYanga, kimeliambia Championi Jumatano kuwa, uongozi umelita benchi la ufundi kupitia kwa mratibu wa mashindano, Thabit Kandoro
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

DJIGUI DIARRA TAYARI KUREJEA KAZINI YANGA NA BIASHARA.​

AVvXsEgfJt8-veLA1GWBmVJ_PuAXq7nQ8LaruVHlqqhdBmDrQlVw5opxxeCPWo4eKllQkMQ3D7IKECpbEkvFtC-OVHaLes7ZDpf7OwQmhP2A9aJjFwTT5nkvJxHIp8Gtb8pYpUT_2gzUolBmyWQBJtDwsNDEepUZm2GaUtX5yOGM7xoRSRhiKgsZub-iRfiK=w640-h634

MLINDA mlango wa kimataifa wa Mali, Djigui Diarra akiwa mazoezini na klabu yake, Yanga SC baada ya kurejea nchini kutoka nchini Cameroon alipokuwa na timu yake ya taifa kwa ajili ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zilizomalizika Jumapili kwa Senegal kuwa mabingwa.
AVvXsEiCLRIiS8eVkjfswPFg8i-am85giJZXYD9HZZBwiB1aCFJARknNar082T-uVxLfRkJxByGYYZnJzg4gPtXClJyc8K9TNf4Gzm9mbJy4ZYor81r9YSwiQtgNhMYKEcaAprAjDEJpk_QjVEFc6GRYNcU2zA6kYtIq_Kks96droNpITw_Ycre7AWX4ZP-9=w640-h634

Baada ya kukosekana tangu mwishoni mwa Desemba, Diarra anatarajiwa kuonekana tena kazini Yanga ikimenyana na Biashara United katika mchezo wa Hatua ya 16 Bora Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) Jumanne Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Yanga dozi nene, mastaa wapikwa upya.​

dozi pic

KOCHA Mkuu wa Yanga, Nasreddine Nabi amebadili programu yote ya mazoezi ya timu hiyo kuanzia asubuhi ya leo. Tofauti na awali ambako mastaa wa timu hiyo walikuwa wakipiga matizi mara moja tu kwa siku sasa wametangaziwa utaratibu mpya ambapo watalazimika kupasha mara mbili kwa siku. Asubuhi wataamkia kwenye mazoezi ya gym kwenye viwanja ghali vya Gymkhana na jioni watakiwasha Avic Town Kigamboni.
Nabi anasema kwamba lengo la mazoezi hayo ni kurudisha utimamu wa miili ya wachezaji hao kuendana na mechi inayofuata ambayo ni dhidi ya Biashara kwenye Kombe la Shirikisho la Azam Sports (ASFC) wiki ijayo.
Kocha huyo aliyeanza kuzungumza maneno kadhaa ya Kiswahili, amesisitiza kwamba anataka wachezaji wake wakirejea uwanjani wawe na kiwango kikubwa na wasiache pointi hata moja.
Alisema kwamba watasimama mazoezi hayo ya nguvu siku chache kabla ya mechi hiyo ili wachezaji wakae sawa tayari kukiwasha kwenye mechi hizo ngumu za kimkakati ambazo hawapaswi kupoteza hata moja kwani wanataka kurejesha hadhi ya Yanga kwa kukusanya makombe mengi msimu huu.
Nabi ameliambia Mwanaspoti kwamba anataka ushindani katika kikosi chake lakini kuhusu winga wake mpya Denis Nkane ambaye hajaonekana muda mrefu ni kwamba ana maumivu lakini mbali na kuwa majeruhi kuna shida ameigundua.
Alisema bado hajaridhishwa na mwanzo wa Nkane ndani ya kikosi chake na amekutana naye na kumwambia ana deni kubwa ndani ya jezi za klabu hiyo.
Kocha huyo alisema Nkane bado ni kijana mdogo na kwamba kama atajiona ni staa mkubwa ni rahisi kupotea ndani ya kikosi hicho.
“Napenda kufanya kazi na vijana, unajua vijana wana nguvu, najua ana maumivu lakini bado sijaridhika na mwanzo wake katika timu nafikiri sasa atakuwa amenielewa.
“Alianza vizuri lakini baada ya kufunga kule Zanzibar kuna aina ya maisha ya kuridhika yamemuingia akilini, hii sio nzuri kwake nimemwambia yeye (Nkane) bado ni mchezaji mchanga asidhani ni staa mkubwa.
“Yanga imemuamini kuja hapa, anachotakiwa ni kutihibitisha kwamba sisi makocha hatukukosea kumleta hapa, anatakiwa kupigania namba kwa nguvu na sio kuwa wa kawaida tena.
“Nimemwambia wakati huu ana maumivu ajiandae kiakili ili akirudi tu awe Nkane tofauti anayekuja kupigania nafasi na sio kuridhika kuwaona wenzake wakicheza,” alisema Nabi.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Diarra kuanza na Mtibwa Manungu.​

diarra pic

KIPA namba moja wa Yanga, Djigui Diarra baada ya kukosekana kwenye mechi nne za Ligi Kuu Bara sasa anatarajia kuanza dhidi ya Mtibwa Sugar katika mechi itakayopigwa Februari 23 kwenye Uwanja wa Manungu sambamba na beki Djuma Shaban.
Diarra aliyekuwa nje ya uwanja kutokana na kujumuishwa kwenye kikosi cha timu yake ya taifa ya Mali, amerejea nchini baada ya timu yake kutolewa huku Djuma alikuwa akitumikia adhabu yake ya kufungiwa mechi tatu kutokana na kumfanyia mchezaji mwenzake mchezo usio wa kiungwana.
Wakati mpango wa wawili hao kurudi uwanjani umeiva, kipa namba mbili aliyekuwa anaibeba Yanga wakati Diarra yupo Afcon, Aboutwalib Mshery anatarajia kucheza mechi yake ya mwisho Februari 15, wakati Yanga itakapoivaa Biashara United katika mechi ya 16 Bora ya Kombe la Shirikisho (ASFC).
Mshery ambaye amedaka mechi nne hadi sasa za Ligi Kuu ambazo ni sawa na dakika 360 bila kuruhusu bao, anatarajia kumalizia dakika 90 za mwisho kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) Jumanne ijayo dhidi ya Biashara United.Chanzo cha ndani ya timu hiyo kililiambia Mwanaspoti, kuwa Mshery ni mgonjwa na kwa mechi kadhaa amekuwa akicheza na maumivu lakini ni mpambanaji na aliomba acheze mechi ya Mbeya City na Biashara United ambayo ni ya shirikisho ili kuondoa maneno kwa mashabiki na wadau wa soka kwamba ameanza kukosa nafasi baada ya Diarra kurudi.
“Mshery anaumwa lakini ni mpambanaji na alikuwa akicheza na maumivu ndio maana aliomba aendelee kuonyesha ubora wake dhidi ya Mbeya City na Biashara Februari 15 na baada ya hapo langoni atakaa Diarra wakati kipa namba mbili anaendelea kujiuguza na kupata mapumziko kwa muda,” kilisema chanzo hicho.
Gazeti hili lilimtafuta daktari wa timu, Dk Shecky Mngazija ambaye alithibitisha kipa huyo kupata tatizo ambalo aliliweka wazi kuwa halikuwa kubwa wamelifanyia kazi haraka na ndio maana alionekana uwanjani.
“Yanga ina majeruhi kama Kibwana Shomari, Yacouba Sogne na Abdallah Shaibu ‘Ninja’ ambao wapo chini ya daktari wa viungo. Mshery alicheza dhidi ya Mbeya City leo mnauliza hali yake, inakuwaje mgonjwa apewe nafasi ya kucheza?” alihoji.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Krosi za mabao zimerudi Yanga.​

krosi pic

KIWANGO cha Yanga dhidi ya Mbeya City kimemkera Kocha Nasreddine Nabi, lakini akasisitiza kwamba baada ya mechi yao na Biashara wana jambo lao.
Kocha huyo ambaye tangu juzi amewarejeshea mastaa wake programu nzito ya mara mbili kwa siku, ametamba kwamba wanarudi na staili yao ya krosi za kasi na mabao na wataanza kuonyesha makali hayo kwenye mechi na Mtibwa kumalizia mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu huku Manungu, Turiani.
Alisema ujio beki wake Mkongomani Djuma Shaban anayecheza beki ya kulia kwenye mechi na Mtibwa utakuja sambamba na staili mpya ambazo wamezifanyia kazi mazoezini kwenye siku hizi chache kuhakikisha Yanga inarejesha makali yake. Djuma alikosa mechi tatu zilizopita akiwa amesimamishwa kwa kumpiga kiwiko beki wa kulia wa Polisi Tanzania, Yahaya Mbegu katika mchezo wa ligi wiki chache zilizopita.
Tangu kusimamishwa kwa Djuma, Yanga imekuwa ikiwatumia mabeki Paul Godfrey ‘Boxer’ katika mechi moja ya Shirikisho huku ile ya ligi akicheza Dickson Job ambao wote Nabi hakuonyesha kuridhishwa na ufanisi wao kwenye staili yake ya uchezaji.
Nabi amegundua kwamba katika mchezo wa Mbeya City, Job ambaye halisi anacheza beki wa kati lakini alishindwa kupiga hata krosi kutokea pembeni.
Mbali na Djuma pia beki wa kushoto, Yassin Mustapha, Nabi alisema kwamba anaweza kuwa tayari kucheza kufikia wiki ijayo wakiwafuata Mtibwa Sugar kule Manungu ambako amesisitiza watapambana kwa namna yoyote.
“Djuma na Yassin wana ubora mkubwa wa kupita pembeni na kutengeneza krosi za kutosha, hii ni nguvu ambayo katika mechi kadhaa zilizopita tumeikosa na sasa watarudi,” alisema Nabi na kuongeza;
“Tulikuwa na ubora mdogo katika kuzalisha mashambulizi katika maeneo hayo hili lilitukwamisha sana ingawa nawapongeza waliocheza kwa kuwa tulizuia vizuri na hatujaruhusu bao wala kupoteza hili ni kubwa nalo.”
Nabi alisema alipanga kufanyia kazi aina ya timu ambazo hucheza na wachezaji wengi nyuma ya mpira na kwamba kurejea kwa wachezaji hao kutatengeneza nguvu mpya ya kuwa na mbinu mbadala katika kuzalisha mashambulizi.
“Timu nyingi kama Mbeya City wanajua nguvu yetu kubwa ni kuwa bora kutoka eneo la katikati ya uwanja sasa tukiwakosa watu bora wa kutengeneza mashambulizi tukitokea pembeni tutakuwa na akili mbadala ya kutafuta ushindi,” alisema Nabi akisisitiza bado wako kwenye kasi nzuri na mzunguko wa pili wataingia na nguvu kubwa.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Yanga inabeba hivi ubingwa.​

ubingwa pic

IKIWA zimechezwa raundi 14 za Ligi Kuu Bara mambo yameanza kupamba moto, na hiki ndicho kipindi ambacho kila timu inakaa mguu sawa ili kumaliza vizuri msimu.
Vita kwenye ligi imeanza kugawanyika kwenye sura tatu ya kwanza ipo kwenye mbio za ubingwa ambazo zimeanza kupamba moto, vita nyingine ni ya timu ambazo zinalenga kumaliza kwenye nafasi za juu ikiwemo nne bora.
Vita ya mwisho ni kusalia Ligi Kuu na hii ni kati ya vita ngumu kwelikweli. Timu mbili ambazo zitamaliza msimu zikiwa mwishoni mwa msimamo zitashuka daraja moja kwa moja huku nyingine mbili zikikabiliwa na kibarua cha kucheza mechi za mchujo kusalia dhidi ya timu za Championship, ambapo shughuli huwa ni pevu.
Licha ya kuwa bado ni mapema, vipo viashiria ambavyo vinaibeba Yanga na kuiweka kwenye mazingira mazuri ya kutwaa ubingwa msimu huu. Hapa tunaigusa vita ya ubingwa ambayo imeanza kupamba moto. hata hivyo, hakuna mwenye uhakika wa kutwaa ubingwa hadi sasa licha ya uwepo wa viashiria hivi kutokana na idadi ya michezo iliyosalia.

UPANA WA KIKOSI
Licha ya kukosa huduma ya wachezaji kadhaa kwa vipindi tofauti, Yanga imeonekana kuwa na kundi kubwa la wale ambao wamekuwa wakibebeshwa majukumu ya kuziba pengo la wenzao. Mfano mzuri ni hivi karibuni Yanga iliondokewa na kipa namba moja, Djigui Diarra aliyeenda Cameroon na timu ya taifa ya Mali kushiriki Fainali za Mataifa ya Afrika (Afcon 2021).
Hata hivyo, uwepo wa Aboutwaleeb Mshery uliifanya timu hiyo kutokuwa na pengo. Mshery alionyesha kiwango kizuri tangu ajiunge na timu hiyo akitokea Mtibwa Sugar wakati wa dirisha dogo la usajili na kipa huyo amekuwa mzuri kuanzisha mashambulizi kitu ambacho amekuwa akikifanya Diarra kiasi cha kutabiriwa mazuri.
Achana na eneo la golini safu ya ulinzi ya Yanga wakati huu ambao anakosekana Kibwana Shomary upande wa beki ya kushoto yupo Yassin Mustapha na David Bryson. Kukosekana kwa Feisal Salum kwenye michezo kadhaa iliyopita wameonekana wengine wakifanya vizuri akiwemo Saido Ntibazonkiza.

POINTI, REKODI
Japokuwa Yanga inaongoza msimamo wa ligi ikiwa na pointi 36, tofauti ya pointi iliyopo baina yao na Simba ambao wapo nafasi ya pili ni tano huku Wekundu wa Msimbazi wakiwa na pointi 31 kwenye michezo 15.
Ingawa ni pointi chache, lakini ni kati ya ishara ambazo zinaifanya Yanga kuonyesha kuwa imepania kubeba ndoo msimu huu, ikizingatiwa kwamba ni hivi karibuni kulikuwa na pengo la pointi 10 kati yao na watani wao hao, Simba.
Msimu uliopita kulikuwa na tofauti ya pointi nyingi baina ya timu hizo mbili, lakini kitendo cha Simba kuwa na idadi kubwa ya viporo kiliiangusha Yanga ambayo hata hivyo ilipoteza mwelekeo kwenye michezo dhidi ya Coastal Union ya Tanga ambao walipoteza kwa mabao 2-1 na dhidi ya Polisi Tanzania kwa satr ya 1-1.
Hii ni ishara tosha kuwa Yanga msimu huu inautaka zaidi ubingwa kuliko ilivyokuwa msimu uliopita ambapo walishuhudia Simba ikiutwaa kwa mara ya nne mfululizo.
Hadi raundi 14 ilizocheza Yanga imepoteza pointi sita tu kwenye michezo mitatu ambayo imetoka sare ambayo ni dhidi ya Namungo sare ya bao 1-1, Simba na Mbeya City zilizoisha kwa suluhu.

NGOME IMARA
Kati ya sifa za timu inayoweza kutwaa ubingwa ni pamoja na kuwa na safu imara ya ulinzi. Hii ina maana kuwa kama washambuliaji watashindwa kufunga, basi isiruhusu bao ili kuondoka uwanjani ikikusanya pointi hata kama ni moja. Ndani ya michezo 14 ambayo Yanga imecheza imeruhusu mabao machache zaidi - manne pungufu ya timu nyingine yoyote. Mabeki Bakari Mwamnyeto, Dickson Job, Shaaban Djuma, Yannick Bangala, Kibwana, Yassin na Bryason wamefanya kazi nzito na bado wanalo jukumu la kuhakikisha wanafikia lengo.

MABAO MENGI
Kasi ya ufungaji ya Fiston Mayele imestua tangu straika huyo alipotua Yanga ambapo amekuwa tishio akiifanya timu kuwa bora kwenye safu ya ushambuliaji tofauti na msimu uliopita. Yanga ndiyo timu iliyofunga mabao mengi zaidi kwenye ligi hadi sasa ikifunga 23, huku Mayele akitupia sita. Mbali na uwepo wa mshambuliaji huyo, kocha Nasreddine Nabi ana wigo mpana wa kufanya vizuri akiwa pia na mastaa wengine wanaombeba katika utupiaji kama Feisal Salum ‘Fei Toto’ na hata Ntibazonkiza.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

Miaka 87 kupanda na kushuka kwa Yanga.​

Yanga PIC

KLABU ya Yanga iliyopo chini ya Mwenyekiti Dk. Mshindo Msolla na timu yake leo Februari 11 imefikisha miaka 87 tangu ilipoanzishwa rasmi mwaka 1935, huku ikiwa na mafanikio kedekede ya kujivunia na kukumbukwa.

Mabingwa hao wa kihistoria katika Ligi Kuu ya Bara ikiwa imebeba taji la ligi hiyo, hilo mara 27 huku wapinzani wao Simba ikibeba mara 22.

Yanga msimu huu ni kama imezaliwa upya kutokana na usajili walioufanya baada ya kukosa ubingwa kwa misimu minne mfululizo, ikipewa nguvu kubwa na GSM, Sportpesa, Taifa Gas, na wadhamini wa Ligi NBC na Azam Media.

Timu hiyo imetoa wachezaji wenye majina makubwa na mafanikio kama Boniface Mkwasa, Sunday Manara ambaye ndio alikuwa mchezaji wa kwanza Tanzania kucheza soka kulipwa nje mwaka 1978 kwenye ligi ya Uholanzi.

Wananchi ndio timu ya kwanza Tanzania kushiriki michuano ya kimataifa ya CAF, ikicheza Klabu BIngwa Afrika mwaka 1969 na kufika robo fainali ikitolewa na Asante Kotoko ya Ghana na kurudia tena 1970.
Yanga PIC1

Pia ndio klabu ya kwanza nchini kufuzu hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika mwaka 1998 baada ya kubadilishwa mfumo 1997 na Kombe la Shirikisho Afrika 2016 na 2018 baada ya kumaliza nafasi za mwisho katika makundi na kuondolewa kwenye mashindano hayo.
Kundi A ambalo lilikuwa na timu za Yanga, TP Mazembe, Mo Bejaia na Madeama SC mnamo mwaka 2016 ambapo Yanga ilifanikiwa kushinda mchezo mmoja, sare 1 na vipigo mara 4.
Lakini haikuishia hapo Yanga ndio timu inayoongoza kuliwakilisha taifa la Tanzania kwenye mashindano ya kimataifa ikiwa ni Klabu bingwa Afrika, Kombe la Shirikisho Afrika na kombe la Kagame.
Ikumbukwe Yanga ndio timu pekee nchini imefanikiwa kutwaa mataji ya Kombe la Kagame nje ya ardhi ya Tanzania ikifanya hivyo, 1993 na 1999 nchini Uganda huku ikitwaa kombe hilo mara 5.

Mafanikio ya Yanga toka imeanzishwa

  • Kombe la Ligi Kuu Bara-27
  • Kombe la FA-5
  • Kombe la Kagame-5
  • Kufika robo fainali klabu bingwa Afrika-1969 na 1970
  • Kufuzu hatua ya Makundi kombe la Shirikisho Afrika-2016 na 2018.
 

Amir

Mgeni
Dec 10, 2021
736
12
5
tanzania

BUMBULI NA MANARA WAPIGWA FAINI KILA MMOJA.​

AVvXsEiMuwdQIetkHtjkEF_L6VlfmnOL6o3_wOBDdpoPfMSg99iywX0B-HcZTTHGTT4wusE0El7ZSNR8RAkEb2283PqfSA_adFQHL4c8Res_UNfewtBsgVmwFyr7iDrtUP_vW1HBcoalkMUwAPC091khETtkpTlPxoQYv6p_oyLmoPJEHQ4XToKIm9JvdikD=w640-h606

MAAFISA Habari wa Yanga SC, Hassan Bumbuli na Haji Manara kila mmoja ametozwa faini ya Sh. 500,000 kwa kosa la kuwashutumu marefa kwenye vyombo vya Habari Februari 8, mwaka huu.
AVvXsEj6Ll8jHB04es10YZo83DH34AaFflp5H2tOc59jQfLs4VPiTZh37PpBVqnI7T-18ewNOO_rQgMmelaKXq7w9q9arp8NUM5Qal69QAocomQ4TSWodbIEn0UbUmEmrosmS60sWJVXsulQRDOIckFAC4GR3y2kSTwjRh_u3XtzQuDmt6MtDYczFYBJ5Nc_=w512-h640
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Yanga Washtukia, Wamuonya Mayele.​

mayele.jpg

MABOSI wa Yanga ni kama wameshtukia vile, unaambiwa juzi walimuita straika wao Fiston Mayele kufanya naye kikao na kumuonya kuhusu suala la kuzungumza na waamuzi pamoja na kupunguza jazba kila anapokuwepo uwanjani.
Hiyo ni kutokana hofu ya kutafutiwa kadi za makusudi zitakazomsababishia kufungiwa na kuikosa michezo muhimu ya Ligi Kuu Bara na Kombe la Shirikisho la Azam Sports (ASFC) msimu huu.
Mayele, mwenye mabao sita, anachuana vikali katika ufungaji bora na mshambuliaji wa Namungo FC, Reliants Lusajo aliyefunga tisa.
Mmoja wa mabosi wa Yanga, ameliambia Championi Ijumaa kuwa adhabu ya beki wa pembeni Mkongomani, Shaaban Djuma ndiyo imeshitusha na kufanya naye kikao kwa hofu ya yeye kukutana na adhabu hiyo wakati yeye ndiye mshambuliaji tegemeo.
Bosi huyo alisema kuwa wameshitukia mabeki wa timu pinzani kuwapania washambuliaji wao na kuwachezea rafu za makusudi kwa lengo la kuwakasirisha halafu warudishie ili wapewe kadi na kufungiwa kama ilivyotokea kwa Djuma.
Aliongeza kuwa mshambuliaji huyo ameshauriwa kupunguza jazba na kuwapuuza mabeki wa timu pinzani wenye lengo la kumtoa mchezoni kwa kumchezea vibaya.
“Mayele mwenyewe uzuri ameshajua kila kitu kinachoendelea juu ya mabeki wa timu pinzani wenye lengo la kumtoa mchezoni kwa kumchezea rafu za makusudi huku wakitumia nguvu nyingi katika kumkaba.
“Hivyo kutokana na umuhimu wake, Mayele katika timu anapokuwepo uwanjani, haraka uongozi umemuita kwa ajili ya kufanya naye kikao kizito.
“Katika kikao hicho pia walikuwepo baadhi ya wachezaji tegemeo katika timu ambao wanapaniwa kila wanapokuwepo uwanjani na wachezaji wa timu pinzani,” alisema bosi huyo.
Akizungumzia hilo, Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Frederick Mwakalebela, alisema: “Tunafahamu kila kitu kuhusiana na hujuma zinazofanywa na wachezaji wa timu pinzani zenye lengo la kuwatoa mchezoni wachezaji wetu.
“Wachezaji wetu wanachezewa rafu za makusudi kutokana na kupaniwa na wanafanya hivyo kwa lengo la kutaka kulipiziwa pale wanapowachezea wachezaji wetu kama ilivyotokea kwa Djuma, hivyo tayari tumewaonya wachezaji wetu.”
Mayele naye hivi karibuni aliwahi kusema: “Mabeki wa timu pinzani walishaniona mimi ndiyo tishio katika timu, hivyo wanacheza kwa kutumia nguvu nyingi kila ninapokuwa nina mpira.
“Tayari nimeongea na kocha wangu Nabi (Nasreddine) kwa ajili ya kuniongezea mazoezi ya binafsi ya nguvu ili nitakapokutana nao niweze kupambana nao.”
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Kocha Yanga Awasifu Makipa Wake “Wote Wako Vizuri.​

makipa-yanga.jpg

KOCHA wa Makipa wa Yanga, Mikton Nienov amewasifu makipa wake, Djigui Diarra, Aboutwaleb Mshery na Erick Johora wotw kwa pamoja wanafanya vizuri na kuisaidia timu yao.
“Namshukuru Mungu kwa timu yetu kuwa na walinda milango mahiri ambao hawajapishana sana viwango vyao. Kazi yetu benchi la ufundi, ni kuboresha viwango vyao, kuvikuza, kulinda na kuweka ushindani ndaji yao ili kuleta matokeo chanya kati yao na timu kwa ujumla.
“Tupo katika FA na ligi kuu na malengo ya klabu ni kufanya vyema kwenye ligi zote, hivyo ni lazima kumsaidia kocha mkuu kuandaa wachezaji wote katika ubora mzuri ili awe na uwanja mpana wa kuwatumia.
“Kuna injury, national call ups, cards, matatizo binafsi, kushuka kiwango, hivyo kama hutakuwa na wachezaji wazuri wenye kuendana viwango kila idara, itakuwa ngumu kushindana na wenzako wenye depth kubwa kwenye selection ya wachezaji,” amesema Milton.
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Nabi aja na mbadala wa Mayele.​

MAKAMBO-MAYELE-NABI.jpg

KOCHA Mkuu wa Yanga, Nasreddine Nabi, amemuangalia mshambuliaji wake Fiston Mayele akipaniwa na kutolewa macho na mabeki wa timu pinzani, haraka amechukua maamuzi magumu ya kumuingiza kikosini Chico Ushindi.
Hiyo ikiwa ni siku chache tangu Mayele kutamka kuwa anapaniwa na mabeki wa timu pinzani huku wakimuangalia yeye pekee baada ya kugundua ni mchezaji hatari katika timu.
Awali kocha huyo alikuwa akimuanzisha benchi Chico katika michezo ya Ligi Kuu Bara na kumuingiza kipindi cha pili akipewa dakika chache baada ya kukosa mechi fitinesi ambayo tayari ameiongeza mazoezini.
Mmoja wa viongozi wa Benchi la Ufundi la Yanga, ameliambia Championi Jumamosi kuwa ili wawavuruge mabeki wa timu pinzani, Nabi ameona ni vyema akamuanzisha Chico katika kikosi chake cha kwanza kutokana na uwezo wake mkubwa wa kufunga na kutengeneza mabao katika mechi.
Kiongozi huyo alisema kuwa Nabi katika kikosi chake anataka wawepo wachezaji hatari wa kuogopwa na mabeki wa timu pinzani kama ilivyo kwa Mayele.
“Kocha anataka kuwa na washambuliaji wenye uwezo wa kufunga na kutengeneza mabao ambao pia ni hatari kwa mabeki wa timu pinzani.
“Nabi anaamini kuwa kama Chico akianza katika kikosi chake cha kwanza, basi namba ya mabeki wa kumkaba Mayele itapungua tofauti na ilivyokuwa hivi sasa katika timu akimtumia Moloko kama winga wa kulia.
“Alichopanga kocha ni viungo wawili wa pembeni wacheze Chico na Saido (Saidi Ntibanzonkiza) huku namba 10 akiwa Fei Toto (Feisal Salum) na 9 awe Mayele, wachezaji wote hao wana uwezo wa kufunga na kutengenezeana mabao,” alisema kiongozi huyo.
Nabi hivi karibuni alimzungumzia Chico na kusema kuwa: “Wachezaji wangu wote wana nafasi za kucheza na Chico nimeshindwa kumtumia katika kikosi cha kwanza kutokana na kutokuwa na mechi fitinesi.
“Nashukuru hivi sasa yupo fiti kabisa, tayari kwa ajili ya kupambana ndani ya uwanja baada ya kumuongezea mechi fitinesi iliyopotea baada ya kukaa nje ya uwanja muda mrefu kutokana na majeraha.”
 

vuligate

Mgeni
Dec 17, 2021
395
3
5

Nabi Amuandaa Djuma Kuwamaliza Mtibwa Sugar.​

DJUMA.jpeg

RASMI beki wa pembeni wa Yanga, Mkongomani, Djuma Shaban ataanza kuonekana katika mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar ya Morogoro ikiwa ni baada ya kumaliza adhabu yake ya kufungiwa mechi tatu.
Mkongomani huyo hivi karibuni alisimamishwa kucheza michezo mitatu ya Ligi Kuu Bara na faini baada ya kumpiga kiwiko mchezaji wa Polisi Tanzania.
Djuma anamaliza adhabu hiyo baada ya kukosa michezo ya ligi dhidi ya Mbeya City na miwili ya FA ambayo ni Mbao FC kabla ya kumalizia na Biashara United, Jumanne ijayo kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar.
Akizungumza na Championi Jumamosi, Kocha Mkuu wa Yanga, Nasreddine Nabi, alisema ameanza kumuingiza beki huyo katika mipango yake ya mchezo ujao wa ligi baada ya kuikosa michezo miwili huku akisubiria dhidi ya Biashara ambao atakuwa anamalizia adhabu yake.
Aliongeza kuwa, hivi karibuni alifanya kikao na beki huyo na kumtaka kupunguza jazba za ndani ya uwanja mara baada ya kuchezewa vibaya na wachezaji wa timu pinzani.
“Wachezaji wangu karibia wote wanachezewa vibaya kwa kupaniwa na wachezaji wa timu pinzani, hivyo nisingependa kuwaona wakiwa na jazba mara baada ya kuchezewa vibaya kwa kurudishia.
“Nilishamuonya Djuma kutorudishia rafu atakazokuwa anachezewa na wachezaji pinzani kwa hofu ya kupewa adhabu kama aliyoipata ambayo inaigharimu timu katika kupata matokeo mazuri ya ushindi,” alisema Nabi.